Msaada Unaopatikana kwa Utayari
1 Anna, aliye dada mkristo ambaye mume ni asiyeamini, alikuwa na kazi yake ya kimwili iliyomchukua wakati mwingi, alikuwa na matatizo ya kuhudhuria mikutano ya Kikristo kikawaida, kushiriki katika huduma, na kujifunza Neno la Mungu. Dada huyo ingawa aliendelea kumpenda Yehova, alifikia kuwa mhubiri asiyetenda. Kwa furaha, yeye alipata msaada wa kiroho kutoka kwa wazee wenye kujali.
2 Kukubali msaada wa kiroho unaotolewa kupitia kutaniko kunaonyesha kwamba mtu anamtegemea Yehova mwenyewe. Kwa kuiga njia ya Yesu Kristo ya kushughulikia wengine kwa upendo, wazee katika kutaniko wanatafuta nafasi za kutoa kitia-moyo na msaada unaofaa kwa wale wanaopambana na matatizo ya kufuatilia utendaji mbalimbali wa kiroho. (1 The. 5:14) Mara nyingi, neno la kifadhili linalotegemea maandiko yenye vitia-moyo linaweza kuwa ndilo jambo linalohitajiwa. Kuchukua hatua ya kutegemeza wale walio dhaifu kwa muda ni jambo linalohusu Wakristo wote, wala si wazee peke yao. Bila shaka kila mmoja wetu amekwisha kujionea nguvu ya “neno linalosemwa wakati unaofaa.”—Met. 25:11; Isa. 35:3, 4.
3 Chukua Hatua: Kuonyesha hangaiko lenye upendo kwa wale wanaohitaji msaada kunaomba kuchukua hatua, kuonyesha hisia-mwenzi, na kuwa mwenye bidii. Yonathani alipojua kwamba Daudi alikuwa katika hali ngumu, “akasimama, akaenda kwa Daudi kule Horeshi, ili autie nguvu mkono wake.” (1 Sam. 23:15, 16) Saidia wengine kwa njia ya upole. Maneno yanayochochewa na hangaiko la kweli kuhusu wengine yanaleta matokeo mazuri. Zaidi ya hayo, Yesu alieleza wazi kwamba jitihada zenye bidii na zenye kusudi zinatiwa ndani katika kusaidia ndugu au dada wa kiroho. (Luka 15:4) Tamaa ya kweli ya kupenda kumsaidia mtu mwingine itatuchochea kudumu katika kutoa msaada hata ikiwa maendeleo hayaonekani kwa haraka.
4 Ni jambo lenye kutia moyo sana tunapochukua hatua ya kuwaalika wengine, kama vile washiriki wa funzo letu la kitabu, ili wajiunge nasi katika huduma. Tunaposaidia mtumishi mwenzetu wa Yehova ili ashiriki katika huduma, tunaweza kutumia nafasi hiyo ili kumtia moyo afanye mengi. Nyakati kama hizo zenye kufurahisha ambazo tunapitisha pamoja katika utumishi wa Yehova ni zenye kutia moyo hasa kwa wale wanaorudilia tena usawaziko wa kiroho.
5 Mpango Wenye Upendo: Wale ambao hawakushiriki katika kazi ya kuhubiri au hawakushirikiana na kutaniko kwa muda fulani, wanaweza kuhitaji msaada wa ziada ili kujenga imani yao. Kujifunza Biblia pamoja nao kwa kutumia kichapo kama vile Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli, Mkaribie Yehova, au Biblia Inafundisha Nini Hasa? huenda liwe ndilo jambo linalohitajiwa kabisa. Kwa kuwa tayari yeye ni mwenye kubatizwa, kwa kawaida si jambo lenye kufaa kwamba funzo liendelee kwa kipindi kirefu. Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko inapaswa kuwa na uangalifu ili kuona ni nani atakayefaidika na mpango huo.—Ona Visanduku vya Maulizo katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 1998 na ya Novemba 2000.
6 Anna, aliyetajwa hapo juu, alikubali kwa shukrani msaada aliotolewa na wazee wa kujifunza Biblia pamoja na dada mmoja aliye mkomavu kiroho. Funzo hilo liliongozwa mara nne tu ili kumsaidia amkaribie Yehova tena. Alianza tena kuhudhuria mikutano ya kutaniko na akarudiwa tena na tamaa yake ya kumsifu Yehova Mungu peupe. Dada huyo aliye mkomavu alimsaidia Anna katika huduma kwa kumchukua amsindikize kwenye mafunzo mengine hadi alipopata nguvu vya kutosha ili kuhubiri nyumba kwa nyumba. Msaada huo ndilo jambo alilohitaji ili arudilie tena utendaji wake mbalimbali wa kiroho.
7 Kuimarisha wale walio katika uhitaji kunatokeza baraka nyingi kwa wote. Mtu anayesaidiwa anapata furaha ya kumkaribia Yehova na kuhusishwa tena katika utendaji mbalimbali wa tengenezo Lake. Wazee wanafurahi kuona maendeleo hayo ya kiroho. (Luka 15:5,6) Washiriki wa kutaniko wanaunganishwa katika umoja kwa kuwa kila mmoja anajali mwenzake kwa upendo. (Kol. 3:12-14) Tuna sababu nzuri za kumwiga Yehova, akiwa msaada unaopatikana kwa utayari.—Efe. 5:1.
[Maulizo ya Funzo]
1. Hali ya kiroho ya mtu inawezaje kudhoofika?
2. Ni katika njia gani Wakristo wote wanaweza kuonekana kuwa msaada unaopatikana kwa utayari?
3, 4. Ni mambo gani yanayoombwa katika kusaidia wengine, na tunawezaje kufanya hivyo?
5. Katika hali fulani, wazee wanaweza kutoa msaada gani?
6. Namna gani dada Anna alipata tena nguvu za kiroho?
7. Ni baraka gani zinazotokana na kuimarisha wengine kiroho?