Shule ya Huduma ya Kitheokrasi Mnamo 2004
1 Yehova anaandalia watu wa kawaida vifaa ili watimize kazi ya maana ulimwenguni pote. Njia moja ambayo katika hiyo anafanya hivyo ni kupitia mazoezi yanayotolewa kila juma kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Je, unashiriki kikamili kulingana na jinsi hali zako zinavyoruhusu? Mnamo Januari, marekebisho machache yatafanywa ili kusaidia wanafunzi wafaidike kikamili zaidi na mipango hiyo.
2 Kupeana Zamu Kati ya Washauri Wasaidizi: Akina ndugu wanaotoa hotuba za maagizo na mambo makuu ya Biblia wamethamini maelezo yaliyotolewa na mshauri msaidizi. Mahali ambapo kuna wazee wa kutosha wenye sifa, mgawo wa mshauri msaidizi unaweza kutolewa kwa mzee tofauti kila mwaka. Katika njia hiyo, mzigo wa kazi utagawanywa; lakini jambo la maana zaidi ni kwamba wazee na watumishi wa huduma wenye sifa watafaidika na jumla ya ujuzi wa wasemaji na walimu mbalimbali wenye uwezo.
3 Kupanga Kujikumbusha kwa Maneno Tu: Ikiwa kutaniko lenu lina mkusanyiko wa mzunguko kwenye juma la kujikumbusha kwa maneno tu, wakati huo kujikumbusha (na sehemu nyinginezo za programu ya juma) kunapaswa kufanywa juma linalofuata mkusanyiko huku programu ya juma hilo ikitumiwa kwenye mkusanyiko. Lakini, si jambo la lazima kufanya programu nzima ya juma ichukue nafasi ya programu nyingine wakati kujikumbusha kwa maneno tu kunapotokea wakati mmoja na ziara ya mwangalizi wa mzunguko. Badala yake, wimbo, hotuba kuhusu sifa ya usemi, na mambo makuu ya Biblia yanapaswa kutolewa kama inavyopangwa. Hotuba ya maagizo (inayotolewa baada ya hotuba kuhusu sifa ya usemi) inapaswa kuchukuliwa kutoka kwenye programu ya juma linalofuata. Mambo makuu ya Biblia yatafuatwa na Mkutano wa Utumishi wa nusu-saa; mkutano huo unaweza kurekebishwa ili uwe na sehemu tatu za dakika 10 kila moja au sehemu mbili za dakika 15 kila moja. (Matangazo ya kufungua yanapaswa kuondolewa.) Mkutano wa Utumishi utafuatwa na wimbo na programu ya nusu-saa itakayotolewa na mwangalizi wa mzunguko. Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya juma litakalofuata itaanza na hotuba kuhusu sifa ya usemi na mambo makuu ya Biblia kama inavyopangwa, sehemu hizo zikifuatwa na kujikumbusha kwa maneno tu.
4 Faidika na kila nafasi ili kukomaa kiroho. Unapofaidika na elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, unatia kutaniko lako moyo, unatimiza fungu katika utimizo wa unabii wa Biblia, na unamletea sifa yule aliye Chanzo cha ujumbe mzuri ajabu tunaopaswa kutangaza.—Isa. 32:3, 4; Ufu. 9:19.