Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/02 uku. 4
  • Furaha Zinazotokana na Utumishi wa Wakati Wote

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Furaha Zinazotokana na Utumishi wa Wakati Wote
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Utumishi Wa Painia: Je! Ni Wako?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • “Unaweza Kuwa Painia Kabisa!”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Na Atimize Mipango Yako Yote
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Kazi ya Upainia Inatia Nguvu Uhusiano Wetu Pamoja na Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 4/02 uku. 4

Furaha Zinazotokana na Utumishi wa Wakati Wote

1 Ukiwa kijana, bila shaka unafikiria wakati ujao wako. Andiko la Mezali 21:5 linatuambia kwamba “mafikili ya wenye bidii yanaelekea utajiri tu.” Itakuwa faida kwako kufikiria kwa uzito miradi yako maishani. Unapofanya mipango yako kwa ajili ya wakati ujao, fikiria kuanza utumishi wa wakati wote. Kwa nini?

2 Uliza watu wazima fulani waliopainia katika miaka yao ya ujana maoni yao ni nini, nao watakuambia bila ubadilifu jambo lilelile: “Hiyo ndiyo iliyokuwa miaka bora zaidi ya maisha yangu!’ Ndugu mmoja aliyepata furaha zinazotokana na utumishi wa wakati wote tangu ujana wake na kuendelea alisema katika maisha yake ya baadaye: “Ni jambo lenye kufanya mtu atosheke kwa kina kirefu kufikiri juu ya wakati wa ujana na kuweza kusema kwamba amefuata shauri hili lenye hekima: ‘Kumbuka vilevile Muumba wako katika siku za ujana wako.’ ” (Mhu. 12:1) Inaomba wewe na wazazi wako mpange mambo vizuri sasa ili kukutayarishia njia ya kupata aina hii ya furaha katika ujana wako ukiwa mvulana au msichana.

3 Wazazi, Chocheeni Utumishi wa Wakati Wote: Akiwa Baba mwenye kujali, Yehova anawaonyesha nyinyi njia kamili ya kufuata. (Isa. 30:​21) Katika kutoa mwongozo huo wenye upendo, anaonyesha mfano mzuri kwenu nyinyi wazazi Wakristo. Badala ya kuacha watoto wenu wachague wenyewe njia iliyo bora kwao, wazoezeni kwa hekima katika njia wanayopaswa kufuata kusudi wapate baraka ya Yehova. Kisha, wakati watakapokomaa, mazoezi yenu yatawasaidia “kutofautisha lililo sahihi na lililo kosa pia.” (Ebr. 5:​14) Watu wazima wanajua kutokana na mambo waliyojionea kwamba hawawezi kutumainia uamuzi wao wenyewe; wanapaswa kumtegemea Yehova ili kunyoosha njia zao. (Mez. 3:​5, 6) Uhitaji huo ni mkubwa hata zaidi kwa vijana, ambao wana ujuzi mdogo zaidi maishani.

4 Wazazi, kadiri watoto wenu wanavyokaribia umri wa miaka kati ya 13 na 19, au hata mapema zaidi, ongeeni nao kikweli juu ya miradi yao kuhusu kazi ya maisha. Washauri wa mambo ya shule, walimu, na wanadarasa wengine watajaribu kuwashawishi ili wafuatie mambo ya kimwili ya kilimwengu. Saidieni watoto wenu wachague masomo ambayo yatawapa mazoezi yenye kufaa, yatakayowawezesha kushughulikia mahitaji yao ya kimwili bila kuacha faida za Ufalme. (1 Tim. 6:​6-​11) Katika hali nyingi, elimu ya shule ya sekondari na mazoezi ya kiufundi na/au yale yanayotolewa huku mtu akifanya kazi huenda vikatosha ili ashughulikie ifaavyo mahitaji yake wakati anapoanza huduma ya painia wa kawaida.

5 Tieni vijana moyo wafuatie zawadi ya useja. Ikiwa baadaye wanaamua kuoa au kuolewa, watakuwa na uwezo mzuri zaidi wa kutimiza madaraka yao mazito ya ndoa. (Ona fungu la 19 katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni 2001, “Je, Unaweza Kujitoa?”) Kwa kusema ifaavyo juu ya upainia, kutumikia mahali ambapo uhitaji ni mkubwa zaidi, utumishi wa Betheli, kazi ya mishonari, ingizeni ndani ya vijana​—hata kwenye umri wa mapema zaidi​—tamaa ya kutumia maisha yao kwa namna yenye kupendeza Yehova, yenye kufaidi wengine, na yenye kuwaletea wenyewe furaha.

6 Vijana, Tieni Utumishi wa Wakati Wote pa Nafasi ya Kwanza: Vijana, hamhitaji kujiuliza jinsi kazi ya upainia ilivyo. Mnaweza kuijaribu kwa namna yenye kuomba tu nusu ya wakati kwa kuwa mapainia wasaidizi inapowezekana katika mwaka wote wa shule na katika vipindi vya mapumziko. Ndipo mtajua jinsi utumishi wa painia ulivyo wenye kutosheleza kwelikweli! Je, unaweza kuchukua mipango sasa ili kuwa painia msaidizi kati ya wakati huu na mwisho wa Agosti?

7 Ikiwa wewe ni ndugu kijana katika tengenezo la Mungu, fikiria pia kwa uzito kujitahidi kutimiza sifa za kuwa mtumishi wa huduma. (1 Tim. 3:​8-​10, 12) Kwa kuongezea, amua ikiwa unapenda kujaza ombi kwa ajili ya utumishi wa Betheli au kuhudhuria Shule ya Mazoezi ya Kihuduma, utakapotimiza umri unaoombwa. Ujuzi wako katika huduma ya painia utakufundisha mambo mengi ya thamani, kama vile jinsi ya kuishi kulingana na programu fulani, jinsi ya kuboresha namna yako binafsi ya kupanga mambo, jinsi ya kushirikiana kwa upatani na wengine, na jinsi ya kusitawisha hali ya kujua kuchukua madaraka yako. Hayo yote yatakutayarisha kwa ajili ya mapendeleo makubwa zaidi ya utumishi baadaye.

8 Jambo la maana sana ili kufanikiwa katika utumishi wa wakati wote ni kuwa na roho ya juhudi katika utumishi wa Mungu. Mtume Paulo alichochea mtazamo kama huo, naye alionyesha baraka ambazo zingetokana nao: “Lolote mnalofanya, lifanyeni kwa nafsi yote kama kwa Yehova . . . kwa maana mnajua kwamba ni kutoka kwa Yehova nyinyi mtapokea thawabu ipaswayo.” (Kol. 3:​23, 24) Yehova na awabariki kwa kuwapa furaha nyingi katika utumishi wa wakati wote!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine