Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/98 uku. 7
  • Majibu Kwa Maulizo Yenu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Majibu Kwa Maulizo Yenu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Msisahau Wale Ambao Wameacha Kutenda
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Kisanduku cha maulizo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • “Munirudilie”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Tuwasaidie Watumikie Tena
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 11/98 uku. 7

Majibu Kwa Maulizo Yenu

◼ Je! lingali jambo lenye kufaa kujifunza Biblia na ndugu au dada wasiotenda mshiriki mmoja wa Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko anapoomba hivyo?

Wazee wanalo daraka la kuchunga washiriki wa kutaniko, kutia ndani wale ambao wamekuwa wasiotenda. Wanawatembelea na kufikiri juu ya msaada wa binafsi wanaouhitaji. Wakati mwingine, linaonekana kuwa jambo la lazima kupendekeza funzo la Biblia kwa mtu asiyetenda. Kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu chaonyesha, kwenye ukurasa 103, kwamba Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko ndiyo inayoamua ni nani atakayetegemezwa kwa njia hiyo.

Mwangalizi wa utumishi ataamua ni nani anayefaa kutoa msaada huo, ni habari gani zitakazochunguzwa na ni kichapo gani kitakachokuwa chenye kufaa zaidi. Labda yule aliyefundisha hapo kabla mhubiri huyo asiyetenda au mtu mwingine ambaye mhubiri huyo anamjua na kumheshimu angekuwa mwenye kufaa ili kumsaidia. Labda dada mwenye ustadi na mwenye kukomaa ataombwa asaidie dada asiyetenda. Kwa kawaida, si jambo la lazima mhubiri mwingine asindikize yule anayeongoza funzo. Mtu aliyechaguliwa aongoze funzo anapojulishwa, anaweza kuhesabu wakati wake, ziara za kurudia na funzo.​—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 1988, ukurasa 3.

Kwa kuwa yule anayejifunza ni mtu aliyebatizwa, kwa kawaida si jambo lenye kufaa kwamba funzo liendelee kwa kipindi kirefu cha wakati. Mradi ni kusaidia asiyetenda arudilie kuhudhuria mikutano na kuwa tena mhubiri wa habari njema aliye wa kawaida. Mwangalizi wa utumishi ataangalia kuendelea kwa mafunzo ya aina hiyo. Msaada huo wenye kujaa upendo ungepaswa kufanya akina ndugu na dada watimize wajibu wao mbalimbali kwa Yehova na kuwa wenye “kutia mizizi na kuimarishwa” katika kweli.​—Efe. 3:17; Gal. 6:5.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine