Maswali Yanayohusiana Na Urafiki Na Mtu Wa Jinsia Tofauti Kwa Ajili Ya Ndoa—Jinsi Gani Kuepuka Matatizo Yake?
1 Ndoa, kama vile vyama vingine vyenye chanzo cha kimungu, ina kusudi la kumuheshimu Mwanzilishi wayo, Yehova, “ambaye kwake kila familia mbinguni na duniani hupata jina layo.” (Efe. 3:15) Ole ni kwamba, tangu uasi katika Edeni, ndoa nyingi zinamalizika kwa kutofanikiwa. Hali inatokana na ukosefu wa ujuzi, wa mashauri na uongozi ufaao. Inatokana pia na sababu katika mwenendo unaochaguliwa muda wa kipindi kinachotangulia ndoa.
2 Urafiki na Mtu wa Jinsia Tofauti: Watu wawili wanapofanya urafiki kwa ajili ya ndoa, heshima ya kanuni za Biblia kuhusiana na swali hilo inaweza kuwa yenye manufaa kwa ajili ya maisha yao ya wakati ujao. Kwa sababu mtu “mwenye akili anaangalia sana namna anavyokwenda,” Mkristo ambaye anapenda kumheshimu Yehova atakuwa mwangalifu kwa urafiki wake na mtu wa jinsia tofauti ili kwamba urafiki huo usilete suto juu ya kutaniko na juu ya jina la Yehova. (Mez. 14:15, ZSB) Wakristo wengine wanakuwa na urafiki wa nguvu sana na mtu wa jinsia tofauti, ijapokuwa wao si tayari kwa ajili ya ndoa. Inaonekana kwamba wengi kati yao hawajui urafiki na mtu wa jinsia tofauti unamaanisha nini, kwamba urafiki huo unaweza kuwa ikiwa tu watu wawili wanatamani kuoana.
3 Wengi hutoa maana mbalimbali kwa urafiki na mtu wa jinsia tofauti: ‘Kutoka pamoja na mtu wa jinsia nyingine’; ‘kujifunza kujuana vizuri sana.’ Kikizungumzia juu ya uhusiano kati ya mvulana na msichana, kitabu fulani kinasema: “Uhusiano mvulana-msichana . . . mara nyingi unafanyika kupitia maneno madogo-madogo, barua au kupitia simu. Njia zote hizo za mawasiliano ni zenye kuvutia [vijana], kwani zinawezesha kuzoeana kwingi mno kwa ukaribu sana watu wakiwa hata mbali.” Hivyo, kutokana na maana inayotolewa na kamusi, kana kuwa “uhusiano wa kijamii kati ya watu wawili wa jinsia tofauti,” Wakristo fulani wanafanya urafiki wa kwelikweli na mtu wa jinsia tofauti kupitia mazungumzo ya kawaida au kwa kuonyeshana shauku nyingine ya kimahaba isiyotakwa, kwa njia ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja. Ikiwa mtu si tayari kwa ajili ya ndoa, mwenendo wa namna hiyo unaweza kuongoza kwenye mwenendo mpotovu. Kuzoeana kwingi mno kwa ukaribu sana kunaweza kuwa na matokeo yenye kusikitisha zaidi. Kijana mwanamume mmoja alijaribu kufariji rafiki wa kike aliyemfunulia siri juu ya mengine ya matatizo yake. Muda si muda, walikuwa wakidodosana (kukumbatiana) kimapenzi. Matokeo yakawa nini? Dhamiri zilizosumbuka na hisia mbaya kati yao. Kwa wengine, mahusiano ya kingono yametokea. Uchunguzi mmoja uliofanywa na gazeti Psychology Today ulifunua hivi: “Karibu nusu ya waliojibu wameona urafiki ukigeuka kuwa uhusiano wa kingono.” Kwa kweli, “karibu theluthi moja (asilimia 31) waliripoti walifanya ngono na rafiki katika mwezi uliopita.”
4 Isemwe nini kwa yule aliye tayari kwa ajili ya ndoa na anakwenda kutafuta mwenzi wa ndoa mbali, katika kutaniko lingine? Habari kutoka katika sehemu mbalimbali za eneo zinaonyesha kwamba akina ndugu waliowesha mabinti wao kwa watu wa ulimwengu waliojitambulisha kuwa ati “Mashahidi wa Yehova,” au watengwa. Ndugu hao walivuna matokeo mabaya. Kwa nini waliangukia ndani ya mitego hiyo? Wamoja walifikiri kwamba kwa kuwa ndoa ni jambo la kibinafsi, wazee hawakuwa na haki ya kutupia jicho juu ya yoyote ya sehemu zayo. Hata hivyo, wakati matatizo yanapotokea au kwamba wale walio na mapendeleo wanapoondolewa yenyewe, wanakimbilia haraka kwa wazee wale wale katika kusudi la kupata msaada. Kwa kuwa, kujikinga na ugonjwa ni vema zaidi kuliko kuutunzisha, wangaliweza kuepuka matatizo kwa kushirikiana na wachungaji. Hakika, ingawa kwa kweli wao ‘sio mabwana-wakubwa juu ya imani yao, wazee hata hivyo ni wafanyakazi wenzi kwa shangwe yao.’—2 Kor. 1:24.
5 Daraka la Wazazi: Wasimamizi wa binti ambaye anaombwa mkono wanaweza kufanya nini? Wanaweza kujifunza mengi kupitia kielelezo kifuatacho. Katika kutaniko fulani, wazee walikuwa na mashaka juu ya mwenendo wa mtu fulani aliyejidai kuwa “Mkristo” ambaye alikuwa ametoka karibuni kuoa kisheria katika kutaniko lao. Walituma mtu ili kwenda kutafuta habari juu ya hali ya kiroho ya mwanamume huyo. Hatua hiyo ilifunua kwamba mwanamume huyo alikuwa tu mwanafunzi wa Biblia. Alifuta kwa ukorofi katika barua ya wazee nafasi iliyomtambulisha kuwa mhubiri asiyebatizwa, kwa kusudi la kuweza kuoa. Ingawa alikuwa mwenye kushikwa na mshangao na kufadhaika, msimamizi wa binti huyo alipoteza mapendeleo yake ya utumishi ingawa aliomba rufani yake ya uamuzi. Alioesha binti yake na mtu wa ulimwengu. (Kumb. 7:3, 4; 2 Kor. 6:14, 15) Ni vizuri hivyo kwamba ushirikiano uwe kati ya wazazi na wazee ambao wanaweza kuwa wenye kujua mambo fulani kuhusu hali ya kiroho ya mchumba au wanaoweza, ikiwezekana, kuuliza kutaniko anakotoka.
6 Jinsi ya Kuepuka Matatizo: Ni jambo lisilotiliwa shaka kwamba wazazi ndio walio nafasi nzuri zaidi ili kuamua ikiwa wataruhusu au hapana mtoto wao afanye urafiki na mtu wa jinsia tofauti kwa ajili ya ndoa. Inafaa hata hivyo kwamba wafahamiane, ikiwezekana, na watu wote ambao binti yao anatembelea kikawaida na kuona katika kusudi gani wanarafikiana, ikiwa ni watu wa jinsia tofauti. Inawezekana kwamba mvulana anafanya urafiki na binti yao pasipo wao kutambua. Wamoja wanatumia neno “mwahidiwa wangu” ili kusema juu ya mtu waliyofanya naye ahadi kwa siri na pasipo maafikiano ya wazazi. Tangu wakati huo, “waafikianaji au waahidianaji” hao wanapelekeana mialiko na wanakutana, mara nyingi pasipo mtu mwingine wa kuwashindikiza huku wakiogopa kwamba siri yao isijulikane. Wanatupilia mbali hivyo mashauri yote kuhusu hatari inayowakabili. Kwa kuwa wazazi watatoa hesabu kwa Yehova, hawatafunga macho kwa mwenendo wa namna hiyo wa watoto wao. Ikiwa hata hivyo hilo linatukia, wazazi watajibu juu ya hilo mbele ya wazee, hata ikiwa kwamba ndoa ni jambo la kibinafsi kati ya watu wawili au familia mbili. Ni vivyo hivyo na Wakristo wanaokubaliana na mwenendo wa namna hiyo.
7 Mwenendo wa namna hiyo unaweza kuwa na matokeo mabaya juu ya kutaniko. Kwa wazi, kufanya urafiki na mtu wa jinsia tofauti pasipo kusudi la kufunga ndoa kunaweza kuongoza kwenye uchafu, kwenye mwenendo mpotovu na kwenye uasherati. Hilo halitaepukika machoni pa watu wa ulimwengu na matokeo yatakuwa suto kwa jina la Yehova na kikwazo kwa utangazaji wa habari njema kwa watu ambao ni washuhuda wa mwenendo huo mpotovu. (1 Tim. 5:25b; Lk. 17:1, 2; Rom. 2:23, 24) Kwa kibinafsi, zaidi ya kupoteza uhusiano mzuri pamoja na Yehova, kuna uhakika wa kwamba yule anayejitoa katika mwenendo huo anaingilia haki zake na zile za mtu wa jinsia tofauti anayefanya naye urafiki. Biblia inasema kwamba tulitupilia mbali matendo ya giza na mambo yote yanayofanyika katika siri. (Rom. 13:14; Efe. 5:7, 8, 11, 12) Ikiwa mwenendo wetu haututofautishe na watu wa ulimwengu, ukweli si tena ndani yetu. Katika hali hiyo, wale waliowekwa rasmi na roho watapaswa labda kuingilia kati ili kutukemea. Hilo linaweza kuepukika ikiwa tunashirikiana kwelikweli nao.
8 Uchumba kama vile ndoa yanabaki mambo ya kibinafsi wakati amani na utulivu wa kutaniko haumo katika hatari. Wakati hali inakuwa jiwe la kukwaza kwa kutaniko, lililokuwa jambo la kibinafsi litafuatwa na wazee wa kutaniko kwa ajili ya kulinda amani ya washiriki walo wote.
[Caption on page 4]
“Inawezekana wenzi wa ndoa wawe na bahati ya kufunga ndoa iliyo imara na yenye furaha ikiwa wanaanza maisha yao wawili kwa kujuana vizuri vya kutosha utu wa ndani wa mmoja na mwingine.”—Journal du mariage et de la famille (angl.).