Tutembelee Eneo Letu Lote
1 Katika mitaa inayokaliwa na watu, wakati mwingine kuna maduka madogo-madogo ya vyakula na viungo, mkahawa au mchuuzi anayeuzisha vitu vya rejareja (vidogo-vidogo). Ikiwa nyumba hizo ni sehemu ya eneo, tungepaswa kuwafikia wale wanaotumikia ndani kwa namna moja na wakaaji wa mtaa.
2 Tunaweza kutumia utoaji mwepesi na mfupi, kwa kusema kwa mfano: “Ningependa kukuonyesha kitu fulani.” Ikiwa inaonekana kwamba mwenye nyumba ana kazi kwa wakati ule, tunaweza tu kumtolea trakti na kusema: “Nitapita wakati utakapokuwa hauna na kazi nyingi. Ningependa kujua yale unayofikiri juu ya trakti hiyo.”
3 Utendaji huo haungepaswa kutuogopesha. Mhubiri mmoja alitambua: “Nilikuwa nikitazamia kuitikia kusikofaa. Hata hivyo, kwa mshangao wangu mkubwa, ni kinyume kilichojitokeza niliposema juu ya Ufalme. Watu walikuwa kweli wenye adabu, wenye urafiki; karibu wote, walichukua magazeti.”
4 Mwanamke mmoja anayetumika katika shirika linaloshughulika na mambo ya ujenzi alialika Mashahidi katika afisi yake. Alikubali magazeti na alionyesha nia ya kujifunza Biblia. Walimwonyesha kitabu Ujuzi, na funzo lilianzishwa haraka katika afisi yake!
5 Tuna daraka la kutembelea eneo letu lote, jambo ambalo linamaanisha kuwaona wachuuzi wa mtaa. (Mdo. 10:42) Tupange kuwatembelea kama watu wengine. Hivyo, si kwamba tu tutatembelea vizuri zaidi eneo letu, lakini inawezekana kwamba tutapata pia matokeo yenye kufurahisha ambayo yatadhawabisha juhudi yetu.