Vijana—Tumieni Kwa Faida Kipindi Chenu Cha Kusoma Shuleni
1 Unahisi namna gani unapofikiria kurudi shuleni baada ya likizo? Je! wewe ni mwenye hamu ya kutumia kwa faida mwaka mpya wa shule? Je! utatumia nafasi ambazo shule hutoa ili kujulisha kweli kwa wanashule wenzako na walimu wako? Tunaamini kwamba una nia ya kufanya vema zaidi shuleni.
2 Uwe Mwanafunzi Mwema: Ikiwa wewe ni mwenye kujitayarisha vema unapohudhuria masomo na kuwa mwangalifu, utapata faida za kudumu. Timiza bila kukawia migawo unayopewa na mwalimu, lakini usiiruhusu ivuruge utendaji wako wa kitheokrasi.—Flp. 1:10.
3 Anza mwaka wako mpya wa shule kwa kusoma broshua Mashahidi wa Yehova na Elimu. Kisha, wewe au wazazi wako mwaweza kutolea kila mmoja wa walimu wako nakala. Wajulishe kwamba watapata majibu kwa maulizo yao yote. Jambo hilo litawasaidia waelewe kanuni na imani zako, na watashirikiana nawe utumiapo yale uliyofundishwa. Kwa kuongezea, hilo litawahakikishia kwamba wewe na wazazi wako mwatamani kushirikiana nao wanaowasaidia kutwaa elimu yenye kufaa.
4 Uwe Shahidi Mwema: Kwa nini usione shule kuwa eneo lako la mahubiri ya vivi hivi? Mnamo mwaka huu wa shule, mtakuwa na nafasi za pekee za kutoa ushahidi. Mnao ujuzi wa kiroho wa ajabu; kwa kuueneza, ‘mtajiokoa nyinyi wenyewe na wale wawasikilizao pia.’ (1 Tim. 4:16) Kwa kuwa sikuzote na mwenendo wa Kikristo wa kuigwa na kwa kutoa ushahidi kila wakati inapofaa kufanya hivyo, mtajifaidisha nyinyi wenyewe na kufaidisha wengine.
5 Ndugu mmoja kijana alitoa ushahidi wa vivi hivi kwa wanafunzi wenzake katika shule yake. Miongoni mwa wale walioitikia ifaavyo mlikuwamo Mkatoliki, mtu asiyeamini kuwako kwa Mungu, ambaye alizoea kudhihaki walioamini Mungu, na kijana mwenye kuvuta sigareti mfululizo na mwenye kunywa vileo sana. Kwa ujumla, ndugu yetu huyo kijana alisaidia wenzake 15 kujiweka wakfu na kubatizwa![1]
6 Kwa hiyo vijana, jizoezeni kujifunza na kutumika eneo lenu la pekee. Hivyo, mtatumia kwa faida kubwa zaidi kipindi chenu cha kusoma shuleni.
[DO NOT SET] Reference 1. w92 8/1 25.