Kisanduku Cha Maulizo
◼ Kuna faida gani kuhudhuria katika kutaniko linalogawiwa eneo tunamoishi?
Kupitia mpango wa kutaniko, tunapata kitia-moyo ‘kinachotuchochea kwenye upendo na kazi zilizo bora.’ (Ebr. 10:24, 25) Kupitia kutaniko tunajifunza kweli na tunaandaliwa vifaa ili kutimiza mgawo wetu wakufanya wanafunzi. (Mt. 28:19, 20) Pia tunatiwa nguvu kuvumilia majaribu kwa uaminifu na tuna waangalizi wenye upendo wanaotusaidia tupambane na mikazo mikubwa na pia mahangaiko kwa matokeo . Bila shaka, kutaniko ni la maana kwa wokovu wetu wa kiroho. Hata hivyo, je, kuna faida katika kuhudhuria katika kutaniko linalogawiwa eneo tunamoishi?
Hali za kibinafsi ni zenye kutofautiana, na mambo kama vile kazi ya kimwili, mwenzi asiyeamini, na usafirishaji yanaweza kuwa na uvutano juu ya uamuzi wa mwisho wa mtu kuhusu jambo hilo. Hata hivyo, kuna faida za kiroho na nyinginezo mtu anaposhirikiana na kutaniko linalogawiwa eneo anamoishi. Wazee wanaweza kuwasiliana na wahubiri wote kwa uharaka zaidi katika visa vinavyoomba kutenda kwa uharaka. Visanduku vya Maulizo vilivyotangulia vimetoa mwangaza kuhusu kiasi fulani cha faida nyingine.—Novemba 1991.
Kwa ujumla, ni jambo lenye kufaa zaidi kuhudhuria mikutano ya karibu, hilo linaturuhusu kufika mapema vya kutosha ili kuzungumza na wengine, kushughulikia mambo ya lazima, na kushiriki wimbo na sala ya mwanzo. Wapya wanaopendezwa wanapoishi katika ujirani wetu, kwa ukawaida tuna nafasi iliyo bora ya kuwasiliana nao, kuongoza mafunzo ya Biblia nao, na kuwaongoza kwenye mikutano inayowafaa zaidi.
Tuko hakika kwamba vichwa vya familia watafikiria jambo hilo kwa njia ya sala, wakifikiria kwa makini mambo yote yanayohusika katika kuamua yale yaliyo bora kwa ajili ya hali njema ya kiroho na ya kimwili ya familia yao.—1 Tim. 5:8.