Faidika Kikamilifu na Shule Yako
1 Tazama wakati mwakani ambao vijana wengi wanapiga kite kwa kutaabika: “Tayari ni kurudi shuleni tena!” Kurudi darasani mara nyingi humaanisha mwito wa kushindana na pia hofu, lakini kunatoa pia faida nyingi kwa vijana wanaojikaza kufaidika kikamilifu na miaka yao ya masomo.
2 Misingi mizuri ya shule inachangia kwa maendeleo ya kiroho. Yale mtu mzima ana uwezo wa kutimiza yanategemea kwa kadiri kubwa yale aliyoyafanya muda wa ujana wake. Hata kwa upande wa elimu, “lolote lile mtu analopanda, hilo atavuna pia.” (Gal. 6:7, TUM) Vijana ambao wanajifunza sana wanaweza kupata uwezo mwingi wa akili utakaowafanya wawe wa lazima zaidi kwa Yehova.
3 Inafaa kuwa mwangalifu ili kufanya uchaguzi mzuri kwa upande wa masomo. Wazazi wangepaswa kuwasaidia watoto wao kuchagua ufundi mbalimbali ambao utaweza kuwaletea mazoezi yenye kutenda kazi zaidi kuliko ili kufikia miradi ya kiroho. Kwa kukomaza uwezo wao mbalimbali wa akili, vijana watapata faida ya kuwa wenye uwezo wa kutosheleza mahitaji yao huku wakiwa mapainia. Misingi yao ya shule ingepaswa kuwasaidia kumsifu Yehova haidhuru mahali gani wanakomtumikia.
4 Enyi vijana, jaribuni kufaidika kikamilifu na miaka yenu ya masomo, mkilenga shabaha maisha yenye utajiri katika utumishi mtakatifu, na si kazi ya maisha katika ulimwengu. Jikazeni kutumia maisha yenu kwa kufanya mapenzi ya Yehova. Ni hivyo mtafanikisha njia zenu, kwa sifa ya Yehova.—Zab. 1:3.