Jinsi Mpango wa Funzo la Kitabu la Kutaniko Unavyotusaidia
1 Kati ya mikutano mitano tunayofanya kila juma, kila mkutano ni tofauti na mwingine na kila mkutano una kusudi lake. Hata hivyo, mikutano yote mitano ni ya maana katika kutusaidia “tufikiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri.” (Ebr. 10:24, 25) Mkutano wa Funzo la Kitabu la Kutaniko una mambo fulani gani ya pekee na yenye kufaidi?
2 Unatusaidia ili Tufanye Maendeleo ya Kiroho: Kwa kawaida, hesabu ya watu wanaohuzuria funzo la kitabu ni ndogo sana kuliko hesabu ya wale wanaohuzuria mikutano mingine ya kutaniko. Hesabu ndogo hiyo inafanya iwe vyepesi kukomalisha urafiki unaoweza kutusaidia katika hali ya kiroho. (Met. 18:24) Je, umejikaza ili kujua washiriki wote wa kikundi chenu cha funzo la kitabu, labda kwa kuomba kila mmoja atumike nawe katika kazi ya kuhubiri? Pia mpango wa funzo la kitabu unamwezesha mwangalizi wa funzo la kitabu ajue hali za kila mshiriki wa kikundi na kumtolea kitia-moyo cha pekee.—Met. 27:23.
3 Je, umekwisha kualika wanafunzi wako wa Biblia wahuzurie funzo la kitabu pamoja nawe? Wale wenye kupendezwa wanaosita kuhuzuria mikutano yenye watu wengi wanaweza kuhuzuria bila woga katika kikundi kidogo cha funzo la Biblia, funzo linalofanyika zaidi sana katika nyumba ya ndugu fulani. Hali ya urafiki inafanya iwe vyepesi sana kwa watoto na wapya kutoa maelezo. Na kwa sababu kikundi ni kidogo sana, tuna nafasi zaidi za kutoa maelezo na hivyo kumsifu Yehova.—Zab. 111:1.
4 Kwa kawaida mafunzo ya kitabu yanafanywa mahali mbalimbali panapofaa wahubiri katika eneo lote. Kwa kuwa haiwezekani kila mtu kuhuzuria kwenye funzo la kitabu lililo karibu sana na mahali anapoishi, huenda kuhuzuria funzo la kitabu la mahali ambapo tumepangiwa kusituombe kufanya safari ndefu kama ile tunayofanya tunapokwenda kuhuzuria mikutano mingine ya kutaniko. Mahali pa funzo la kitabu panaweza pia kutumiwa kuwa mahali pa mkutano kwa ajili ya mahubiri.
5 Unatusaidia Kuhusu Kazi ya Kuhubiri: Mwangalizi wa funzo la kitabu anafurahia kusaidia kila muhubiri wa funzo ashiriki kwa ukawaida katika kazi ya kuhubiri, na pia awe na matokeo mazuri na furaha katika kazi hiyo. Kwa hiyo, anajikaza kuhubiri na kila mmoja katika kikundi, akitoa msaada wa pekee katika sehemu mbalimbali za kazi ya kuhubiri. Ukiona sehemu fulani ya kazi ya kuhubiri kuwa ngumu, kama vile kurudilia watu, julisha mwangalizi wa funzo lenu la kitabu. Labda anaweza kufanya mpango ili utumike pamoja na mhubiri wa kikundi chenu aliye na uzoefu. Uwezo wako wa kufundisha kwenye mafunzo ya Biblia utakuwa mzuri zaidi unapofuata kwa uangalifu njia nzuri za kufundisha za mwangalizi wa funzo la kitabu anapoongoza funzo la kitabu.—1 Kor. 4:17.
6 Funzo la Kitabu la Kutaniko ni mpango wenye kuleta baraka kabisa! Mpango huo wenye upendo kutoka kwa Yehova unatusaidia tuendelee kuwa na nguvu katika hali yetu ya kiroho katika nyakati hizi zilizo ngumu ambamo tunaishi.—Zab. 26:12.
[Maulizo ya Funzo]
1. Mikutano yetu mitano ya kila juma inatusaidia jinsi gani?
2. Ni faida gani zinazotokana na kukusanyika tukiwa kikundi kidogo sana kwenye funzo la kitabu?
3. Jinsi gani mpango wa funzo la kitabu unatia moyo kutoa maelezo na kusaidia wanafunzi wa Biblia wahuzurie?
4. Mpango wa funzo la kitabu unaweza kuwa wenye kufaa katika njia gani mbalimbali?
5. Namna gani tunaweza kupata msaada katika kazi ya kuhubiri kupitia mwangalizi wa funzo letu la kitabu?
6. Kwa nini tunapaswa kutafuta kufaidika kabisa kupitia mpango wa funzo la kitabu?