Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/97 uku. 1
  • Tuhubiri Mahali Watu Walipo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuhubiri Mahali Watu Walipo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tuhubiri Habari Njema Mahali Pote
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Unaweza Kutoa Ushahidi Wakati Haukupanga Kufanya hivyo!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuanzisha Mazungumuzo ili Kuhubiri Wakati Hatukupanga Kufanya Hivyo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Ongeza Furaha Yako katika Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 8/97 uku. 1

Tuhubiri Mahali Watu Walipo

1 Akitambua kazi inayotimizwa na roho ya Mungu katika huduma yake, mtume Paulo alisema: “Mungu akafuliza kuikuza.” Alikubali pia kwamba: “Sisi ni wafanyakazi wenzi wa Mungu.” (1 Kor. 3:​5-9, TUM) Ni pendeleo la ajabu. Jinsi gani tunaweza kuonyesha peupe kwamba tunathamini heshima ya kuwa wafanyakazi wenzi wa Mungu? Kwa kutangaza habari njema kwa watu wote ambao tunakutana nao katika ushuhuda wa nyumba kwa nyumba na popote kwengineko.

2 Tulipokea amri ya ‘kufanya wanafunzi.’ (Mt. 28:19) Ikiwa, wakati tunaposhiriki katika huduma, tunazungumza tu na watu wachache, kuna hatari tuchoke haraka na kuwa na maoni ya kwamba hatutimize jambo lolote. Kinyume na hilo, wakati tunapofaulu kupata watu wengi na kuzungumza nao, tunapata shangwe nyingi kutokana na huduma yetu. Hilo linaomba bidii kwa upande wetu, kwa kadiri ambayo imetupasa kuchukua hatua ya kwenda mahali watu hupatikana kwa namna tuweze kuwakuta.

3 Vielelezo Vinavyotenda Kazi: Tunaweza kutoa ushuhuda sokoni, katika mashamba ya wanyama na vituo vya usafirishaji wa watu wote. Tunaposafiri katika magari ya watu wote, je! sisi ni wenye kujitayarisha ili kutoa ushuhuda safarini? Ndani ya basi inayojaa na watu, Mashahidi wawili waliokuwa wakijielekeza mahali pa mkutano wa utumishi walianza kueleza picha ya kitabu Ujuzi inayoonyesha paradiso na kuzungumzia ahadi mbalimbali za Mungu kuhusu wakati ujao. Kama walivyokuwa wakitazamia, kijana mmoja aliyekuwa pembeni yao alijiunga kwenye mazungumzo. Yale aliyosikia yalimshangaza, na wakati wa kushuka katika basi alikubali kitabu na aliomba atembelewe nyumbani kwake.

4 Wahubiri wengi wanapata shangwe katika ushuhuda wa vivi hivi. Dada mmoja kisha saa sita, alikwenda katika mtaa wa kibiashara na alianza kuzungumza na watu ambao walikuwa wamemaliza kununua lakini ambao walionekana wasiokuwa haraka. Aliangusha vichapo vyote alivyokuwa navyo ndani ya mfuko wake. Mwanamume mmoja aliyekuwa akingoja ndani ya motokaa yake alikubali kwa shangwe magazeti ambayo alimtolea. Alikuwa akihudhuria mikutano wakati wa nyuma na mazungumzo yao yaliamsha kupendezwa kwake.

5 Kutukuza jina la Yehova ni pendeleo. Kwa kuwa wenye juhudi kwa ajili ya mahubiri, tunaonyesha kwamba hatukukosa kusudi la fadhili isiyostahilika ya Mungu kutuelekea sisi. “Sasa ndio wakati wenye kukubalika hasa” wa kuwasaidia wengine; kwa hiyo twende basi mahali watu walipo na tuwatolee ushuhuda kuhusu “siku ya wokovu.”​—2 Kor. 6:1, 2, TUM.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine