Mikutano Ya Utumishi Ya Aprili
Juma Toka Aprili 7
Wimbo 53
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. “Majibu kwa Maulizo Yenu” na Matangazo yaliyochaguliwa ya Huduma Yetu ya Ufalme. Tia kila mmoja moyo kufuata kupendezwa kulikoonyeshwa na wale waliohudhuria kwenye Ukumbusho Machi 23.
Dak. 15: “Tujenge Watu wa Nyumbani Mwetu.” Kwa maulizo na majibu. Taja mambo yaliyoonwa kutokana na Kitabu-Mwaka 1995, uku. 228.
Dak. 20: “Tusaidie Familia Kujijengea Wakati Ujao Udumuo.” (Maf. 1-5) Eleza kwa kifupi fungu la 1 na sema baadaye jinsi tunaweza kuchochea kupendezwa kwa ajili ya kitabu Furaha ya Familia kwa msaada wa vichwa vya sura, picha zenye rangi na visanduku vya kujikumbusha. Omba wahubiri wenye uwezo wafanye onyesho la mafungu 2-5. Tia kila mmoja moyo kufanya bidii ya pekee ili kuacha kitabu Furaha ya Familia kwa familia ambazo tayari zilionyesha kupendezwa. Fikiria kusema juu ya michango ya kujipendea.
Wimbo 71 na sala ya mwisho.
Juma Toka Aprili 14
Wimbo 56
Dak. 10: Matangazo. Hali ya akaunti na “Habari za Kitheokrasi.”
Dak. 20: “Tujionyeshe Wenye Shukrani.” Kwa maulizo na majibu. Tia moyo wote ambao wanaweza kuwa mapainia wasaidizi mnamo Mei.
Dak. 15: “Tusaidie Familia Kujijengea Wakati Ujao Udumuo.” (Maf. 6-8) Toa madokezo fulani juu ya namna ya kutolea kitabu Furaha ya Familia wakati tunapotoa ushuhuda wa vivi hivi kazini, shuleni, sokoni, katika usafirishaji wa watu wote, na pia wakati mtu anapotembelea washiriki wa familia yake. Omba kwa mhubiri mmoja mwenye uwezo kufanya onyesho moja la vielelezo vya mafungu 6 na 7. Mazungumzo wakati wa ziara ya kurudia yangepaswa kumsaidia mtu kuelewa kwamba funzo la Biblia linaweza kutia nguvu vifungu vya familia. Mafunzo yanapaswa kuongozwa kwa msaada wa broshua Mungu Anataka Nini Kwetu? pamoja na mradi wa kupitia kitabu Ujuzi, labda iwe kwamba funzo limeanzishwa moja kwa moja katika kitabu Ujuzi.
Wimbo 72 na sala ya mwisho.
Juma Toka Aprili 21
Wimbo 67
Dak. 5: Matangazo. Sema kwamba bado ni wakati wa kutoa ombi ili kuwa painia msaidizi mnamo Mei. Sema juu ya mikutano ya ziada kwa ajili ya mahubiri iliyopangwa kwa mwezi huu katika kutaniko.
Dak. 25: “Tujipe Ujasiri ili Kufanya Ziara za Kurudia.” (Maf. 1-16) Kwa maulizo na majibu. Onyesho fupi juu ya fungu la 16.
Dak. 15: Tusaidie Mhubiri Mpya Anayeanza. Chunguzeni fungu la 19 la nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1996. Onyesho: mhubiri mwenye uwezo anaonyesha mwanafunzi wa Biblia ambaye amekubaliwa na wazee kuwa mhubiri asiyebatizwa jinsi ya kujitayarisha. Wanachunguza pamoja kitabu Huduma Yetu, uku. 111, fungu la 2. Mhubiri mwenye ujuzi anasema juu ya yale yanayoweza kufika wakati mwingine tunapohubiri nyumba kwa nyumba, akionyesha kwamba haifai kuvunjika moyo ikiwa watu wengi hawaitikii vizuri. Anaeleza jambo moja lililoonwa lenye kutia moyo linaloonyesha shangwe ambayo mtu huhisi tunapokutana na mtu mnyofu aliye tayari kusikiliza. Wanatayarisha pamoja toleo fupi na rahisi la magazeti na wanajizoeza. Vitia moyo vyenye shauku vinatolewa na wahubiri wawili wanachukua mipango kamili ili kushiriki pamoja katika mahubiri mnamo juma.
Wimbo 89 na sala ya mwisho.
Juma Toka Aprili 28
Wimbo 70
Dak. 15: Matangazo na Tufanye Matumizi Mazuri ya Kitabu-Mwaka 1997 cha Mashahidi wa Yehova. Baba anachunguza nukta kubwa za kurasa 3-9 pamoja na washiriki wa familia yake. Sema kwa nini tunafurahi kuona maendeleo ya kitheokrasi ulimwenguni pote. Baba anafasiria kwamba mnamo mwaka huu ambao umeanza watachukua dakika fulani kila siku wakati wa kula chakula ili kusoma hatua kwa hatua Kitabu-Mwaka, namna ileile kama wanavyochunguza andiko la siku.
Dak. 15: “Tujipe Ujasiri ili Kufanya Ziara za Kurudia.” (Maf. 17-21). Kwa maulizo na majibu. Chunguzeni kisanduku kwenye ukurasa wa 3. Tia kila mmoja moyo kuhesabu ziara zote za kurudia ambazo atafanya muda wa mwezi wakati atakaporipoti utendaji wake wa mahubiri.
Dak. 15: Vichapo Vitakavyotolewa Mnamo Mei. Tutatolea Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Sema kwa kifupi juu ya madokezo yanayotolewa na mafungu 3, 4 na 8, uku. 8, wa Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 1996 juu ya namna ya kutayarisha utoaji mbalimbali wa magazeti. Maonyesho: wahubiri wawili wanafanya utoaji moja au mbili fupi. Wahubiri wangepaswa kuandika wale wanaokubali magazeti na kuwaongeza kwenye njia yao ya magazeti.
Wimbo 92 na sala ya mwisho.