Waangalizi Wanaoongoza—Mwangalizi Wa Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi
1 Mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ni mwanamume mzee kiroho anayetumika nguvu katika kusema na kufundisha na anayestahili tumheshimu na kushirikiana naye. (1 Tim. 5:17) Madaraka yake ni gani?
2 Ni yeye anayesimamia maktaba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kwenye Jumba la Ufalme. Yeye anapendezwa sana kutia moyo wote wanaostahili kujiandikisha kwenye shule. Anaangalia kwamba maandishi sahihi yafanywe ili migawo itolewe kwa utaratibu angalau majuma matatu kabla ya kila kipindi cha shule. Anahitaji kujua kutaniko vema, akijua kila mwanafunzi na uwezo wake mbalimbali. Ingawa anaweza kusaidiwa na ndugu mwingine katika kutayarisha programu ya shule, ugawaji wa vipindi wataka usimamizi wa mwangalizi binafsi.
3 Ili afundishe kwa matokeo kwenye shule, mwangalizi anapaswa kujitayarisha kwa bidii kila juma, akijifunza kwa makini habari zilizopangwa kuzungumziwa. Jambo hilo hufanya iwezekane kwake kufanya kutaniko lipendezwe na taratibu ya mafundisho, kuamua ikiwa habari iliyopangwa ilizungumziwa kwa usahihi, na kukazia mambo ya maana yatakayotiwa ndani ya kujikumbusha kwa kuandika.
4 Baada ya kila hotuba ya mwanafunzi, mwangalizi atampongeza na kufasiria kwa nini sifa fulani ya usemi ilikuwa nzuri au kwa nini inahitaji kufanyiwa maendeleo. Wakati mtu fulani anapohitaji msaada wa ziada wa binafsi ili kutayarisha vipindi vyake vya shule, mwangalizi au mtu mwingine atakayemchagua anaweza kuutoa.
5 Ili tufaidike kikamili na kazi ngumu ya Mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na washauri wengine wowote wa ziada wanaotumika chini ya uongozi wake, tunapaswa kuhudhuria shule kikawaida. Tunapaswa vilevile kutimiza migawo yetu na kutumia mashauri tunayopewa na yale yanayotolewa kwa wanafunzi wengine. Kwa njia hiyo, tutafanya uwezo wetu wa kutoa ujumbe wa Ufalme peupe na kutoka nyumba hadi nyumba uwe bora hatua kwa hatua.—Mdo. 20:20; 1 Tim. 4:13, 15.