Majibu Kwa Maulizo Yenu
◼ Je! lingali jambo lenye kufaa kujifunza Biblia na ndugu au dada wasiotenda mshiriki mmoja wa Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko anapoomba hivyo?
Wazee wanalo daraka la kuchunga washiriki wa kutaniko, kutia ndani wale ambao wamekuwa wasiotenda. Wanawatembelea na kufikiri juu ya msaada wa binafsi wanaouhitaji. Wakati mwingine, linaonekana kuwa jambo la lazima kupendekeza funzo la Biblia kwa mtu asiyetenda. Kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu chaonyesha, kwenye ukurasa 103, kwamba Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko ndiyo inayoamua ni nani atakayetegemezwa kwa njia hiyo.
Mwangalizi wa utumishi ataamua ni nani anayefaa kutoa msaada huo, ni habari gani zitakazochunguzwa na ni kichapo gani kitakachokuwa chenye kufaa zaidi. Labda yule aliyefundisha hapo kabla mhubiri huyo asiyetenda au mtu mwingine ambaye mhubiri huyo anamjua na kumheshimu angekuwa mwenye kufaa ili kumsaidia. Labda dada mwenye ustadi na mwenye kukomaa ataombwa asaidie dada asiyetenda. Kwa kawaida, si jambo la lazima mhubiri mwingine asindikize yule anayeongoza funzo. Mtu aliyechaguliwa aongoze funzo anapojulishwa, anaweza kuhesabu wakati wake, ziara za kurudia na funzo.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 1988, ukurasa 3.
Kwa kuwa yule anayejifunza ni mtu aliyebatizwa, kwa kawaida si jambo lenye kufaa kwamba funzo liendelee kwa kipindi kirefu cha wakati. Mradi ni kusaidia asiyetenda arudilie kuhudhuria mikutano na kuwa tena mhubiri wa habari njema aliye wa kawaida. Mwangalizi wa utumishi ataangalia kuendelea kwa mafunzo ya aina hiyo. Msaada huo wenye kujaa upendo ungepaswa kufanya akina ndugu na dada watimize wajibu wao mbalimbali kwa Yehova na kuwa wenye “kutia mizizi na kuimarishwa” katika kweli.—Efe. 3:17; Gal. 6:5.