Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/97 uku. 3-4
  • Tujipe Ujasiri Ili Kufanya Ziara Za Kurudia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tujipe Ujasiri Ili Kufanya Ziara Za Kurudia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ziara za Kurudia Huongoza Kwenye Mafunzo ya Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Mafunzo Ya Biblia Zaidi Yanatakwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Tumtegemee Yehova ili ‘Kufululiza Kukuza’
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 4/97 uku. 3-4

Tujipe Ujasiri Ili Kufanya Ziara Za Kurudia

1 Je! ungependa kufanya ziara za kurudia? Ndivyo ilivyo kwa wahubiri wengi. Labda ulikuwa na woga mwanzoni, hasa wakati ulipokuwa ukirudi kuwaona watu ambao walionyesha tu kupendezwa kidogo wakati wa kukutana kwa mara ya kwanza. Lakini kwa kadiri ‘ulivyojipa ujasiri kwa njia ya Mungu wetu ili kusema habari njema’ kwa kufanya ziara za kurudia, uliweza labda kushtushwa kuona kwa kiasi gani utendaji huo ungeweza kuwa rahisi na wenye kutajirisha. (1 Thes. 2:2) Jinsi gani kuufikia?

2 Kwa wazi, ziara ya kurudia ni tofauti na ziara ya kwanza. Wakati wa ziara ya kurudia tunazungumza na rafiki, si mtu mgeni, na kwa ujumla ni rahisi kuzungumza na mtu ambaye tumekwisha kuona. Tunajipatia faida nyingi kwa kujitoa kabisa katika utendaji huo: ziara za kurudia zinaweza kuongoza kwenye mafunzo ya Biblia yanayofanya maendeleo.

3 Tunapohubiri nyumba kwa nyumba, tunatambua kwa ukawaida watu ambao hawakupendezwa na ujumbe wakati wa kupita kwetu kwa mara ya kwanza. Kwa nini basi tunaendelea kwenda kuwaona? Tunajua kwamba hali ya watu inabadilika na kwamba mtu aliyekuwa akionekana mwenye ubaridi, hata mpinzani kuelekea ujumbe, anaonyesha kupendeza wakati ufuatao. Tunapotambua hilo, tujitayarishe vizuri na tusali ili kupokea uongozi wa Yehova ili kwamba watu watege sikio kwa uangalifu kwa yale tutakayosema.

4 Ikiwa, katika utendaji wa nyumba kwa nyumba, tupo tayari kuhubiri watu ambao hawakuonyesha kupendezwa kokote, je! hatungepaswa kutaka zaidi kuwarudilia wale wote waliosikiliza ujumbe wa Ufalme?​—Mdo. 10:34, 35.

5 Wengi kati yetu leo wako katika ukweli kwa sababu mhubiri fulani aliwatembelea kwa uvumilivu mara nyingi. Ikiwa ndivyo, tujiulize: ‘Ni maoni gani niliacha mwanzoni kwa mhubiri huyo? Je! nilikubali ujumbe wa Ufalme tangu tu nilipousikia? Je! nilikuwa mwenye ubaridi?’ Tungepaswa kuwa wenye furaha kama vile ule mhubiri aliyerudi kuja kutuona kwa kuwa alituona kuwa wenye kustahili kurudiliwa upya, kwamba ‘alijipa ujasiri kwa njia ya Mungu,’ akaja kwetu na akaanza kutufundisha ukweli. Tuseme nini basi juu ya wale wanaoanza kuonyesha kupendezwa fulani mwanzoni lakini ambao baadaye wanaonekana kuwa wanataka kutuepuka? Ni jambo la muhimu kwamba tuwe na hali ya akili yenye kutazamia mema, kama inavyoonyeshwa na jambo lililoonwa lifuatalo.

6 Asubuhi mapema, wahubiri wakike wawili walikuwa wakitoa ushuhuda barabarani wakati walipokutana na mwanamuke mmoja akiwa na kiti cha mtoto cha magurudumu. Alikubali gazeti na aliwaalika dada hao kuja nyumbani kwake Siku ya Yenga ifuatayo. Walifika kwa saa waliyopatana, lakini mama wa nyumba huyo aliwaambia kwamba hakuwa na wakati wa kuzungumza. Hata hivyo, aliahidi kuwa huru juma lifuatalo. Dada hawakuwa hakika kwamba ataheshimu programu hiyo ya kukutana, lakini waliporudi tena mwanamuke huyo alikuwa akiwangoja. Funzo lilianzishwa, na maendeleo ya mwanamuke huyo yalikuwa yenye kushangaza. Hakukawia kuhudhuria kwa ukawaida kwenye mikutano na baadaye kushiriki katika mahubiri. Kwa sasa ni mwenye kubatizwa.

7  Tuweke Msingi Tangu Mazungumzo ya Kwanza: Mara nyingi, tunaweka msingi wa ziara ya kurudia yenye mafanikio wakati wa mazungumzo ya kwanza. Tumsikilize kwa makini msikilizaji wetu. Anasema nini? Je! anafurahia mambo ya dini? Je! anapendezwa na maswali ya kijamii? ya kisayansi? ya kihistoria? ya kimazingira? Mwishoni mwa mazungumzo, tunaweza kutokeza ulizo linalomfanya mtu kufikiri na kumuahidi msikilizaji kuzungumzia jibu linalotolewa na Biblia tutakaporudi tena.

8 Kwa mfano, ikiwa msikilizaji wetu anagusika moyo na ahadi ya Biblia ya Paradiso duniani, mazungumzo mengine juu ya habari hiyo yanaweza kuwa yenye kufaa. Kabla ya kuondoka, tunaweza kuuliza: “Jinsi gani unaweza kuwa hakika kwamba Mungu atatimiza ahadi yake?” Na kuongeza: “Ningeweza labda kurudi tena familia yote itakapokuwapo na kukuonyesha jibu ambalo Biblia inatoa.”

9 Ikiwa mtu hakuonyesha kupendezwa kwa ajili ya habari fulani, tungeweza kutokeza mojawapo ya maswali ambayo hupatikana katika vielelezo vya ukurasa wa mwisho wa Huduma Yetu ya Ufalme na kuvitumia kama msingi kwa ajili ya mazungumzo yetu ya baadaye.

10 Tuandike Mambo kwa Usahihi: Maandishi yetu ya nyumba kwa nyumba yangepaswa kuwa sahihi na kamili. Tuandikie jina na anwani ya msikilizaji wetu tangu tu tunapoachana naye. Tusiandike kwa kuwazia tu namba ya nyumba na jina la barabara: tuchunguze kwamba maelezo ni sahihi. Tuandike mambo fulani kuhusu mtu, habari ambayo tulizungumzia, maandiko tuliyosoma, vichapo ambavyo labda tuliacha na maulizo ambayo tutajibu wakati wa ziara yetu ijayo. Tuonyeshe pia siku na saa ya mazungumzo yetu na wakati ambao tuliagana kuonana tena. Kwa sasa fomu yetu ni kamili, tusiipoteze! Tuitie mahali ambapo tupo hakika kuipata. Tufikirie mtu na namna ambayo tungeweza kuendeleza mazungumzo wakati ujao.

11 Tusisahau ni Nini Mradi Wetu: Kwanza kabisa, kwa kuwa wenye shauku na wenye urafiki, tufanye yote tuwezayo ili kumfanya msikilizaji wetu awe mwenye starehe. Tuonyeshe kwamba tunapendezwa naye kama vile mtu binafsi, bila kuwa wenye kuzoeana sana. Tena, tumkumbushe maulizo ambayo tulitokeza wakati wa nyuma. Tusikilize kwa makini maoni yake na tumshukuru kikweli kwa maelezo yake. Kisha tumuonyeshe ni katika nini wazo la Biblia ni lenye manufaa. Ikiwezekana, tumuongoze kwenye wazo lenye kufanana na hilo katika kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Tukumbuke vizuri kwamba mradi wetu wa kwanza wakati wa ziara ya kurudia ni kuanzisha funzo la Biblia.

12 Sauti ya moja kwa moja ya kitabu Ujuzi ilisaidia wengi kati yetu ‘kujipa ujasiri’ katika mafunzo ya Biblia ili kuwatia moyo wanafunzi kuhudhuria kwenye mikutano na kujiunga na tengenezo la Yehova. Wakati wa nyuma, tulikuwa na maelekeo ya kungoja kwamba watu wajifunze muda wa wakati fulani kabla ya kuwaalika kujiunga nasi. Kwa sasa, wanafunzi wengi wanahudhuria kwenye mikutano tangu tu wanapoanza kujifunza na wanafanya hivyo maendeleo ya haraka zaidi.

13 Wenzi wawili wa ndoa walitoa ushuhuda wa vivi hivi kwa mfanyakazi mwenzao. Kwa kuwa mfanyakazi huyo alionyesha kupendezwa na ukweli, ndugu na mke wake walimtolea funzo la Biblia kwa msaada wa kitabu Ujuzi. Wakati huohuo, walimtia moyo kuhudhuria kwenye mikutano, ambako angepata jibu kwa mengi ya maulizo yake. Si kwamba tu mtu huyo alikubali funzo, lakini alianza kujifunza mara mbili kwa juma na kuhudhuria kwa ukawaida mikutano kwenye Jumba la Ufalme.

14 Tutumie Broshua Mungu Anataka Nini Kwetu?: Kwenye kusanyiko la wilaya “Wajumbe wa Amani ya Kimungu,” tulipokea broshua Mungu Anataka Nini Kwetu? Broshua hiyo inawezesha kuanzisha mafunzo ya Biblia pamoja na watu wanaomuogopa Mungu haidhuru kiwango cha elimu yao. Ina masomo kamili yanayotia ndani mafundisho ya msingi ya Biblia. Kichapo hicho ni chombo chenye matokeo sana ili kutangaza ujuzi wa Mungu. Inafasiria ukweli kwa namna iliyo wazi zaidi na rahisi zaidi hivi kwamba tungepaswa sote kuwa wenye uwezo kabisa wa kuitumia ili kufundisha yale Mungu anataka kwetu. Wahubiri wengi watakuwa bila shaka na pendeleo la kuongoza funzo la Biblia kwa msaada wa broshua hiyo.

15 Watu fulani wanaofikiri kutokuwa na wakati wa kujifunza kitabu Ujuzi watakuwa labda tayari kutumia wakati mdogo wa mazungumzo kwenye funzo la broshua Anataka. Watafurahia yale watakayojifunza. Katika kurasa mbili tu au tatu, watapata jibu kwa maulizo ambayo watu wanajiuliza tangu karne nyingi: Mungu ni nani? Shetani ni nani? Ni nini mapenzi ya Mungu kwa ajili ya dunia? Ufalme wa Mungu ni nini? Jinsi gani kupata dini ya kweli? Ijapokuwa broshua inaonyesha ukweli katika maneno mepesi, ujumbe uliomo ni wenye nguvu sana. Ina nukta za msingi ambazo wazee watachunguza pamoja na watu wanaopenda kubatizwa na inaweza kutumiwa kama kikanyagio kwa ajili ya funzo kamili zaidi kwa msaada wa kitabu Ujuzi.

16 Ili kutoleo funzo wakati wa ziara ya kurudia, inatosha tu sisi kusema: “Je! unajua kwamba kwa kujiwekea dakika fulani tu unaweza kupata jibu kwa ulizo la maana la kibiblia?” Kisha tuulize ulizo kati ya yale ambayo yanapatikana mwanzoni mwa mojawapo ya masomo ya broshua. Kwa mfano, ikiwa tunazungumza na mtu mzee-mzee tungeweza kusema: “Tunajua kwamba zamani Yesu aliponyesha watu. Lakini atafanya nini katika wakati ujao kwa ajili ya wagonjwa? watu wazee-wazee? wafu?” Tunapata jibu kwa maulizo hayo katika somo la 5. Udadisi (kupekuwa mambo) wa mtu anayependezwa na mambo ya dini labda utaamshwa na ulizo: “Je! Mungu anasikiliza sala zote?” Somo la 7 linajibu kwa ulizo hilo. Washiriki wa familia watataka kujua: “Mungu anataka nini kwa wazazi na watoto?” Watajua hilo kwa kujifunza somo la 8. Kuna maulizo mengine kama vile: “Je! wafu wanaweza kuzuru wale wanaoishi?” (somo 11); “Kwa nini kuna dini nyingi sana zinazojidai kuwa za Kikristo?” (somo 13); na “Unapaswa kufanya nini ili uwe rafiki ya Mungu?” (somo 16).

17   Tusingoje ili Kufanya Ziara za Kurudia: Ni kwa muda gani tungepaswa kungoja kabla ya kufanya ziara ya kurudia? Wahubiri fulani wanarudi siku moja au mbili kisha kupita kwao kwa mara ya kwanza. Wengine wanarudi baadaye katika mchana ule ule! Je! ni mapema sana? Kwa ujumla, inaonekana kwamba watu hawashangae na hilo. Mara nyingi, ni mhubiri anayehitaji kuwa na mwelekeo zaidi wa kutazamia mema na kujipatia ujasiri kidogo. Tuone mambo fulani yaliyoonwa.

18 Mhubiri mmoja wa miaka 13 alikuwa akihubiri nyumba kwa nyumba alipowaona wanawake wawili waliokuwa wakijitembeza. Akikumbuka kwamba tunatiwa moyo kuhubiri kwa watu haidhuru mahali gani wanapopatikana, aliwakaribia wanawake hao barabarani. Waliguswa moyo na ujumbe wa Ufalme na wote wawili walikubali nakala ya kitabu Ujuzi. Ndugu huyo kijana alipata anwani zao, na alikwenda kuwaona siku mbili baadaye na alianzisha funzo la Biblia na kila mmoja wao.

19 Dada mmoja, kwa upande wake, anachukua mipango ili kurudi kuzungumza na msikilizaji wake juma lifuatalo. Lakini siku moja au mbili kisha kuonana kwa mara ya kwanza, anarudi kumuona ili kumtolea gazeti linaloeleza habari waliyozungumzia wakati wa nyuma. Anamwambia mtu: “Makala hii ilivutia uangalifu wangu na nilifikiri kwamba ungefurahi kuisoma. Siwezi kuzungumza sasa lakini nitarudi Siku ya Tatu kisha-mchana kama tulivyosikilizana. Je! bado unakubali?”

20 Mtu anapoonyesha kupendezwa kwa ajili ya ukweli, tunaweza kuwa hakika kwamba atapambana na upinzani kwa namna moja au nyingine. Kwa kurudi haraka baada ya kuonana kwetu kwa mara ya kwanza, tutamtia nguvu kwa kumsaidia kusimama imara dhidi ya mikazo ya washiriki wa familia yake, marafiki zake wa karibu, n.kCette portion a été omise, jusqu’au paragraphe 34.

21 Ujasiri ni sifa ya muhimu ili kupata matokeo katika utendaji wa ziara za kurudia. Jinsi gani kuupata? Mtume Paulo anajibu kwa kusema kwamba ‘tujipe ujasiri’ kwa kutangazia wengine habari njema “kwa njia ya Mungu wetu.” Ikiwa tunahitaji kufanya maendeleo kwa upande huo, tusali ili kupokea msaada wa Yehova. Kisha, kulingana na sala zetu, tufuatie kupendezwa. Yehova atabariki hakika bidii yetu!

[Box on page 3]

Jinsi ya Kupata Matokeo kwa Msaada wa Ziara za Kurudia

■ Tuonyeshe kwamba tunapendezwa kibinafsi na kwa kwelikweli na watu.

■ Tuchague habari fulani ya kibiblia yenye kuvutia kwa ajili ya mazungumzo.

■ Tuweke kila mara msingi kwa ajili ya ziara ifuatayo.

■ Tuendelee kumfikiria mtu kisha kuachana naye.

■ Turudi baadaye siku moja au mbili ili kufuatia kupendezwa.

■ Tukumbuke kwamba mradi wetu ni kuanzisha funzo la Biblia.

■ Tusali ili kupokea msaada kwa ajili ya kujipa ujasiri katika utendaji huo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine