Makusanyiko Ya Kimataifa Katika Amerika Ya Kaskazini Mnamo 1998
Kama hilo lilivyotangazwa Siku ya Posho Oktoba 6, 1996 wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania, Baraza linaloongoza linapanga kutayarisha makusanyiko ya kimataifa mnamo 1998. Zaidi ya makusanyiko ya wilaya ya kawaida kutatayarishwa makusanyiko ya kimataifa katika Amerika ya Kaskazini na pia katika Afrika, Asia, Ulaya, Amerika ya Kilatini, Katika Antilles na katika Pasifiki ya Kusini.
Mengi ya makusanyiko hayo ya pekee yatafanyika katika Amerika ya Kaskazini, na wajumbe kutoka ulimwenguni pote wataalikwa huko. Zaidi ya hayo, tunatazamia kupokea wamishonari kwenye makusanyiko hayo ya kimataifa. Wamishonari na akina ndugu wengine wanaojitoa kabisa katika utumishi wa pekee ugenini na wanaotimiza matakwa yanayoombwa, wataalikwa kuhudhuria mojawapo ya makusanyiko hayo katika nchi yao ya asili, au katika nchi jirani.
Mtapokea katika wakati ujao ulio karibu maelezo zaidi kuhusu tarehe, mahali, matakwa yanayopaswa kutimizwa ili kuwa mjumbe, mipango inayochukuliwa kwa ajili ya wajumbe watakaotoka ugenini na mambo mengine tena. Hesabu yenye kikomo ya wajumbe wa Shirikisho ya Amerika watakuwa na uwezekano wa kuhudhuria makusanyiko ya kimataifa katika nchi nyingine. Wahubiri wanaotazamia kujaza ombi ili kuwa kati ya wajumbe hao watataka labda kuanza kuweka kando akiba ya fedha kwa matazamio ya matukio hayo ya pekee.