Tupendezwe Na Wenzi Wa Ndoa Wasio Mashahidi
1 Ni furaha kama nini kuona wenzi wa ndoa wakiungana katika ibada ya kweli! Hata hivyo, katika familia nyingi, mwenzi mmoja ndiye huwa amekubali njia ya ukweli. Tunaweza kufanya namna gani ili kupendezwa na wenzi wa ndoa wasio Mashahidi na kuwatia moyo wamtumikie Yehova pamoja nasi?—1 Tim. 2:1-4.
2 Tuwaelewe: Ni kweli kwamba wenzi fulani wa ndoa wasio Mashahidi ni wapinzani. Hata hivyo, mara nyingi, ni ubaridi au kutoelewana ndio huwa sababu. Mtu fulani anaweza kujihisi kuwa hawamjali au kuona wivu kuelekea masilayi (faida) mapya ya kiroho ya mwenzi wake wa ndoa, “Nikiwa peke yangu nyumbani, nilihisi nimeachwa pekee,” alikumbuka mume mmoja. w90 15:8 p. 21, à vérifier “Nilihisi kama kwamba mke wangu na watoto wangu walikuwa wakiniacha,” asema mwingine. Wanaume wanaweza kuwa hakika kwamba wamepoteza familia zao kwa sababu ya dini. (Ona Mnara wa Mlinzi, Agosti 15, 1990, kurasa 20-3.) Ni kwa sababu hiyo ni jambo nzuri, kwa kadiri iwezekanavyo, kuchochea mume kujiunga kwenye mazungumzo tangu tu mke wake anapoanza kujifunza Biblia.
3 Tushirikiane: Mume mmoja na mke wake, wote wawili Mashahidi, walisaidia wenzi wa ndoa kuja kwenye ukweli kwa kushirikiana kwa namna yenye matokeo. Mara dada alipoanza funzo pamoja na mke, ndugu alikuwa akimtembelea mume wake. Aliweza mara nyingi kuanza kujifunza na mume huyo.
4 Tuwe Wenye Urafiki na Wema: Katika kutaniko, familia zinaweza kutimiza sehemu yazo kwa kupendezwa na zile ambazo hazijaungana katika ibada ya kweli. Kupitia ziara chache za kirafiki, mwenzi wa ndoa asiye Shahidi ataona kwamba Mashahidi wa Yehova ni wenye shauku, kwamba wao ni Wakristo wenye makini wanaoweka moyoni hali njema ya wengine.
5 Mara kwa mara, wazee wataweza kuchunguza jitihada zilizofanywa ili kushughulikia wenzi wa ndoa wasio Mashahidi na kile kinachoweza kuboreshwa tukitumaini kuwavuta kwa Yehova.—1 Pt. 3:1.