Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 7/96 uku. 1
  • Tuwasaidie Watumikie Tena

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuwasaidie Watumikie Tena
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Msisahau Wale Ambao Wameacha Kutenda
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • “Munirudilie”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Majibu Kwa Maulizo Yenu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Kisanduku cha maulizo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 7/96 uku. 1

Tuwasaidie Watumikie Tena

1 Akitambua kwamba hatari ya kiroho ilikuwa ikiangalia washiriki wenzake Wakristo, mtume Paulo aliandika: “Tayari ni saa ya nyinyi kuamka kutoka katika usingizi, kwa maana sasa wokovu wetu uko karibu zaidi kuliko tulipopata kuwa waamini.” (Rum. 13:​11, NW) Paulo alikuwa akiangaikia ndugu zake ambao walikuwa wenye kuchoka kiroho; hangaiko lake lilikuwa ni kuwatia moyo wawe tena wenye kutenda.

2 Tunaweza hakika kusema kwamba usiku wenyewe kwa ulimwengu huu wa kale unasonga mbele na kwamba mapambazuko ya ulimwengu mpya yanachomoza kwenye upeo wa macho. (Rum. 13:12) Tunazo sababu nzuri zakuangaikia ndugu zetu walioacha kushiriki karibu nasi katika mahubiri ya habari njema. Mwaka jana, katika Shirikisho ya Amerika peke yake, zaidi ya wahubiri 27,000 walirudi tena kuwa watendaji. Jinsi gani tunaweza kuwasaidia Wakristo wengine wasiotenda kumtumikia tena Yehova?

3 Yale Wazee Wanaweza Kufanya: Wakristo walio wengi wasiotenda hawakuacha ukweli; walisimamisha tu kuhubiri kwa sababu ya vivunja-moyo, matatizo ya kipekee, kupenda vitu vya kimwili au mahangaiko mengine ya maisha. (Lk. 21:34-36) Kwa kadiri iwezekanavyo, ni vizuri zaidi kuwasaidia wahubiri kabla ya wao kuwa wasiotenda. Ikiwa mhubiri anaanza kutoa si kwa ukawaida ripoti ya utendaji, mwandishi wa kutaniko atajulisha kiongozi wa funzo lake la kitabu. Mipango itachukuliwa ili kumtembelea katika ziara ya uchungaji. Wazee wangepaswa kujikaza kujua sababu isiyoonekana ya tatizo na msaada ambao unapaswa kutolewa.​—Ona Mnara wa Mlinzi wa Septemba 15, 1993, kurasa 20-3.

4 Jinsi Tunavyoweza Kutoa Msaada Wetu: Walio wengi wetu wanajua mtu fulani ambaye amekuwa asiyetenda. Labda ni mtu ambaye tulikuwa naye uhusiano wa karibu sana wakati wa nyuma. Nini la kufanya ili kumsaidia? Kwa nini usisimame kwake kwa ajili ya ziara fupi? Mwambie kwamba mnasikitika kukosa ushirika wake. Uwe mwenye furaha na mwenye kujenga. Mjulishe kwamba mnamuhangaikia bila hata hivyo kumwambia kwamba yeye ni mgonjwa, kiroho. Elezeni mambo yaliyoonwa yenye kujenga au mambo mengine yenye kutia moyo ambayo kutaniko linatimiza. Mweleze kwa shauku juu ya kusanyiko la wilaya “Wajumbe wa Amani ya Kimungu.” Mtie moyo kuhudhuria kwenye kusanyiko la wilaya ikiwa bado halijafanyika. Kushirikiana mara tena na kutaniko kutamsaidia labda zaidi kwa njia nyingine iwayo yoyote. Mtolee pendekezo la kumshindikiza mikutanoni. Julisha wazee jinsi alivyoitikia.

5 Mkristo asiyetenda anaporudilia mikutano, bila shaka yeye anakosa starehe kwa kuona watu fulani aliowajua. Msimuulize “Ulikuwa wapi?” Badala yake, msaidieni ajisikie kwamba amepokelewa vizuri. Mtieni katika mazungumzo. Mumwonyeshe kwa wale asiojua. Kaeni pembeni naye wakati wa mkutano na iweni hakika kwamba ana kitabu cha wimbo na pia vichapo mnavyojifunza. Mtieni moyo arudi tena na mtoleeni msaada wenu ikiwa kuna uhitaji.

6 Kwa kuwa wana shauku ya kindugu ya kina kirefu kwa wale wanaopotea, Yehova na Yesu wanashangilia wakati watu wa namna hiyo wanapopona kiroho. (Mika 3:7; Mt. 18:12-14) Tutapata shangwe ileile ikiwa tunafikia kuwasaidia Wakristo kumtumikia tena Yehova.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine