Usisite
1. Ni nini kinachohitajiwa ili kuhubiria wengine kwenye masomo, na kwa nini?
1 Je, umekwisha kusita kuhubiria wengine kwenye masomo kwa kuwa uliogopa kwamba watakuchekea? Inaomba kuwa na ujasiri ili kuhubiria wengine, zaidi sana ikiwa wewe ni mwenye haya. Ni nini inayoweza kukusaidia?
2. Kwa nini kutumia akili ni kwa lazima ili kuhubiria wengine kwenye masomo?
2 Tumia Akili: Hata ikiwa unaweza kuona masomo kuwa eneo lako la kuhubiri, kumbuka kwamba haitawezekana uzungumuzie mambo ya kiroho na kila mutu kama unavyofanya unapohubiri nyumba kwa nyumba. Kwa hiyo, tumia akili ili kujua ni wakati gani unaweza kusema. (Mhu. 3:1, 7) Unaweza kupata nafasi ya kueleza imani yako munapozungumuzia jambo fulani darasani ao munapopewa mugawo fulani wa masomo. Ao mwanafunzi mwenzako anaweza kukuuliza kwa nini haushiriki katika mambo fulani. Mwanzoni mwa mwaka wa masomo, Wakristo fulani wamejulisha walimu wao kwamba wao ni Mashahidi wa Yehova na wamewatolea vichapo vinavyoeleza mambo tunayoamini. Wengine wametia kichapo fulani kwenye meza yao ili wanafunzi wengine wakione na hivyo wachochewe kuuliza maulizo.
3. Namna gani unaweza kujitayarisha ili kuhubiria wengine kwenye masomo?
3 Ujitayarishe: Ikiwa unajitayarisha, utakuwa na uhakika zaidi. (1 Pet. 3:15) Kwa hiyo, jaribu kufikiria mbele ya wakati maulizo ambayo wanafunzi wenzako wanaweza kukuuliza, na ufikiri kuhusu jinsi unavyoweza kuyajibu. (Met. 15:28) Ikiwezekana, chunga Biblia yako kwenye masomo na vitabu vichache, kama vile kitabu Kutoa Sababu, Vijana Huuliza, buku la 1 na la 2, na vichapo vinavyozungumuzia uumbaji, ili uvitumie unapovihitaji. Omba wazazi wako wapange pia kufanya vipindi vya mazoezi katika ibada yenu ya familia.
4. Kwa nini unapaswa kuendelea kuhubiria wengine kwenye masomo?
4 Usiwazie Wengine Vibaya: Usifikiri kwamba wanafunzi wenzako watakuchekea kila wakati utakapotaka kuwaelezea kweli. Huenda wanafunzi fulani watakuheshimu kwa sababu ya ujasiri wako na wanaweza hata kukusikiliza. Lakini usivunjike moyo ikiwa hakuna mutu anayekusikiliza. Yehova atafurahi kwa kuwa ulijaribu. (Ebr. 13:15, 16) Endelea kumwomba akusaidie ‘uendelee kusema kwa ujasiri wote.’ (Mdo. 4:29; 2 Tim. 1:7, 8) Wazia furaha utakayokuwa nayo utakapopata mutu atakayekusikiliza. Mwishowe mutu huyo anaweza kuwa mutumishi mwenzako wa Yehova!