Mikutano Ya Utumishi Ya Agosti
Juma Toka Agosti 4
Wimbo 6
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa ya Huduma Yetu ya Ufalme. Kueleza ripoti ya utumishi ya kutaniko ya Julai.
Dak. 15: “Uaminifu Unathawabishwa.” Kwa maulizo na majibu. Kusema juu ya habari inayoripotiwa katika Amkeni! ya Januari 22, 1993, kur. 18-21.
Dak. 20: “Tusaidie Wengine Wapate Faraja.” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Kuambatanisha mafungu 4 na 5 na hali ya mahali penu. Kutayarisha onyesho moja au mawili kwa msingi wa utoaji mbalimbali unaopendekezwa. Kualika washiriki wa hudhurio kueleza jinsi walivyoanzisha mazungumzo juu ya broshua zilezile kupitia njia mbalimbali. Tutatia moyo matumizi ya maneno mepesi na yaliyochaguliwa vizuri ili kuamsha kupendezwa. (Ona Kiongozi cha Shule, uku. 7, § 9-11.) Kusema juu ya broshua nyingine katika stoki kutanikoni, ambazo tunaweza kutolea.
Wimbo 70 na sala ya mwisho.
Juma Toka Agosti 11
Wimbo 5
Dak. 12: Matangazo. Hali ya akaunti. Kifupi cha makala “Tutajifunza Kitabu Furaha ya Familia.”
Dak. 18: “Tuhubiri Mahali Watu Walipo.” Hotuba. Kwa kadiri ya wakati uliopo, tutataja mambo mengine yaliyoonwa kutokana na Kitabu-Mwaka 1997, kur. 43-6.
Dak. 15: Wazazi: Fundisheni Watoto Wenu Tangu Utoto Sana. Mzee anachunguza kanuni za Maandiko zinazokazia ulazima kwa wazazi kufundisha watoto tangu utoto sana. (Mez. 22:6; 2 Tim. 3:14, 15) Wazazi wanaona kwamba inafaa kungoja kwamba watoto wao wawe katika umri wa kuchukua maamuzi yao wenyewe ili kuwatolea malezi mazito ya kibiblia. Ni sababu hiyo kwamba watoto wengi wamepotea katika ulimwengu. Elimu ya kiroho ingepaswa kuanza tangu utoto sana. (g97-SW 3/8 26-7; w88-SW 8/1 12-13) Kuhoji mume na mke wake wanaohangaikia hali ya kiroho ya watoto wao. Kuonyesha kwamba baba ndiye anayeanzisha kwanza mambo, lakini kwamba mke wake na yeye wanatimiza kila mmoja sehemu yake kuhusu kutoa programu ya mafundisho yenye kupatana na yenye kina kirefu kwa watoto wao. Wanafasiria juhudi wanayofanya ili kufundisha ukweli kwa watoto wao kwa kufuata madokezo ya tengenezo ili kuwa na programu yenye kutenda kazi ya mafundisho nyumbani. Mzee anakazia juu ya ulazima wa kutumikisha mashauri ambayo Neno la Mungu linatoa kwa wazazi.—Efe. 6:1-4.
Wimbo 71 na sala ya mwisho.
Juma Toka Agosti 18
Wimbo 14
Dak. 12: Matangazo. Kifupi cha makala “Programu ya Kusanyiko la Mzunguko Lijalo.”
Dak. 13: “Nani Atakayekwenda kwa Ajili Yetu?” Hotuba yenye kutia moyo. Kusema juu ya mwaliko wa kuwa painia wa kawaida na yale yanayoonyeshwa katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 1997, § 16-17. Wale ambao hawawezi kuwa mapainia wa kawaida wanatamani labda kupanga mwezi au miezi katika hiyo watakuwa mapainia wasaidizi katika mwaka wa utumishi ujao.
Dak. 20: Tujitayarishe Kutoa Ushuhuda wa Vivi Hivi. Kila siku, nafasi za kutoa ushuhuda kwa watu ambao tunakutana nao zinajitokeza kwetu. Ikiwa ndivyo ilivyo, labda tunatambua kwamba hatuna Biblia wala kichapo. Tuwe wenye kuona mambo kimbele. Nyumbani, tuwe na vichapo nafasi mkono unaweza kuvichukua wepesi, karibu na mlango ambako tunapokea wageni wetu. Tuweke mojawapo yavyo ndani ya mfuko mwembamba au mfuko wa mkononi na tuwe navyo au tuviangushe katika matembezi yetu, mahali petu pa kazi. Tuchukue kitu fulani pamoja nasi tunaposafiri katika magari ya watu wote. Tunapofanya safari ya mambo ya biashara, iwe tunakwenda kwenye kusanyiko au kwamba tunakwenda likizoni, tuweke vichapo fulani katika mizigo yetu. Kuchunguza madokezo ya ziada yanayotolewa katika kitabu Kiongozi cha Shule, kur. 80-2, § 11-16. Maonyesho mafupi juu ya namna ya kumkaribia mchuuzi, mfanyakazi mwenzetu, mwanashule mwenzetu, mtu anayesafiri au aliye mapumzikoni.
Wimbo 72 na sala ya mwisho.
Juma Toka Agosti 25
Wimbo 15
Dak. 12: Matangazo. Kukumbusha kila mmoja kutoa ripoti yake ya utumishi. Kusema juu ya toleo la mwezi wa Septemba. Mnamo Septemba, tutafanya juhudi ya pekee ili kuwatembelea tena watu ambao tuliachia broshua mnamo Agosti, kwa ajili ya kuanzisha mafunzo ya Biblia. Kwa msaada wa nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Aprili 1997, kukazia nukta fulani za lazima ili kufanya ziara za kurudia zenye matokeo. Tungepaswa kuanzisha mafunzo kwa msaada wa broshua Anataka au kitabu Ujuzi.
Dak. 15: “Maswali Yanayohusiana na Urafiki na Mtu wa Jinsia Tofauti kwa Ajili ya Ndoa—Jinsi Gani Kuepuka Matatizo Yake?” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji ikitolewa na mzee.
Dak. 18: Tutimize Kikamilifu Huduma Yetu. Hotuba inayotolewa na mwangalizi wa utumishi ikitegemea kitabu Huduma Yetu, kur. 5-8. Kukazia ulazima wa mahubiri na hali yake ya uharaka kwa kuchochea kila mmoja kuchukua kwa uzito madaraka yake ya huduma.
Wimbo 75 na sala ya mwisho.