Wazazi Wenye Furaha!
1 Kwa ninyi ambao ni vijana na wanaoishi katika nyumba ya Kikristo, kuna namna moja ya pekee ya kuwafurahisha wazazi wenu. Ikiwa unatembea katika haki, ‘baba yako na mama yako watafurahi.’ (Mez. 23:22-25.) Wazazi wako wanatamani kwa kawaida kile kilicho chema kwako. Hakuna jambo lolote lingewafurahisha kuliko kukuona unazingatia ukweli moyoni mwako na kutoa wakfu maisha yako kwa Yehova.
2 Ni bahati kama nini kuwa na wazazi Wakristo! Tangu kuzaliwa kwako, wanakulisha, wanakuvika, wanakupangisha na wanakutunza. Jambo la lazima zaidi, wanajikaza kukufundisha Yehova na njia zake za haki za kutenda; mazoezi hayo yanaweza kukuhakikishia uhai wa milele. (Efe. 6:1-4) Jinsi gani kuonyesha shukrani yako?
3 Zingatia Ukweli Moyoni: Wazazi wako walijikaza kukusaidia kuchukua kwa uzito ukweli, kufanya maendeleo ya kiroho na kubaki karibu na tengenezo la Yehova. Unaweza kuonyesha shukrani yako kwa kupendezwa kwa moyo na funzo la familia. Onyesha nia ya kushiriki kwenye mikutano, chukua mipango kwa kujitayarisha ili kwamba familia ianze funzo pa wakati kamili. Kaa karibu na wazazi wako na uwe mwenye makini sana; fuata katika vichapo vinavyochunguzwa. Jikaze kushiriki. Iweni wanafunzi wenye kujiheshimu kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, mkubali vipindi na mvitayarishe kwa nia yenu yote. Kwenye Jumba la Ufalme, toeni utumishi wenu kwa kazi mbalimbali za kutimiza. Kwa kushughulika hivyo, mtakaza akili juu ya mambo yaliyo yenye faida kwa hali yenu ya kiroho.
4 Jiwekee Miradi Hatua kwa Hatua. Msiridhike na kushiriki kwa mfano tu katika mahubiri; komazeni tamaa ya kuwa wahubiri wenye kustahili. Fuateni programu ya usomaji wa kila juma wa Biblia, au vizuri zaidi tena mwiisome yote kulingana na programu ya kibinafsi. Iweni na mradi wa kutimiza matakwa kwa ajili ya kujitoa wakfu wa utu wenu kwa Mungu na ubatizo. Wazazi wenu wanaweza kuwasaidia kufikiria kwa makini miaka yenu ya shule ili mpate mazoezi yatakayowawezesha kumtumikia Yehova kikamilifu. Mjifanyie sifa itakayowatolea uwezekano wa kupendekezwa kwenye mapendeleo ya pekee, utumishi wa painia au wa Betheli. (Mdo. 16:1, 2) Jiwekeeni miradi ili mpata ‘kujihakikishia mambo yaliyo ya maana zaidi, ili kwamba mpate . . . kujazwa matunda ya uadilifu.’—Flp. 1:10, 11.
5 Ujana ni kipindi ndani yacho inafaa kujielimisha, kupata ujuzi na kujifunza kuishi katika jamii. Ni kipindi ambamo mtu anaweza kujifurahisha maishani kabla ya kutokea mikazo na madaraka ya ulimwengu wa watu wazima. Sulemani alisema: “Wewe, kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako.” (Muh. 11:9) Ikiwa mnaazimia kumtumikia Yehova katika ujana wenu, mtavuna baraka za milele.—1 Sik. 28:9.
6 Ikiwa ‘mnafuatia uadilifu’ badala ya “tamaa zenye kutukia ujanani”, mtaepusha wazazi wenu tabu na sikitiko nyingi. (2 Tim. 2:22, NW) Moyo wenu utakuwa na sababu za kufurahi. (Mez. 12:25) Zaidi ya yote, mtafurahisha Muumba wenu, Yehova Mungu.—Mez. 27:11.