Umati Mkubwa Unaongezwa
1 Kama vile kwenye Karne ya Kwanza, kutaniko la Kikristo linapata leo ongezeko la ajabu. (Mdo. 2:41; 4:4) Mwaka wa nyuma, wahubiri wapya 366,579 walibatizwa, hiyo ikiwa wastani zaidi ya waliobatizwa 1,000 kila siku! Zaidi ya milioni moja ya watu walibatizwa muda wa miaka mitatu ya nyuma. Hakika, Yehova anaendelea kuongeza umati mkubwa wa waamini.—Mdo. 5:14.
2 Wapya wengi, wasio na ujuzi mwingi wa maisha ya Kikristo, wanahitaji kupokea msaada na mazoezi ya wale walio na nguvu katika imani. (Rom. 15:1) Kati ya Wakristo wa kwanza, wamoja hawakuweza ‘kusonga mbele kwenye ukomavu’, hata miaka baada ya ubatizo wao. (Ebr. 5:12; 6:1) Ni kwa sababu hiyo Paulo alikazia, katika barua yake kwa Waebrania, mambo katika hayo Wakristo wanapaswa kusonga mbele kiroho. Ni mambo gani, na ni msaada gani unaweza kutolewa?
3 Kupata Mazoea Mazuri ya Funzo: Kulingana na mafundisho ya Paulo, ili kuwa mwanafunzi mzuri inafaa kujifunza kwa namna yenye bidii, kurudilia yale tunayojifunza na kutumia “chakula kigumu” ambacho tengenezo la Yehova linatoa. (Ebr. 5:13, 14; ona Mnara wa Mlinzi wa Agosti 15, 1993, kur. 12-17) Kwa kuwa na mazungumzo ya kiroho na wapya na kwa kushiriki nao hazina za ukweli ambazo tulivumbua kwa kujifunza kibinafsi, tutawapa bila shaka tamaa ya kupata mazoea mazuri ya funzo. Mara kwa mara, labda tungeweza kumualika mpya kujiunga nasi kwenye funzo letu la kibinafsi au la kifamilia.
4 Kuhudhuria kwa Ukawaida Kwenye Mikutano: Kielelezo chetu cha uaminifu na maneno yetu yenye kutia moyo yanayosemwa kwa upendo yatawasaidia washiriki wapya wa kutaniko kuwa chonjo (wangalifu) katika jambo lingine linalotajwa na Paulo: “zoea” la wengine kukosa mikutano ya Kikristo. (Ebr. 10:24, 25) Tuwasaidie kutambua kwamba mikutano ni njia yao ya mawasiliano ya kiroho pamoja na kutaniko. Tuchukue hatua ya kufanya ili kwamba wajisikie kuwa wenye kukaribishwa kati ya akina ndugu.
5 Kusema na Yehova Tukiwa na Uhakika: Ili kushindana na udhaifu mbalimbali wa mwili na makosa ya utu wetu, tunapaswa kutafuta msaada wa Yehova katika sala, kwa kumuonyesha mawazo yetu ya ndani kabisa na mahangaiko yetu ya moyoni zaidi. Wapya wanapaswa kujifunza kwamba wanapomsihi Yehova awasaidie, kama vile Paulo anavyotuhimiza kufanya hivyo, hawapaswi kuacha. (Ebr. 4:15, 16; 10:22) Kwa kueleza sisi wenyewe binafsi hali tulizokabiliana nazo kwa upande huo, tutajenga imani yao kwamba Yehova anasikiliza sala zinazotoka moyoni.
6 Kuweka Wakati kwa Ajili ya Huduma: Paulo alionyesha pia kwamba kwa ‘kumtolea sikuzote Mungu dhabihu ya sifa’ tunajitia nguvu kwa upande wa kiroho. (Ebr. 13:15) Je! tunaweza kupendekeza kwa mhubiri mpya kujiunga nasi katika programu ya kila juma ya mahubiri? Labda tungeweza kujitayarisha pamoja kutoa ujumbe au kuchunguza sehemu fulani ya huduma ambayo hajapima bado.
7 Umati mkubwa ulioongezeka unatokeza shangwe kubwa. Kwa kujitia kabisa ili kutoa mazoezi na kutia moyo washiriki wapya wa kutaniko, tutawasaidia kujijengea imani yenye nguvu, ya lazima kwa “kuhifadhi hai nafsi.”—Ebr. 3:12, 13; 10:39, TUM.