Tutangaze Habari Njema Za Kitu Bora Zaidi
1 Sasa ni miaka 117 tangu Mnara wa Mlinzi unatetea ukweli wa Biblia. Kwa sasa nakala 18, 950, 000 za kila namba zinachapwa katika lugha 125. Amkeni! pia ni mteteaji wa miaka mingi wa Neno la Mungu na nakala 15, 739, 000 zinatolewa katika lugha 80.—Ona Wakolosai 1:23.
2 Magazeti Yanatosheleza Uhitaji wa Kiroho: Mamilioni ya watu wanyofu wanafaidika na Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ambayo yanawasaidia kutosheleza mahitaji yao ya kiroho kwa msaada wa makala zinazojenga imani. Kwa mfano, katika Mnara wa Mlinzi wa Februari 1, 1996, tulijifunza makala moja iliyozungumzia ulazima wa kutumainia katika Yehova na katika Neno lake. Mnara wa Mlinzi wa Machi 1, 1996, ulitutia moyo kubaki wenye kushughulika katika utumishi kwa ajili ya Yehova na kuendelea kungoja. Uchunguzi mzito wa unabii wa Sefania ulikuwa wenye kutia nguvu kama nini! Kisha tulipata mazungumzo yenye kusisimua juu ya uaminifu wa Kikristo katika Mnara wa Mlinzi wa Machi 15, 1996. Namba ya Mei 15, 1996, ilitilia mkazo ulazima wa kusoma na kujifunza kikawaida Neno la Mungu. Makala hizo zilituwezesha kuchimbua sana katika kuelewa kwetu Neno la Mungu na kuongeza shukrani yetu kwa ajili ya Ufalme wake.
3 Kwa upande mwingine, magazeti yana makala zifaazo na zenye kutenda kazi juu ya mwenendo unaomfurahisha Mungu, adili ya Kikristo na habari nyingine za muhimu. Yanazungumzia maswala ya lazima yanayogusa uhai wetu. Tunaweza pia kuwa na maisha ya hali ya juu tangu sasa kwa kungoja kwamba ahadi za kimungu kuhusu kitu kilicho bora kwa ajili ya wakati ujao zitimie.—Is. 48:17; 1 Tim. 6:19.
4 Kwa kusoma tena kwa kifupi yale yanayosemwa kwenye ukurasa wa 4 wa Amkeni! tutaona kwamba tunazo sababu nzuri za kupendekeza gazeti hilo. Iwe watu wanatoka wapi, wawe ni vijana au wazee-wazee, huo ni usomaji bora kwao. Inasemwa hivi ndani yalo: “Amkeni! ni gazeti la kupatia familia nzima nuru. Huonyesha jinsi ya kukabiliana na matatizo ya wakati wetu. Huripoti habari, husimulia juu ya watu katika nchi nyingi, huchunguza dini na sayansi. Lakini si hayo tu. Huchunguza sana matukio ya sasa na hutoa maana ya kweli ya matukio hayo, hata hivyo linabaki sikuzote bila kuingilia siasa wala kutukuza jamii moja ya watu juu ya nyingine. La maana kuliko yote, gazeti hili hujenga uhakika katika ahadi ya Muumba ya kuleta ulimwengu mpya wenye amani na usalama ambao uko karibu kuchukua mahali pa mfumu wa mambo uliopo mwovu na usiotii sheria.”
5 Tutolee Magazeti kwa Wengine: Tuwe wakarimu kwa habari ya kutolea Mnara wa Mlinzi na Amkeni! (Ona 1 Timotheo 6:18.) Tuwe na namba fulani fulani mikononi ili kuzitolea iwezekanavyo kwa wale ambao tungeweza kukutana nao. (Mh. 11:6) Sisi sote, kutia na vijana na wahubiri wapya, tunaweza kushiriki kikamilifu katika ugawaji wa magazeti mwezi huu kwa kutumia utoaji mbalimbali mfupi wenye msingi juu ya makala za habari za ulimwengu zilizomo katika namba za mwisho-mwisho. Tufahamiane vizuri na mambo yaliyomo na tuyatolee kwa unyofu na uhakika.
6 Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yana habari ambazo kila mmoja anahitaji kujua. Tuyaache kwa watu; ni mojawapo ya njia bora ya kuwasaidia kujifunza habari njema ya kwamba kitu fulani kilicho bora ni karibu kutukia.