“Nani Atakayekwenda Kwa Ajili Yetu?”
Wakati Yehova alipouliza ulizo hilo, Isaya alijibu papo hapo: “Mimi hapa! Nitume Mimi.” (Is. 6:8, UV) Leo, kwa kuwa mavuno ni mengi, mwito huohuo unatolewa. Kuna uhitaji mkubwa sana wa watumishi wa wakati wote, mapainia wa kawaida! (Mt. 9:37) Je! wewe unataka kutumikia? Ikiwa ndiyo, kwa kuwa Septemba 1 ndiyo mwanzo wa mwaka wa utumishi 1998, ungekuwa wakati ufaao kuanzisha utumishi huo. Kwa nini kutokuwaambia wazee kwamba unatamani kupata fomu ya ombi?