Kisanduku cha Maulizo
◼ Ni nani anayepaswa kualika watu waimbe wimbo wa kufungua Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, Mkutano wa Utumishi, Mkutano wa Watu Wote, na Funzo la Mnara wa Mlinzi, na namna gani jambo hilo linapaswa kufanywa?
Nyimbo za kufungua mkutano wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi wa kila juma zinaonyeshwa katika Programu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ambayo ni nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi wa 10. Nyimbo za kufungua na kumalizia Mkutano wa Utumishi wa kila juma, zinaonyeshwa kwenye ukurasa wa 2 wa Huduma Yetu ya Ufalme. Vilevile, nyimbo kwa ajili ya kila Funzo la Mnara wa Mlinzi la kila juma zinapatikana kwenye ukurasa wa 2 wa kila Mnara wa Mlinzi. Nyimbo zinazopangwa kwa ajili ya mkutano fulani ni sehemu ya mkutano huo, na kwa sababu hiyo ni ndugu mwenye kuongoza mkutano huo ndiye atakayeomba watu waimbe wala si mwenyekiti wa mkutano uliotangulia.
Kwa mfano, mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi atakaribisha wasikilizaji, atawaomba kuimba wimbo wa kufungua, ataongoza shule, na kisha shule ataalika kwenye jukwaa msemaji wa kwanza wa Mkutano wa Utumishi. Ndugu huyo anayefanya sehemu ya kwanza ya Mkutano wa Utumishi ndiye anayepaswa kuomba ndugu wasimame ili kuimba wimbo unaofungua Mkutano wa Utumishi.
Vivyohivyo, Mkutano wa Watu Wote utafunguliwa na mwenyekiti. Atakaribisha kwa uchangamfu watu wote wenye kuhuzuria na kuwaomba wasimame ili waimbe pamoja wimbo wa kufungua uliochaguliwa na msemaji atakayetoa hotuba. Mwenyekiti (au ndugu mwingine mwenye kustahili aliyechaguliwa mbele ya wakati) atafungua mkutano kwa sala. Atamwalika msemaji na kutaja kichwa cha hotuba yake. Hotuba inapomalizika, mwenyekiti hatarudilia kwa kifupi mambo ambayo msemaji alisema lakini atatoa tu maelezo mafupi ya shukrani kuhusu hotuba ya msemaji. Atatangaza kichwa cha hotuba ya juma lifuatalo na kisha ataalika wasikilizaji wabaki tena ili kufuata Funzo la Mnara wa Mlinzi. Si lazima mwenyekiti awaulize wasikilizaji ikiwa wangependa kutuma salamu zenye upendo wa kindugu kwa kutaniko ambako msemaji mgeni alitoka. Kisha, mwenyekiti atakaribisha kwenye jukwaa, ndugu atakayeongoza Funzo la Mnara wa Mlinzi.
Kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi atawaomba ndugu wasimame ili kuimba wimbo wa kwanza unaolingana na Funzo. Ataongoza funzo kufuatana na maagizo ya namna ya kuongoza funzo na kisha atajulisha wimbo wa kumalizia. Kwa kawaida, kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi ataalika ndugu aliyetoa hotuba ili atoe sala ya kumalizia.
Kufuata miongozo hii ya kawaida kutatusaidia kuwa hakika kwamba mikutano yetu inaongozwa kwa njia ya umoja.