Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/11 uku. 2
  • Yehova Anatupatia Mazoezi ili Tufanye Kazi Hii

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yehova Anatupatia Mazoezi ili Tufanye Kazi Hii
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Shule Inayotuandalia Vifaa kwa Ajili ya Utendaji wa Maana Zaidi Maishani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Wahubiri wa Ufalme Wanapewa Mazoezi
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Jinsi Tunavyofaidika na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Tufaidike Na Programu Ya Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 1999
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2011
km 9/11 uku. 2

Yehova Anatupatia Mazoezi ili Tufanye Kazi Hii

1. Yehova anapowapa watu kazi fulani, ni jambo gani analofanya pia?

1 Yehova anapowapatia wanadamu kazi fulani, anawapa pia musaada wanaohitaji ili kutimiza kazi hiyo. Kwa mufano, Yehova alipomwambia Noa ajenge safina, alimwambia pia jinsi ya kuifanya. Noa alikuwa hajawahi kufanya kazi hiyo mbele. (Mwa. 6:14-16) Musa, muchungaji wa kondoo aliyekuwa mutu mupole, alipopewa kazi ya kwenda kukutana na wanaume wazee wa Israeli na Farao, Yehova alimuhakikishia hivi: “Nitakuwa pamoja na kinywa chako nami nitakufundisha unayopaswa kusema.” (Kut. 4:12) Kuhusu kazi yetu ya kuhubiri habari njema, Yehova ametutolea pia maagizo kuhusu jinsi ya kuitimiza. Anatupatia mazoezi ili tufanye kazi hii kupitia Shule ya Huduma ya Kiteokrasi na Mukutano wa Utumishi. Namna gani tunaweza kufaidika na mazoezi ambayo anatutolea?

2. Namna gani tunaweza kufaidika na Shule ya Huduma ya Kiteokrasi?

2 Shule ya Huduma ya Kiteokrasi: Soma na kujifunza habari zilizopangwa kwenye programu mbele ya kuhuzuria kila mukutano. Kisha unapofuata jinsi wanafunzi wanavyotoa sehemu zao, utaelewa zaidi kile unachopaswa kufanya ili kutengeneza namna yako ya kufundisha. (Met. 27:17) Usisahau kitabu chako Shule ya Huduma unapokwenda kwenye mikutano na ukitumie kama kitabu cha mazoezi. Mwalimu wa shule anapozungumuzia habari fulani katika kitabu hicho ili kumushauri mwanafunzi kisha kila mugawo, tia kistari chini ya mambo makuu unayotaka kutumia, na uyaandike kwenye nafasi za pembeni zilizo wazi. Lakini, kushiriki ndiyo njia nzuri zaidi ya kufaidika na shule hiyo. Je, umekwisha kujiandikisha kwenye Shule ya Huduma ya Kiteokrasi? Unapopewa mugawo, uutayarishe vizuri na utumie mashauri unayopewa. Unapokuwa katika mahubiri, utumie mambo ambayo umejifunza.

3. Ni nini kinachoweza kutusaidia tufaidike na Mukutano wa Utumishi?

3 Mukutano wa Utumishi: Tutakumbuka vizuri mapendekezo tunayotolewa wakati wa mukutano huo kwa kusoma mbele ya wakati habari itakayozungumuziwa na kujitayarisha ili kutoa maelezo. Ikiwa tunatoa maelezo mafupi, hilo litawezesha watu wengi zaidi watoe maelezo. Fuata kwa uangalifu maonyesho yanapofanywa, na utumie mapendekezo yoyote ambayo unaona kwamba yatakusaidia upate matokeo mazuri zaidi katika kazi yako ya kuhubiri. Unapoona kwamba katika Huduma Yetu ya Ufalme kuna habari inayoweza kukusaidia katika kazi ya kuhubiri, chunga vizuri habari hiyo.

4. Kwa nini tunapaswa kutumia vizuri mazoezi tunayopewa na Mungu?

4 Kazi ambayo Noa na Musa walipewa haikuwa rahisi, vivyo hivyo kazi yetu ya kuhubiri habari njema katika dunia yote inayokaliwa si kazi rahisi. (Mt. 24:14) Tunaweza kuitimiza vizuri kwa kumutegemea Yehova, Mufundishaji wetu Mukuu, na kutumia vizuri mazoezi anayotutolea.—Isa. 30:20.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine