Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 7/96 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Ya Julai

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mikutano Ya Utumishi Ya Julai
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 7/96 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Ya Julai

TAARIFA: Huduma Yetu ya Ufalme itakuwa na programu ya mkutano wa utumishi kwa kila juma la miezi ambamo kunafanyika makusanyiko ya wilaya. Makutaniko yatafanya marekebisho ya lazima kufuatana na jambo la kwamba yatahudhuria kwenye kusanyiko la wilaya “Wajumbe wa Amani ya Kimungu” na kwamba yatafanya, kwenye mkutano wa utumishi utakaofanyika juma lifuatalo, kujikumbusha kwa dakika 30 ya nukta kuu za programu. Kujikumbusha huko siku baada ya siku kutatolewa mbele ya wakati kwa ndugu wawili au watatu wenye ujuzi ambao wataonyesha mawazo makuu. Kukiwa kwenye kutayarishwa vizuri, kutawasaidia washiriki wa kutaniko kukumbuka mawazo makuu, ili wafanye matumizi ya kibinafsi na wayatumikishe katika mahubiri. Maelezo ya wahudhuriaji na mambo yaliyoonwa yanayotajwa yatakuwa mafupi na kamili.

Juma Toka Julai 1

Wimbo 181

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo ya Huduma Yetu ya Ufalme. Eleza juu ya ripoti ya utumishi ya kutaniko.

Dak. 15: “Tuige Imani Yao.” Kwa maulizo na majibu. Chunguzeni namna mbalimbali ya mtu kuonyesha imani yake inayotajwa katika kisanduku ukurasa 13 wa Mnara wa Mlinzi wa Septemba 15, 1991. Hoji mhubiri mmoja au wawili na waulize kile kilichowasaidia kulinda utendaji wa kitheokrasi wa kawaida tangu miaka mingi.

Dak. 20: “Broshua: Vyombo vya Thamani kwa Ajili ya Huduma.” Mazungumzo juu ya utoaji mbalimbali wa habari unaopendekezwa. Toa kwa kifupi mawazo juu ya sehemu fulani za pekee za broshua. Maonyesho mawili au matatu yanayoonyesha jinsi ya kuyatolea.

Wimbo 143 na sala ya mwisho.

Juma Toka Julai 8

Wimbo 63

Dak. 10 : Matangazo ya kwenu. Hali ya akaunti

Dak. 15: Tuzoeze Watoto Katika Mahubiri. Hotuba inayotolewa na mzee. Tangu utoto wao, watoto wetu wangepaswa kuwa wenye kutenda pembeni nasi katika mahubiri. Watafaidika na mazoezi na ujuzi wanapopata msingi imara kwa imani yao na bidii kwa miaka inayokuja. Ni jambo la muhimu watambue ulazima wa kuona huduma kama kitu fulani cha muhimu na kuwa na mwenendo unaofaa. Watoto hawapaswi kufanya makelele; mahubiri sio wakati wa kucheza. Ni vizuri zaidi kwao wawe wenye kushindikizwa na watu wazima. Watu wazima wataweza kuwasaidia kutoa ujumbe kulingana na uwezo wao mbalimbali wa akili. (Ona Mnara wa Mlinzi wa Agosti 1, 1988, uku. 15 fu. 20.) Wazazi wana daraka la kuwaangalia watoto wao; hawapaswi kuwatuma kwenye mikutano kwa ajili ya mahubiri bila mtu mzima atakayeshughulika nao. Pongeza watoto wanapofanya jambo fulani nzuri.

Dak. 20: “Jinsi ya Kufanya Wanafunzi kwa Msaada wa Kitabu Ujuzi.” Maneno mafupi ya utangulizi yanayotegemea mafungu 1-2. Chunguzeni mafungu 3-11 kwa maulizo na majibu. Sema kwamba mafungu mengine ya nyongeza yatachunguzwa wakati wa mikutano ya utumishi ya miezi ifuatayo. Tia kila mmoja moyo kuilinda.

Wimbo 92 na sala ya mwisho.

Juma Toka Julai 15

Wimbo 157

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Kumbusha mipango iliyochukuliwa kwa ajili ya mahubiri mwisho wa juma na tia kutaniko moyo kuitegemeza. Fanyeni onyesho fupi juu ya utoaji wa magazeti ya mwisho mwisho.

Dak. 15: “Mazungumzo ya Kirafiki Yanayoweza Kugusa Moyo.” Kwa maulizo na majibu. Alika mhubiri mmoja au wawili kueleza mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo yanayoonyesha kwamba walipata matokeo mazuri kwa kujionyesha wenye urafiki.

Dak. 20: “Tukuze Kupendezwa Wakati wa Ziara za Kurudia.” Ndugu ambaye anapewa sehemu hii ya mkutano anazungumza pamoja na wahubiri watatu juu ya umuhimu wa kuwarudilia tena wale wote walioonyesha kupendezwa au kukubali vichapo. Wanachunguza utoaji mbalimbali unaopendekezwa na wanajizoeza kuutumikisha.

Wimbo 211 na sala ya mwisho.

Juma Toka Julai 22

Wimbo 6

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Kumbusha mipango iliyochukuliwa kwa ajili ya mahubiri mwishoni mwa juma na tia kutaniko moyo kuitegemeza.

Dak. 15: “Wazazi Wenye Furaha!” Mazungumzo yanayofanywa na mzee. Toa mawazo kwa msaada wa Mnara wa Mlinzi wa Agosti 15, 1987, kurasa 13 mpaka 15, mafungu 14 mpaka 23.

Dak. 20: “Tuwasaidie Watumikie Tena.” Hotuba na mazungumzo yanayofanywa na mzee. Dokeza kutumia makala “Nirudieni Mimi, Nami Nitawarudia Ninyi”, iliyotokea katika Mnara wa Mlinzi wa Agosti 1, 1992 katika kusudi la kuwatia moyo Wakristo wasiotenda. Taja nukta fulani fulani kuu.

Wimbo 71 na sala ya mwisho.

Juma Toka Julai 29

Wimbo 136

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Kumbusha mipango iliyochukuliwa kwa ajili ya mahubiri mwishoni mwa juma. Fanyeni maonyesho mafupi mawili juu ya utoaji wa magazeti nyumba kwa nyumba. Tia kutaniko lote moyo kutegemeza mahubiri ya nyumba kwa nyumba.

Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko. (Au hotuba inayotegemea makala “Exposons correctement la parole de la vérité”, iliyotolewa katika Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 1996, kurasa 29-31.)

Dak. 15: Mzee na mtumishi wa huduma wanazungumzia makala “Les familles pieuses du passé: un modèle pour aujourd’hui”, inayopatikana kwenye kurasa 20-3 za Mnara wa Mlinzi wa Septemba 15, 1995. Wanafanya matumizi ya mawazo kwa mahitaji ya familia za kutaniko.

Wimbo 179 na sala ya mwisho.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine