Mlango Mkubwa Kuelekea Utendaji Umefunguliwa
1 Paulo, mhubiri mwenye bidii wa habari njema, alitafuta maeneo ambamo uhitaji ulikuwa mwingi. Mji wa Efeso ulikuwa mojawapo. Paulo alipata matokeo bora humo, hivi kwamba aliandikia Wakristo wenzake: “Nimefunguliwa mlango mkubwa uongozao kwenye utendaji.” (1 Kor. 16:9, TUM) Alifuatia utumishi wake katika eneo hilo na, kupitia yeye, Waefeso wengi wakawa waamini.—Mdo. 19:1-20, 26.
2 Leo, mlango mkubwa uongozao kwenye utendaji umefunguliwa. Tunaalikwa kutegemeza makutaniko ambayo hayafikii kutumika kikamili na kila mwaka maeneo yayo yote. Kwa jitihada zetu, tunaweza hivyo kutosheleza uhitaji ulioko katika maeneo fulani fulani.—Ona 2 Wakorintho 8:13-15.
3 Je! Tunaweza Kutumikia Mahali Ambapo Uhitaji wa Wahubiri ni Mwingi? Je! tumefikiria katika sala uwezekano wa kutumikia mahali pengine? Kutaniko lililo katika mji wetu linahitaji labda msaada. Tumzungumzie mwangalizi wa mzunguko hilo naye atatutolea madokezo. Yawezekena pia kwamba eneo la kutaniko letu lina idadi kubwa ya watu wasiosikia vizuri au watu wenye kuzungumza lugha ya kigeni ambao hawajapata kusaidiwa. Na ingekuwaje tungefanya jitihada ya kujifunza lugha yao ili kutosheleza uhitaji huo? Zaidi ya hayo, kuna labda kikundi au kutaniko la lugha ya kigeni karibu na mahali petu, ambalo ‘linaomba Bwana-mkubwa ili kupata wafanya kazi zaidi wa Ufalme.’ (Mt. 9:37, 38, TUM) Ikiwa ndivyo ilivyo, je! tunaweza kutoa msaada wetu?
4 Miaka hii ya nyuma, maelfu ya familia za Kikristo zimehamia katika nchi nyingine ili kushiriki kwa kadiri kubwa zaidi kwenye mavuno. Wenzi wawili wa ndoa waliofanya hivyo walisema: “Sisi tulitaka kutumikia Yehova mahali tungeweza kufanya mema yaliyo mengi zaidi.” w88 15/8 p. 22, à vérifier Ikiwa tuna tamaa na uwezo wa kuhamia katika sehemu ya mashambani katika nchi yetu au ikiwa tunaweza kutumikia katika nchi ya kigeni, kabla ya yote, tuzungumzie wazee wa kutaniko miradi yetu.
5 Ikiwa unatamani kupata habari kutoka Sosaiti kuhusu mahali ambapo uhitaji ni mwingi, onyesha kwa kifupi nia yako katika barua utakayotoa kwa halmashauri ya utumishi ya kutaniko lenu. Halmashauri ya utumishi itaongeza maelezo machache na kutuma barua yako kwenye Sosaiti. Hata mambo yawe namna gani, na kwa kadiri mlango mkubwa kuelekea utendaji unabaki wazi, tuwe sote wenye shughuli sikuzote katika kazi ya Yehova.—1 Kor. 15:58.