Shule Inayotuandalia Vifaa kwa Ajili ya Utendaji wa Maana Zaidi Maishani
1 Watu wanaenda shuleni kupokea mafunzo yatakayowasaidia wafikiye miradi yao maishani. Hata hivyo, ni mradi gani unaoweza kuwa wa lazima zaidi kuliko kumsifu Yehova Mpaji mkuu wa uhai na kusaidia wengine katika kujifunza makusudi yake na njia zake? Hata mmoja. Kusudi la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ni kututayarisha kufundisha imani yetu kwa wengine. Kwa hiyo, tunapohudhuria shule kila juma, tunajitwalia ufundi mbalimbali unaotundalia vifaa kwa ajili ya utendaji wa maana zaidi maishani.
2 “Programu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2003” iliandaliwa katika toleo la mwezi uliopita katika Huduma Yetu ya Ufalme. Programu inatia ndani mambo madogo-madogo kuhusu namna shule itakavyoongozwa. Unaweza kuona kuwa ni jambo lenye kufaa kulinda programu katika nakala yako ya Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, ambayo unapaswa kuleta kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kila juma. Chunguza baadhi ya mambo makuu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2003.
3 Sifa ya Usemi: Kuanza Januari, kila mkutano wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi utaanza kwa hotuba ya dakika tano kuhusiana na sifa ya usemi au pande moja ya usomaji, funzo, au kufundisha. Mwangalizi wa shule atatoa hotuba hizi za mwanzo, au anaweza kumpa mgawo mzee mwengine mwenye kustahili ili atoe hotuba hiyo. Msemaji anaweza kuzungumzia fasili na umaana wa sifa ya usemi. Basi, anapaswa kutoa maelezo ya habari kwa kuzungumzia mifano ya Kimaandiko na kuonyesha jinsi ya kutumia sifa ya usemi, akikazia uangalifu wa pekee juu ya jinsi kufanya hivyo kunavyoweza kuboresha huduma yetu ya shambani.
4 Mgawo Na. 1: Ndugu wanaopewa mgawo wa hotuba ya maagizo wanashauriwa tena ‘kukazia uangalifu juu ya matumizi yenye kufaa ya habari inayozungumziwa.’ Hilo linamaanisha kuonyesha kutaniko jinsi ya kufanya matumizi ya habari. Ukipata mgawo huu, chunguza ukurasa wa 48-9 wa kitabu Shule ya Huduma kwa ajili ya madokezo kuhusu jinsi ya kutayarisha, na ya kujifunza mitajo inayoonyeshwa katika fahirisi ya kitabu chini ya kichwa ‘Matumizi yafaayo’
5 Programu ya Usomaji wa Biblia: Ikiwa, wakati uliopita haukuweza kushikamana na usomaji wa Biblia wa kila juma, kwa nini usiazimie kushikamana na programu mwaka huu? Wanaofanya hivyo watamaliza Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo mwisho wa mwaka. Faida za kuanza programu ya usomaji wa Biblia na Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ni zenye kuchunguzwa katika kitabu Shule ya Huduma kwenye ukurasa wa 10, fungu la 4.
6 Mambo Makuu Kutoka Katika Usomaji wa Biblia: Sehemu hii imeongezwa urefu kufikia dakika kumi ili kwamba wahudhuriaji wawe na uwezekano wa kutoa maelezo kuhusu usomaji wa juma. Wale wanaopewa mgawo wanapaswa kushikamana na wakati uliotolewa. Itatolewa kila juma, kutia ndani na juma la kujikumbusha kwa maneno tu. Unaposoma sura zilizotolewa kuwa mgawo, tafuta nukta ambazo zitakutolea faida katika funzo lako la familia, katika huduma yako, au katika namna yako ya kuishi. Ni sifa gani za Yehova zilizoonyeshwa aliposhughulika na watu na mataifa? Ni jambo gani ulilojifunza linaloimarisha imani yako na linaloongeza uthamini wako kuelekea Yehova? Ujisikie huru kutoa maelezo juu ya kila nukta katika sura zilizotolewa kuwa mgawo, hata kutoka katika mistari itakayosomwa wakati wa Mgawo Na. 2, kwani ndugu anayefanya usomi hatatowa maelezo kuhusu mistari.
7 Mgawo Na. 2: Mgawo wa mwanafunzi wa kwanza kila juma utakuwa ni mazoezi katika usomi wa peupe. Usomaji wote utachukuliwa kutoka usomaji wa Biblia wa juma isipokuwa tu usomaji wa mwisho wa kila mwezi. Usomaji wa mwisho wa mwezi utachukuliwa kutoka Mnara wa Mlinzi. Mwanafunzi anapaswa kusoma habari iliyotolewa kuwa mgawo bila kutoa utangulizi au umalizio. Katika njia hii, anaweza kukazia uangalifu wake wa kwanza kwenye ufundi wa usomaji wake.—1 Tim. 4:13.
8 Migawo Na. 3 na Na. 4: Baadhi ya migawo hiyo ina chanzo cha habari zaidi kutoka katika kitabu Kutoa Sababu kuliko vingine; migawo fulani ina kichwa cha habari tu. Wale wanaotolewa migawo isiyo kuwa na habari nyingi au yenye kichwa cha habari tu watakuwa na nafasi ya kuzungumzia habari zao ambazo zitatokana na kufanya utafiti katika vichapo vyetu vya Kikristo. Jambo hilo linaweza kufanya iwe rahisi kwa akina dada kupatanisha maelezo yao na wahudhuriaji.
9 Vikao: Kama inavyoonyeshwa kwenye ukurasa wa 45 wa kitabu Shule ya Huduma, mwangalizi wa shule anaweza kugawia mwanafunzi kikao. Ikiwa hafanye hivyo, basi akina dada wanaweza kuchagua kikao kutoka orodha kwenye ukurasa 82. Ikiwa dada anatoa habari moja kila miezi miwili, vikao hivyo 30 vitaandalia vikao vya kutosha mbalimbali vya kuweza kudumu miaka mitano. Dada wanaochagua Na. 30, yenye kichwa, ‘Kikao kingine kinachofaa kwa eneo lenu,’ anapaswa kuandika kikao mwisho au nyuma ya kikaratasi cha mgawo (S-89). Mwangalizi wa shule ataandika tarehe ya hotuba ya mwanafunzi kwenye ukurasa wa 82 wa kitabu chake, pembeni ya kikao ambacho alitumia. Anaweza kufanya hivi wakati uleule anapotia alama kwenye kikaratasi cha shauri cha mwanafunzi.
10 Kikaratasi cha Shauri: Kikaratasi chako cha shauri kimebanishwa katika kitabu chako. Kinapatikana kwenye ukurasa wa 79-81. Kwa hiyo, utahitaji kumtolea mwangalizi wa shule kitabu chako baada ya kila hotuba unayotoa. Mwangalizi wa shule atahitaji kulinda rekodi ya nukta za shauri ambayo juu yayo wanafunzi wanatumikia.
11 Kujikumbusha kwa Maneno Tu: Kujikumbusha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kutaongozwa kwa maneno tu. Kutakuwa kukifanywa mara moja kila miezi miwili na kutadumu dakika 30. Maswali yatakayochunguzwa wakati wa kujikumbusha yataendelea kutokea katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ikiwa juma linalopangwa kwa ajili ya kujikumbusha kwa maneno tu linapatana na juma la kusanyiko la mzunguko au ziara ya mwangalizi wa mzunguko, basi hotuba za juma lifuatalo zitatolewa juma moja mapema na kujikumbusha kwa maneno tu kunapaswa kupangiwa juma lifuatalo.
12 Madarasa ya Ziada: Katika makutaniko ambamo hesabu ya wanafunzi ni zaidi ya 50, wazee wanaweza kufikiria matumizi ya madarasa ya ziada. ‘Mpango huo unapaswa kutumikishwa kuhusu habari zote za wanafunzi au kuhusu migawo miwili ya mwisho tu.’ (Shule ya Huduma, uku. 285) Dokezo hilo la mwisho linafanywa kwa kufikiria kutaniko ambamo mna akina dada wengi lakini mna akina ndugu wachache tu wanaohusika na migawo ya usomaji. Wazee wangepaswa kuchagua ndugu wenye kustahili ili kuongoza madarasa hayo.
13 Mshauri Msaidizi: Kama inavyoonyeshwa katika programu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, mshauri msaidizi anapaswa kuchaguliwa na baraza la wazee ili kutoa shauri kwa siri kwa wazee na watumishi wa huduma wanaotoa mambo makuu ya Biblia na wanaotoa hotuba za maagizo. Ndugu anayepewa mgawo huo anapaswa kuwa na uzoefu, mtu ambaye shauri lake litaheshimiwa na wazee wengine. Shauri lake linapaswa kuwa lenye kujenga, akipongeza usemi mzuri na ufundi wa kufundisha na kupendekeza nukta moja au mbili za kuboresha. Hakuna uhitaji wa kutoa shauri baada ya kila habari inayotolewa na ndugu anayesema kwa ukawaida. Hata hivyo, ndugu aliyepewa mgawo wa kutoa mashauri haya anapaswa kuwa mwenye kutafakari na kuelewa kwamba hata ndugu ambao sasa wanatoa hotuba za watu wote wanaweza kusaidiwa ili kufanya maendeleo zaidi.—1 Tim. 4:15.
14 Mambo ya Kutolea Uangalifu: Jambo gani linaweza kumsaidia mshauri katika kuchanganua utoaji? Kisanduku cha tatu kati ya zaidi ya sura 53 zilizo na namba za kitabu Shule ya Huduma kina muhtasari wa mambo ya kutolea uangalifu. Mwangalizi wa utumishi anapaswa pia kutoa uangalifu kuhusu vikumbusha vingine au madokezo katika kitabu ambayo yatamsaidia kukadiria kwa uharaka maelezo ya habari yenye mapatano na jinsi ilivyotolewa kwa matokeo. Kwa mfano, angalia mfululizo wa maulizo kwenye sehemu ya juu ya ukurasa wa 55 na mawazo katika fungu la mwisho kwenye ukurasa wa 163.
15 Jaza Nafasi Iliyowazi: Zaidi ya pambizo zake kubwa, kitabu Shule ya Huduma kina nafasi nyingi zilizowazi zilizokusudiwa kwa ajili yako ili kuongeza maandishi wakati wa funzo la kibinafsi na unaposhiriki Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. (Ona kurasa 77, 92, 165, 243, 246, na 250.) Uhakikishe kwamba unaleta kitabu chako kila juma. Fuata ndani wakati wa hotuba ya utangulizi. Acha kitabu chako kikiwa chenye kufunguliwa kwa ajili ya sehemu ya shule inayobaki. Andika madokezo yanayotolewa na mwangalizi wa shule. Uwe mwangalifu kuhusu namna ya kufundisha, maswali, mifano, semi za kimfano, vielezi, misaada ya kuonwa, na mambo yenye kupingana yanayotumiwa na wasemaji. Kwa kuandika vizuri, utakuwa na uwezo wa kukumbuka na kutumia nukta nyingi za maana zilizokusanywa kutokana na shule.
16 Yesu Kristo alijua kwamba kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu ni pendeleo kubwa sana ambalo linaweza kutolewa kwa yeyote. Ilikuwa utume wake mkuu. (Mk. 1:38) Alisema: “Ni lazima nitangaze habari njema ya ufalme wa Mungu, kwa sababu kwa ajili ya hili nilitumwa.” (Luka 4:43) Kama wale waliokubali aliko la kumfuata yeye, sisi pia tuko wenye kujishughulisha sana na kutangaza habari njema, na siku zote tunajitahidi kuboresha sifa ya “zabihu ya sifa” yetu. (Ebr. 13:15) Ili kutimiza mradi huo, na tuazimie kushiriki kikawaida kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, shule ambayo itasaidia kututayarisha kwa ajili ya utendaji wa maana zaidi maishani.