Kisanduku cha Maulizo
◼ Ni wakati gani lingekuwa jambo lenye kufaa kuunda kikundi cha ziada cha Funzo la Kitabu?
Kuunda kikundi kipya kungepaswa kufikiriwa wakati kufanya hivyo kunapohitajika ili kuendelea kuwa na hudhurio la watu 15 hivi au wachache zaidi kila mahali pa kufanyia funzo la kitabu, kutia ndani Jumba la Ufalme. Kwa nini jambo hilo linapendekezwa?
Wakati vikundi vya Funzo la Kitabu vinapofanywa viendelee kuwa vidogo, kiongozi ana uwezo bora wa kutoa uangalifu kwa kila mtu anayehudhuria. Kwa kuongezea, wote wana nafasi ya kutosha ili kutoa maelezo katika hali inayoelekea kuwachochea wafanye tangazo la peupe la imani yao. (Ebr. 10:23; 13:15) Kuwa na vikundi vidogo-vidogo mahali pengi katika eneo lote la kutaniko kunafanya kuhudhuria Funzo la Kitabu na mikutano kwa ajili ya utumishi wa shambani kuwe rahisi zaidi. Makutaniko ambayo yameongeza hesabu ya mahali pa kufanyia funzo la kitabu yametambua pia kwamba jumla ya hudhurio kwenye mkutano huo imeongezeka pia.
Kunaweza kuwa hali za pekee zinazofanya iwe vizuri zaidi kuunda kikundi kingine, hata ikiwa kitakuwa kidogo zaidi. Hilo linaweza kuwa kweli katika eneo lenye kujitenga au ambapo nafasi zilizopo ni zenye kujaa watu au kwamba zinakosa viti vyenye kufaa. Kinapohitajiwa, kikundi kinaweza kuundwa ambacho hufanya mkutano mchana kwa faida ya wazee-wazee, wafanyakazi wa usiku, au akina dada walio na waume wasio Mashahidi.
Kila kikundi cha funzo la kitabu kinapaswa kuwa na wahubiri mbalimbali wenye nguvu kiroho na wenye kutenda wanaotumwa huko, na pia kiongozi na msomaji mwenye sifa. Akina ndugu wanapaswa kujitahidi ili kutosheleza mahitaji hayo katika kutaniko.
Wazee wanaweza kuchochea maendeleo ya kutaniko kwa kuhakikisha kwamba vikundi vya funzo la kitabu ni vyenye ukubwa wa kadiri na vyenye kushughulikiwa vizuri kiroho, na kwamba vinafanyia mikutano mahali penye kufaa. Wakati wowote linapokuwa jambo lenye kufaa, vikundi vipya vinapaswa kuundwa ili wote wafaidike kikamili na manufaa ya mpango huo wa kiroho usiolinganika. Je, mnaweza kutoa nyumba yenu kuwa mahali pa kufanyia funzo la kitabu? Wengi waliofanya hivyo wamepata baraka za kiroho.