Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 10/11 uku. 2
  • Usisite

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Usisite
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Vijana—Tumieni Kwa Faida Kipindi Chenu Cha Kusoma Shuleni
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Je, Watoto Wenu Wako Tayari?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Tushiriki Katika Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Shule ya Huduma ya Kitheokrasi Mnamo 2002
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2011
km 10/11 uku. 2

Usisite

1. Ni nini kinachohitajiwa ili kuhubiria wengine kwenye masomo, na kwa nini?

1 Je, umekwisha kusita kuhubiria wengine kwenye masomo kwa kuwa uliogopa kwamba watakuchekea? Inaomba kuwa na ujasiri ili kuhubiria wengine, zaidi sana ikiwa wewe ni mwenye haya. Ni nini inayoweza kukusaidia?

2. Kwa nini kutumia akili ni kwa lazima ili kuhubiria wengine kwenye masomo?

2 Tumia Akili: Hata ikiwa unaweza kuona masomo kuwa eneo lako la kuhubiri, kumbuka kwamba haitawezekana uzungumuzie mambo ya kiroho na kila mutu kama unavyofanya unapohubiri nyumba kwa nyumba. Kwa hiyo, tumia akili ili kujua ni wakati gani unaweza kusema. (Mhu. 3:1, 7) Unaweza kupata nafasi ya kueleza imani yako munapozungumuzia jambo fulani darasani ao munapopewa mugawo fulani wa masomo. Ao mwanafunzi mwenzako anaweza kukuuliza kwa nini haushiriki katika mambo fulani. Mwanzoni mwa mwaka wa masomo, Wakristo fulani wamejulisha walimu wao kwamba wao ni Mashahidi wa Yehova na wamewatolea vichapo vinavyoeleza mambo tunayoamini. Wengine wametia kichapo fulani kwenye meza yao ili wanafunzi wengine wakione na hivyo wachochewe kuuliza maulizo.

3. Namna gani unaweza kujitayarisha ili kuhubiria wengine kwenye masomo?

3 Ujitayarishe: Ikiwa unajitayarisha, utakuwa na uhakika zaidi. (1 Pet. 3:15) Kwa hiyo, jaribu kufikiria mbele ya wakati maulizo ambayo wanafunzi wenzako wanaweza kukuuliza, na ufikiri kuhusu jinsi unavyoweza kuyajibu. (Met. 15:28) Ikiwezekana, chunga Biblia yako kwenye masomo na vitabu vichache, kama vile kitabu Kutoa Sababu, Vijana Huuliza, buku la 1 na la 2, na vichapo vinavyozungumuzia uumbaji, ili uvitumie unapovihitaji. Omba wazazi wako wapange pia kufanya vipindi vya mazoezi katika ibada yenu ya familia.

4. Kwa nini unapaswa kuendelea kuhubiria wengine kwenye masomo?

4 Usiwazie Wengine Vibaya: Usifikiri kwamba wanafunzi wenzako watakuchekea kila wakati utakapotaka kuwaelezea kweli. Huenda wanafunzi fulani watakuheshimu kwa sababu ya ujasiri wako na wanaweza hata kukusikiliza. Lakini usivunjike moyo ikiwa hakuna mutu anayekusikiliza. Yehova atafurahi kwa kuwa ulijaribu. (Ebr. 13:15, 16) Endelea kumwomba akusaidie ‘uendelee kusema kwa ujasiri wote.’ (Mdo. 4:29; 2 Tim. 1:7, 8) Wazia furaha utakayokuwa nayo utakapopata mutu atakayekusikiliza. Mwishowe mutu huyo anaweza kuwa mutumishi mwenzako wa Yehova!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine