Tutolee Kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
1 Ni shangwe kama nini tuliyohisi wakati kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele kilipotolewa! Kitabu hicho kimetengenezwa ili kuwasaidia watu kupata haraka ujuzi kamili wa ukweli. Mnamo Juni, tutakitolea katika eneo letu. Tunaweza kusema nini ili kuamsha kupendezwa kwa wasikilizaji wetu?
2 Tazama utoaji unaoweza kupendeza watu ambao imani katika Mungu ilidhoofika:
◼ “Watu wengi waliolelewa katika imani katika Mungu wanatambua kwamba imani yao si yenye nguvu tena kama ilivyo kuwa. Kulingana nawe, sababu inaweza kuwa ni nini? [Tuache mtu ajibu.] Imani yetu katika Mungu inaimarika wakati tunapofikiri juu ya maajabu ya maumbile ya ulimwengu. [Tusome Zaburi 19:1.] Yeye ambaye sheria zake zinaongoza sayari angani anatutolea pia miongozo yenye thamani. [Tusome Zaburi 19:7-9.] Mistari hiyo inaonyesha kwamba ni jambo la lazima kujifunza yote tuwezayo juu ya Mungu na juu ya makusudio yake. [Tuvutie uangalifu juu ya picha kwenye kurasa 4 na 5, na tusome maandishi yaliyo pembeni ya picha.] Ikiwa unatamani kufaidika na ujuzi huo wa pekee, ningefurahi kukuachia kitabu hiki.”
3 Tukiwa wenye kufikiria tukio fulani lenye kuogofya la hivi karibuni, tungeweza kusema:
◼ “Umesikia bila shaka wakisema juu ya [tutaje tukio]. Je! umekwisha kujiuliza ikiwa Mungu anajali hakika udhalimu na mateso ambayo tunashuhudia au hata tunapatwa nayo? [Tuache mtu ajibu.] Biblia hutupa sisi uhakika wa kwamba Mungu anatupenda na kwamba atatusaidia katika hali ngumu.” Tusome sehemu ya Zaburi 72:12-17. Tufungue kitabu kwenye ukurasa 70, na tuonyeshe kwamba kitabu hicho, Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, kinajibu ulizo moja ambalo mamilioni ya watu wanajiuliza: Kwa nini Mungu anaruhusu mateso? “Utaona kuwa jambo lenye kuburudisha jibu ambalo Biblia hutoa kwa ulizo hilo. Ningependa kukuachia kitabu hiki ili ujivumbulie mwenyewe jibu hilo.”
4 Ikiwa tunakutana na baba au mama, tuzungumzie juu ya familia:
◼ “Wazazi walio wengi wanatambua kwamba ni vigumu kuwa na maisha ya familia yenye furaha. Kulingana na wewe, vizuizi vikubwa zaidi ni gani? [Tuache mtu ajibu.] Wengi wetu hufanya yote wawezayo, lakini tunatamani sote kujua kile kinachoweza kutusaidia kupata matokeo bora. Biblia inatoa mashauri bora. [Tusome sehemu za Wakolosayi 3:12, 18-21.] Biblia ina mambo mengi ya kusema juu ya habari hiyo, kama inavyokaziwa na sura ya 15 ya kitabu hiki, yenye kichwa cha habari ‘Kujenga Familia Inayomheshimu Mungu.’ Inakusanya mashauri ya kibiblia yanayoonyesha jinsi ya kutatua mikazo kati ya wenzi wa ndoa na kuwasaidia watoto wetu kupambana na matatizo yao. Niko hakika kwamba utathamini usomaji wa sura hii.”
5 Ikiwa tunapendelea kusema kwa kifupi, tungeweza kuanzisha mazungumzo hivi:
◼ “Je! haujawahi kujiuliza kamwe kwa nini tunazeeka na tunakufa? Sura ya 6 ya kitabu hiki inafasiria ni nini sababu ya kifo na jinsi Mungu atakavyokikomesha. Biblia inatuambia kwamba Mungu ameahidi uhai wa milele kwa wale wanaompenda. [Tusome Yohana 17:3.] Ikiwa unapenda kujua mengi zaidi juu ya habari hiyo, utathamini kitabu hiki chenye kuelimisha zaidi.”
6 Ikiwa tunajitayarisha vizuri, tutaweza kutumia kitabu hicho ili ‘kufungulia kabisa wengine Maandiko,’ kwa njia itakayowaletea shangwe kubwa.—Lk 24:32.