Mikutano Ya Utumishi Ya Novemba
Juma Toka Novemba 4
Wimbo 47
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na matangazo yaliyochaguliwa ya Huduma Yetu ya Ufalme. Eleza juu ya ripoti ya utumishi ya kutaniko ya mwezi wa nyuma.
Dak. 15: Majibu kwa Maulizo Yenu. Mwangalizi wa utumishi au mzee mwingine mwenye uwezo anazungumzia habari pamoja na wasikilizaji.
Dak. 20: “Tutayarishe Utoaji Wetu Wenyewe wa Magazeti.” (Maf. 1-7) Uliza maulizo juu ya mafungu 1-4. Kisha maonyesho mawili au matatu mafupi yanayoonyesha jinsi tunavyoweza kutolea magazeti ya mwisho-mwisho kwa kutumia madokezo ya mafungu 5-7. Eleza pia juu ya Mnara wa Mlinzi wa Machi 1, 1987, ukurasa 17, maf. 8-9.
Wimbo 222 na sala ya mwisho.
Juma Toka Novemba 11
Wimbo 39
Dak. 10: Matangazo. Hali ya akaunti.
Dak. 15: “Tutangaze Habari Njema za Kitu Bora Zaidi.” Kwa maulizo na majibu. Vutia uangalifu juu ya makala za Mnara wa Mlinzi zilizovuma sana.—Ona Mnara wa Mlinzi wa Machi 1, 1987, ukurasa 13.
Dak. 20: “Tutayarishe Utoaji Wetu Wenyewe wa Magazeti.” (Maf. 8-11) Kwa maulizo na majibu. Eleza madokezo manne ya Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 1994, kurasa 24-5, mafungu 18-21. Kwa msaada wa magazeti mliyo nayo, onyesha jinsi ya kutayarisha utoaji. (1) Chagua makala moja inayoweza kupendeza watu wa eneo lenu, (2) tafuta wazo moja lenye kupendeza la kukazia, (3) tayarisha ulizo moja ambalo litawezesha kuelekeza uangalifu juu ya wazo hilo, (4) chagua andiko moja ambalo ungeweza kusoma ikiwa wanakupa uwezekano na (5) tayarisha utangulizi na pia yale utakayosema kuhusu gazeti ili kumtia msikilizaji wako moyo alikubali. Omba wahubiri wawili au watatu wenye uwezo wafanye kila mmoja utoaji. Onyesho la utoaji mwepesi wa gazeti likitolewa na kijana.
Wimbo 82 na sala ya mwisho.
Juma Toka Novemba 18
Cantique 169
Dak. 15: Matangazo. Fasiria jinsi tunavyoweza kufanyiza njia ya ugawaji: (1) kuandika kila gazeti tuliloacha na makala iliyoonyeshwa, (2) kupanga mambo ili kurudi pamoja na namba zinazofuata na (3) kutayarisha wakati kamili katika programu ya kila juma ya mahubiri ili kufanya ziara za kurudia. Pendekeza kwa watu wanaoonyesha kupendezwa kujiandikisha kwa muda wa miezi sita, na fikiria kuhesabu ziara ya kurudia kila mara unapopeleka magazeti mapya kwa mtu fulani.
Dak. 15: “Tutembelee Eneo Letu Lote.” Zungumzia makala na mipango inayochukuliwa mahali penu ili kuhubiri kwa wachuuzi. Alika wasikilizaji waeleze mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo ambayo yaliwafikia kwa kuhubiri katika maduka yanayopatikana katika eneo lao.
Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko au hotuba inayotolewa na mzee yenye msingi juu ya makala iliyotolewa katika Mnara wa Mlinzi wa Mei 1, 1996, kurasa 21-4.
Wimbo 12 na sala ya mwisho.
Juma Toka Novemba 25
Wimbo 27
Dak. 10: Matangazo. Miezi ya Desemba na Januari inakaribia, pamoja na siku zayo za sikukuu na likizo, zikiacha zaidi wakati huru kwa wale wanaotumika au kwenda shuleni. Tia kila mmoja moyo kufikiria uwezekano wa kuwa painia msaidizi. Eleza kwa wahubiri wote kutoa ripoti yao ya utumishi mwisho huu wa juma.
Dak. 20: “Jinsi ya Kununua Wakati Unaofaa.” Kwa maulizo na majibu. Toa mawazo ya ziada kwa msaada wa Mnara wa Mlinzi wa Desemba 1, 1989, kurasa 16-17, mafungu 7-11.
Dak. 15: Kichapo Tunachotolea Mnamo Desemba. Tutatolea kitabu Ujuzi na tutafanya juhudi ya pekee ili kurudi kuwaona watu tulioachia chenyewe, tukiwa na mradi wa kuanzisha mafunzo ya Biblia. Wahubiri wawili au watatu wenye uwezo wanazungumza juu ya thamani ya kitabu na namna ambayo tunaweza kukitumia. Habari zilizomo zinagusa maisha ya watu wa tabaka zote za jamii. Kinazungumzia habari na kanuni za Biblia za msingi ambazo wapya wanapaswa kuelewa kabla ya wao kubatizwa. Ikiwa funzo linaendelea kwa mwendo wa kawaida, mwanafunzi atafanya maendeleo haraka. Mazungumzo na onyesho juu ya namna ya kuanzisha funzo kwa msaada wa ufundi wa moja kwa moja: chunguzeni picha na maelezo ya kurasa 4-5; fasiria ufundi wetu wa funzo; zungumzeni kwa kifupi mafungu tano ya kwanza ya sura 1; pataneni siku ya kurudi tena ili kuendeleza mazungumzo na kujibu kwenye ulizo lifuatalo: “Je! Uhai Udumuo Milele ni Ndoto?” Kazia kwamba pendeleo la kuongoza funzo la Biblia huleta shangwe.
Wimbo 162 na sala ya mwisho.