Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 10/08 uku. 1
  • Programu Mpya ya Mikutano ya Kutaniko

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Programu Mpya ya Mikutano ya Kutaniko
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mukutano kwa Ajili ya Mahubiri Wenye Kutimiza Kusudi Lake
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Kisanduku cha Maulizo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Mikutano Yenye Inatuchocheaka Katika “Upendo na Matendo ya Muzuri”
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Maagizo kwa Ajili ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo
    Maagizo kwa Ajili ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 10/08 uku. 1

Programu Mpya ya Mikutano ya Kutaniko

1 Juma la tarehe 21-27 mwezi wa 4, 2008, ndugu na dada wa ulimwenguni pote walisikia tangazo lenye kusisimua. Tangazo hilo lilisema hivi: “Kuanzia tarehe 1 mwezi wa 1, 2009, Funzo la Kitabu la Kutaniko litafanywa wakati uleule pamoja na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na Mkutano wa Utumishi. Funzo la Kitabu la Kutaniko litabadilishwa na kuitwa sasa Funzo la Biblia la Kutaniko.”

2 Programu ya Mikutano Hiyo ya Kila Juma: Mikutano hiyo itachukua saa 1 dakika 45, kutia ndani nyimbo na sala. Mikutano itaanza kwa wimbo na sala (Dak. 5). Kisha wimbo na sala, Funzo la Biblia la Kutaniko (Dak. 25) litafuata. Bila kukatizwa, Shule ya Huduma ya Kitheokrasi (Dak. 30) itafuata. Kisha, wimbo (Dak. 5) utaimbwa ili kuanza Mkutano wa Utumishi (Dak. 35). Mikutano itamalizwa kwa wimbo na sala (Dak. 5). Ili kuwasaidia kutayarisha mikutano hiyo, programu ya Funzo la Biblia la Kutaniko, Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na Mkutano wa Utumishi, itatolewa kila mwezi katika Huduma Yetu ya Ufalme.

3 Funzo la Biblia la Kutaniko: Mkutano huo utaongozwa kama Funzo la Mnara wa Mlinzi. Haitakuwa lazima kujikumbusha habari ya juma lililopita mbele ya kuanza mkutano huo. Lakini, mkutano utaanza tu kwa maneno machache sana ya utangulizi. Hilo litawezesha wahuzuriaji wote wapate wakati wa kutosha ili kutoa maelezo mafupi. Mwangalizi msimamizi atotolea wazee mgawo ili kuongoza mkutano huu, mzee mmoja baada ya mwingine kila juma.

4 Mkutano wa Utumishi: Mkutano wa Utumishi hautabadilika lakini sehemu zake zitafupishwa. Kwa kawaida, matangazo yatachukua dakika 5. Dakika hizo zinapaswa kutosha ili kutoa matangazo ya lazima na kusoma barua fulani zilizotumwa na biro ya tawi. Matangazo mengine kama vile mipango kwa ajili ya utumishi wa shambani, programu kuhusu usafishaji, ripoti za feza na barua zinazotumwa kwa kawaida na biro ya tawi, hayahitaji kusomewa kutaniko, lakini yatabandikwa kwenye ubao wa matangazo ili ndugu wayasome wenyewe. Wale walio na vipindi watajitayarisha vizuri na kuheshimu wakati na pia kufuata maagizo yaliyotolewa.

5 Ziara ya Mwangalizi wa Mzunguko: Programu ya juma ya mwangalizi wa mzunguko haitabadilika. Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na Mkutano wa Utumishi vitafanywa Siku ya Pili, na kisha wimbo utaimbwa. Kisha hapo mwangalizi wa mzunguko atatoa hotuba ya dakika 30. Kama ilivyo kawaida mwangalizi wa mzunguko anapotembelea kutaniko, Funzo la Biblia la Kutaniko litafanywa magaribi ya siku nyingine, likifuatwa na wimbo na hotuba ya utumishi ya mwangalizi wa mzunguko. Mikutano itamalizwa kwa wimbo na sala.

6 Mikutano kwa Ajili ya Utumishi wa Shambani: Baraza la wazee litawatolea waangalizi wa vikundi mgawo wa kushugulikia vikundi kwa ajili ya utumishi wa shambani na pia kufanya ziara za uchungaji kwa watu wanaofanyiza vikundi hivyo. Ikiwa mtumishi wa huduma anahitajiwa ili kutimiza daraka hilo, ataitwa “mtumishi wa kikundi.”

7 Kupitia habari hii, tunaona wazi kwamba tutakuwa na nafasi ya kupata chakula cha kiroho cha magaribi chenye kuelimisha na kujenga. Hilo litatuwezesha kuwa wahubiri na walimu wenye matokeo, wenye kuzoezwa kwa ajili ya utumishi wenye kuzaa matunda zaidi.—Efe. 4:13, 14; 2 Tim. 3:17.

8 Kujitayarisha mbele ya wakati kwa ajili ya mikutano hiyo kutatusaidia kufuata kwa uangalifu mambo makuu yanayokaziwa wakati wa kila mkutano. Sisi wote tutakuwa na nafasi ya kutoa maelezo na hivyo kutoa msaada wetu katika kutiana moyo. (Rom. 1:11, 12; Ebr. 10:24) Kusudi letu linapaswa kuwa ‘kufanya maendeleo yetu yawe wazi’ kwa ‘kulitumia sawasawa neno la kweli.’—1 Tim. 4:15; 2 Tim. 2:15.

9 Tunafurahia sana badiliko hili la maana kuhusu mikutano yetu ya kutaniko. Sisi wote na tuendelee kufuata mwongozo wa “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” na tubaki karibu na Mchungaji wetu Mkuu anapotutayarisha kwa ajili ya “dhiki” kuu inayokaribia.—Mt. 24:21, 45; Ebr. 13:20, 21; Ufu. 7:14.

[Maulizo ya Funzo]

1, 2. Ni mabadiliko gani yatakayofanywa kuhusu mikutano kuanzia mwezi wa 1, 2009?

3. Funzo la Biblia la Kutaniko litaongozwa namna gani?

4. Ni mabadiliko gani yatakayofanyika kuhusu Mkutano wa Utumishi?

5. Katika juma ambamo mwangalizi wa mzunguko anatembelea kutaniko, programu ya mikutano itakuwa namna gani?

6. Mwangalizi wa kikundi ana daraka gani?

7. Tunaweza kutazamia nini kutokana na programu yetu mpya ya mikutano ya kutaniko?

8. Namna gani kujitayarisha mbele ya wakati kutatufaidi sisi na wengine pia?

9. Tunakusudia kufanya nini, na kwa nini?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine