Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 12/01 uku. 1
  • Shule ya Huduma ya Kitheokrasi Mnamo 2002

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Shule ya Huduma ya Kitheokrasi Mnamo 2002
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Shule Inayotuandalia Vifaa kwa Ajili ya Utendaji wa Maana Zaidi Maishani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Katika 1998
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Shule ya huduma ya kitheokrasi mnano 2000
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2001
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 12/01 uku. 1

Shule ya Huduma ya Kitheokrasi Mnamo 2002

1 Watu wengi huona uwezo wa kusema kuwa jambo la kawaida tu. Lakini, usemi ni zawadi kutoka kwa Yehova. Unatuwezesha kupashana habari na wengine na kusema mawazo yetu na hisia zetu. Jambo la maana zaidi ni kwamba kupitia huo tunaweza kumsifu Mungu wetu.​​—Zab. 22:22; 1 Kor. 1:​4-7.

2 Wanaume, wanawake, na watoto wanazoezwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ili kutangaza jina la Yehova. (Zab. 148:​12, 13) Programu ya shule mnamo 2002 inazungumzia habari nyingi za Biblia ambazo tunaweza kufaidika nazo kibinafsi na kuzitumia katika huduma. Kwa kutayarisha shule na kuishiriki, tunaweza kuongeza ujuzi wetu na ufundi wetu mbalimbali tukiwa walimu wa Neno la Mungu.​​—Zab. 45:1.

3 Soma Biblia Kila Siku: Ikiwa kwa kawaida tuna Biblia karibu nasi, tunaweza kutumia kwa faida wakati wowote tusipokuwa na kazi ili kuisoma. Wengi wetu wana dakika chache za ziada katika mchana ambazo tunaweza kutumia katika njia hiyo. Ni jambo lenye mafaa kama nini kusoma hata ukurasa mmoja kila siku, kiasi ambacho kinatosha ili kwenda sambamba na programu ya usomaji wa Biblia, kama inavyoonyeshwa katika programu ya shule!​​—Zab. 1:​1-3.

4 Uwezo wa kusoma Biblia vizuri unaweza kutusaidia kugusa moyo wa wasikilizaji wetu na kuwachochea wamsifu Yehova. Akina ndugu wanaotoa Mgawo Na. 2 katika shule wanapaswa kujizoeza, kujizoeza, kujizoeza kusoma mgawo wao kwa sauti kubwa. Mwangalizi wa shule atatoa pongezi na mapendekezo ili kuboresha usomaji.

5 Tumia Kitabu Kutoa Sababu: Migawo Na. 3 na Na. 4 inategemea kitabu Kutoa Sababu. Labda wengi wetu wanapaswa kujitahidi zaidi kutumia kitabu hicho chenye mafaa katika huduma ya shambani. Akina dada wanapaswa kuchagua vikao vinavyofaa kulingana na eneo. Mwangalizi wa shule anapaswa kuangalia kipekee jinsi wanavyofundisha na wanavyofanya matumizi ya Maandiko.

6 Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na itusaidie sote tuendelee kutumia zawadi ya usemi tuliyopewa na Mungu ili kutangaza habari njema na kumsifu Mungu wetu mkuu, Yehova!​​—Zab. 34:1; Efe. 6:​19.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine