Tunalihitaji Kutaniko
1 Wana wa Kora walionyesha uthamini wao kwa kutaniko la Yehova kwa maneno haya: “Siku moja katika viwanja vyako inapita elfu moja [kwingine].” (Zab. 84:10) Kwa maoni yao, ulimwengu haukuwa na chochote cha kutolea watu chenye kulingana na hilo. Ikiwa wewe pia unajisikia kama wao, ungepaswa kufanya kutaniko la Kikristo lichukue sehemu ya maana katika maisha yako.
2 Tangu mianzo yalo, kutaniko la Kikristo linafaidika kwa wazi na baraka ya kimungu. (Mdo. 16:4, 5) Kusiwe hata mmoja kati yetu ambaye angeliona kama kitu chenye maana ndogo au kulichukua kuwa tu njia ya kukutanika pamoja. Kutaniko ni kitovu chenye kurudisha nguvu cha Mashahidi wa Yehova wa kila mahali. Tunakusanywa huko katika umoja ili tufundishwe na Yehova na kutayarishwa kwa ajili ya utendaji wa Ufalme.—Isa. 2:2.
3 Kutaniko la Kikristo ndiyo njia kuu kupitia kwayo sisi tunafundishwa kweli. (1 Tim. 3:15) Wanafunzi wa Yesu wanapaswa ‘wote kuwa mmoja,’ kuwa na umoja na Mungu, na Kristo, na pia kila mtu na mwenziwe. (Yn. 17:20, 21; Ona pia Isa. 54:13.) Mahali pote ulimwenguni, ndugu zetu Wakristo wanaamini mafundisho na kanuni za kibiblia na wanaishi kulingana nazo.
4 Sisi tunazoezwa na kupewa vifaa ili kutimiza kazi yetu ya kufanya wanafunzi. Kila mwezi, Mnara wa Mlinzi, Amkeni! na Huduma Yetu ya Ufalme vinatoa mashauri yenye kufaa ili kuanzisha mazungumzo ya kibiblia. Mikutano inalo kusudi la kutuonyesha namna gani kuvumbua na kuchochea kupendezwa kwa watu. Ongezeko linaloripotiwa ulimwenguni kote linaonyesha tegemezo la kimbinguni ambalo kazi hii inapata.—Mat. 28:18-20.
5 Kwa njia ya kutaniko, sisi ni wenye ‘kuchochewa kwenye upendo na kazi zilizo nzuri’ kila siku.’ (Ebr. 10:24, 25) Tukiwa wenye kutiwa nguvu, tunavumilia kwa uaminifu yale majaribu. Waangalizi walio wema wanatusaidia kupambana na mikazo na mahangaiko. (Mhu. 4:9-12) Ikiwa tunataka kwenda kando, tunapokea mashauri yenye kufaa. Je! kuna tengenezo lingine linalotoa msaada wa upendo kama huo?—1 Tes. 5:14.
6 Yehova anapenda tubaki karibu na tengenezo lake ili umoja wetu ulindwe. (Yn. 10:16) Kutaniko linatusaidia kuchunga upashanaji habari na mtumwa mwaminifu kwa kututolea kwa mfano waangalizi wasafiri ambao hutumwa ili kututia moyo. Kwa kuitikia kwetu vizuri mpango mwema huo, sisi tunakaribiana na wengine, na hilo linatusaidia kubaki nguvu kiroho.
7 Kutaniko ni mpango wa lazima sana kwa kuokoka kwetu kiroho. Bila hilo, haingewezekana kumtumikia Yehova sawasawa. Basi tubaki karibu na njia hii iliyowekwa na Yehova. Tushirikiane nalo katika miradi linayofuatia na tutumie bila unafiki mashauri ambayo tunapokea kutoka kwalo. Ni kwa kufanya hivyo tu kwamba sisi tutaonyesha uthamini wetu kuhusu kutaniko.—Zab. 27:4.