Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/97 uku. 2
  • Majibu Kwa Maulizo Yenu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Majibu Kwa Maulizo Yenu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Je, Unatimiza Fungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Wahubiri wa Habari Njema
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Saidia Mwangalizi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko Lako
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Je, wewe ni mtangazaji aliye kawaida wa ufalme?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 2/97 uku. 2

Majibu Kwa Maulizo Yenu

◼ Kwa nini tunapaswa kutoa ripoti ya utumishi bila kuchelewa kila mwezi?

Sisi sote ni wenye shangwe tunaposikia matokeo mazuri yanayopatikana katika mahubiri ya ujumbe wa Ufalme. (Ona Mezali 25:25.) Matendo 2:41 inaripoti kwamba siku ya Pentekoste, kutokana na hotuba moto moto ya Petro, “nafsi karibu elfu tatu zikaongezwa.” Baadaye, hesabu hiyo ikaongezeka kufikia “karibu elfu tano.” (Mdo. 4:​4, TUM) Wakristo wa karne ya kwanza walishangilia kama nini waliposikia hilo! Leo, tunaitikia vivyo hivyo tunapopokea ripoti zenye kutia moyo. Tunahisi shangwe kubwa kwa kusikia matokeo mazuri ambayo ndugu zetu ulimwenguni wanapata katika mahubiri ya habari njema.

Inaomba wakati mwingi na bidii ili kuhesabu ripoti zote hizo, pia ushirikiano wa kila mhubiri wa Ufalme ni wa muhimu. Je! sisi tunatambua umuhimu wa kutoa bila kukawia ripoti yetu kila mwezi?

Ongezeko ambalo tunaripotiwa linatutolea shangwe kubwa. Zaidi ya hilo, ripoti zinaiwezesha Sosaiti kujua ni wapi tunafikia katika maendeleo ya kazi ulimwenguni. Maamuzi yanapaswa kuchukuliwa kuhusu maeneo ambako kunahitajiwa msaada, uchaguzi wa vitabu vya kutolea na jumla yavyo. Katika kila kutaniko, wazee wanachunguza ripoti za utumishi ili kuona ni katika sehemu gani tunaweza kufanya vizuri zaidi. Ripoti nzuri zinatutia moyo na zinamsukuma kila mmoja wetu kuchunguza huduma yake ili kuona ni wapi inawezekana kufanyia maendeleo.

Kila mhubiri anapaswa kutambua daraka lake mwenyewe la kutoa haraka ripoti yake ya utumishi kila mwezi. Viongozi wa funzo la kitabu wana nafasi nzuri ya kuwakumbusha wahubiri daraka hilo, kwa kuwa wanajikaza pia kutoa msaada wa kibinafsi kwa wale walio labda na matatizo ili kuhubiri kila mwezi, kwa ukawaida. Wanaweza kukumbusha hilo wakati wa funzo la mwisho la mwezi, au kwa wakati mwingine wenye kufaa. Ikiwa haiwezekani kutoa ripoti za utumishi kwenye Jumba la Ufalme, kiongozi wa funzo la kitabu ataweza kuzikusanya na kuangalia ili kwamba zitolewe kwa mwandishi pa wakati ili mwandishi azihesabu katika ripoti ya mwezi ya kutaniko inayotumwa kwenye Sosaiti.

Unyofu wetu kuhusu kuripoti kiaminifu pa wakati utendaji wetu bila kuchelewa unawarahisishia kazi wale wanaosimamia hali yetu njema ya kiroho.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine