Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 12/04 uku. 6
  • Jinsi Tunavyofaidika na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Jinsi Tunavyofaidika na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Shule Inayotuandalia Vifaa kwa Ajili ya Utendaji wa Maana Zaidi Maishani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Waangalizi Wanaoongoza —Mwangalizi Wa Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Yehova Anatupatia Mazoezi ili Tufanye Kazi Hii
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Shule ya Huduma ya Kitheokrasi Mnamo 2002
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 12/04 uku. 6

Jinsi Tunavyofaidika na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

1 Watu wa Yehova wanalo pendeleo la pekee la kufundishwa naye. (Isa. 54:13; Yoh. 6:45) Hata hivyo, kufaidika kwetu na shule hiyo kunategemea sana jitihada tunayofanya. Je, unaweza kutambua matokeo mazuri ambayo Shule ya Huduma ya Kitheokrasi imekuwa nayo juu ya hali yako ya kiroho?

2 Maelezo Yenye Kuthaminiwa: Waangalizi wengi wa shule wameona kwamba kujifunza kikamili sifa za usemi kumekuwa na matokeo bora juu ya utumishi wa makutaniko yao katika huduma ya shambani. Zaidi ya hayo, mwangalizi mmoja wa shule aliona kwamba mpango wa kufanya wasikilizaji washiriki katika mambo makuu ya usomaji wa Biblia, unafanya wengi zaidi waendelee kuwa na programu ya usomaji wa Biblia. Kuhusu Mgawo Na. 2, ndugu wengi wamefanya maelezo mazuri juu ya faida zinazopatikana kutokana na kutumia wakati ili kutayarisha habari ya kusoma bila utangulizi na umalizio. Wale wanaogawiwa sehemu hiyo ni wenye kukazia sasa akili juu ya jinsi ya kufanya ufundi wao wa kusoma uwe bora zaidi.—1 Tim. 4:13.  

3 Wote Wanaweza Kufaidika: Kutoa maelezo kwenye mikutano kunaweza kupendeza. (Met. 15:23) Kuwa na maulizo ya kujikumbusha kimbele kunatuwezesha kujitayarisha na kushiriki kwa urahisi katika kujikumbusha. Zaidi ya hayo, kuanzia na toleo la Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 2004, mambo makuu kutoka vitabu vya Biblia yametokea, ambayo yanalingana na usomaji wetu uliopangwa kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Makala hizo zimesaidia wengi kutoa maelezo yenye kujenga wakati wa mambo makuu ya usomaji wa Biblia.

4 Kila mtu aliyejiandikisha katika shule analo pendeleo la pekee la kutayarisha na kutoa migawo. Sote tunaweza kufaidika na maelezo yenye kujenga ya mwangalizi wa shule kutoka jukwaani. Wanafunzi mmoja mmoja wanafaidika zaidi na mashauri anayoweza kuwatolea kwa siri kisha mkutano. Mazoezi yanayozungumzia sifa za usemi mwishoni mwa kila sura ya kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi yanatoa msaada wa ziada.

5 Mawazo yanayofaa na ya Kimaandiko yanapotolewa wakati wa shule na baadaye, uyaandike katika kitabu chako cha Shule ya Huduma. Tafakari juu ya mambo ambayo umejifunza, na ufikiri jinsi sehemu hii ya elimu ya kimungu inavyokusaidia kufanya hali yako ya kiroho iwe bora zaidi.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine