Tugawe Kwa Uwingi Trakti Habari Za Ufalme Na. 35
1 Sisi sote tutakuwa wenye shughuli mnamo miezi ya Novemba na Desemba. Muda wa siku 8 za kwanza za mwezi wa Novemba, tutatolea Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Kisha, kuanzia Siku ya Yenga Novemba 9 mpaka Siku ya Yenga Desemba 14, tutashiriki katika ugawaji wa ulimwenguni pote wa trakti Habari za Ufalme Na. 35. Tutakuwa na pendeleo la kutoa ujumbe wa maana kwa wakaaji wote wa eneo letu. Ujumbe huo unajibu kwenye ulizo “Je! Kuna Wakati Ambao Watu Wataweza Kupendana?” Muda wa kampeni hiyo ya pekee, tutagawa trakti Habari za Ufalme mnamo siku za juma; miisho-juma, tutaongeza kwenye trakti hiyo magazeti ya mwisho mwisho.
2 Nani Anaweza Kushiriki Kwenye Ugawaji? Kama wanavyofanya kikawaida, wazee watachukua uongozi wa utendaji. Kila mmoja anapendezwa kugawa trakti Habari za Ufalme, na hakuna shaka kwamba hesabu kubwa ya wahubiri wataanzisha utumishi wa painia msaidizi muda wa mwezi au miezi miwili itakayodumu kampeni. Wahubiri wengine watapenda kupitisha wakati mwingi zaidi kuliko kawaida katika huduma.
3 Je! tunajifunza pamoja na mtu ambaye alifanya maendeleo mazuri katika uchunguzi wa kitabu Ujuzi na ambaye atatimiza hivi karibuni matakwa yanayoombwa ili kushiriki katika mahubiri? Labda angeweza kuwa mhubiri asiyebatizwa kabla ya mwanzo wa kampeni ili kuweza kuishiriki. Kile kinachohitajiwa ili kutolea trakti Habari za Ufalme, ni utoaji mwepesi tu. Tunaweza kwa mfano kusema: “Ujumbe huu ni wa lazima sana hivi kwamba unatolewa ulimwenguni pote mwezi huu katika lugha 169. Ningependa kukutolea nakala yako binafsi.” Hata watoto wadogo wanaweza kujitoa katika utendaji huo wenye kuchangamsha.
4 Viongozi wa funzo la kitabu watatia moyo washiriki wote wa sehemu zao kushiriki kikamilifu kwenye ugawaji wa trakti Habari za Ufalme Na. 35. Labda kuna pia wahubiri ambao wamekuwa wasiotenda na ambao wangerudilia tena kutenda ikiwa wangepata vitia-moyo ambavyo wanahitaji. Kabla ya mwanzo wa kampeni, wazee wangepaswa hivyo kumtembelea kila mmoja wa wahubiri hao ili kujua jinsi ya kuwasaidia kushindikiza wahubiri wenye ujuzi katika sehemu hiyo ya huduma.
5 Wakati Gani Tunaweza Kukusanyika kwa Ajili ya Mahubiri? Utendaji huu unaomba kwamba mikutano kwa ajili ya mahubiri ipangwe kwa wakati nzuri na wenye kufaa. Kila mara hilo litakapowezekana, mikutano kwa ajili ya mahubiri inapaswa kupangwa kila siku ya juma, mwisho-juma na magharibi. Ingepaswa kufanyika kwa wakati utakaowawezesha wahubiri na mapainia kutumia kikamilifu wakati unaotolewa kwa mahubiri. Mikutano kwa ajili ya mahubiri inaweza pia kupangwa mwishoni mwa kisha mchana-kati kwa ajili ya vijana wenye umri wa kwenda shule, wafanyakazi na wengine. Mwangalizi wa utumishi ataangalia ili kwamba kuwe na maeneo ya kutosha kwa ajili ya mahubiri ya nyumba kwa nyumba na maeneo ya kibiashara, ili kwamba kila mmoja aweze kushiriki kwa bidii katika kazi hiyo. Katika mahali ambako kuna wahubiri wengi, tutaonyesha akili nzuri kwa kuepuka kuwa wengi zaidi kuhubiri katika sehemu fulani ya eneo.
6 Namna Gani Juu ya Wasiokuwako? Nia yetu ni kuwakuta kibinafsi watu wengi iwezekanavyo ili kuwafasiria kwa nini wangepaswa kusoma trakti Habari za Ufalme Na. 35. Hivyo, ikiwa hakuna mtu mahali tunapogonga, tuandike anwani na turudi kwa wakati tofauti muda wa mchana. Ikiwa jitihada yetu ili kukutana na watu hao haikufanikiwa juma la mwisho la kampeni, tunaweza kuacha nakala moja ya trakti Habari za Ufalme mlangoni, kwa kuangalia ili kwamba wapita-njia wasiione. Katika mitaa inayokaliwa na watu, tuwe wepesi kutoa trakti Habari za Ufalme kwa watu wanaopita barabarani. Ikiwa tunahubiri katika eneo la mashambani na kwamba eneo ni kubwa mno hivi kwamba haitawezekana kulitembelea kikamilifu muda wa kampeni, tutaweza kuacha nakala moja ya trakti Habari za Ufalme kwa watu wasiokuwako tangu tu ziara yetu ya kwanza.
7 Kusudi Letu ni Nini? Makutaniko yanapaswa kujitahidi kugawa trakti zote Habari za Ufalme ambazo yalipokea katika eneo lao lote kabla ya mwisho wa kampeni, Desemba 14. Ikiwa eneo la kutaniko letu ni kubwa na kwamba si hatari kuhubiri mwenyewe badala ya kuwa wawili, tutaona labda inafaa kutenda hivyo. Hilo litatuwezesha kutangaza habari njema kwa watu wengi zaidi iwezekanavyo wenye kustahili. (Mt. 10:11) Linaweza kuwa jambo la akili kuwa na nakala fulani za trakti ambazo tutalinda mkononi na kuwa na Biblia mfukoni mwetu au katika mfuko wetu mdogo wa mkononi, badala ya kutumia mfuko mkubwa. Tuwe wangalifu ili kuandika sawasawa kupendezwa kulikoamshwa.
8 Je! Sisi ni Tayari Kuanza? Wazee watakadirisha mapema ni magazeti ngapi ya ziada kutaniko litahitaji na watafanya ombi kutokana na hilo. Si lazima kufanya ombi la trakti Habari za Ufalme kwa kuwa furushi itatumwa kwa kila kutaniko. Mapainia wa pekee, wa kawaida na wasaidizi watapata kila mmoja trakti 250 za kugawa, lakini wahubiri watapokea kila mmoja nakala 50. Tuna kazi nyingi. Je! sisi ni wenye kugonja kwa hamu kushiriki katika utendaji huo wenye kuchangamsha? Bila shaka! Hivyo basi tutoe kwa ujumbe wa Biblia wa trakti Habari za Ufalme Na. 35 ugawaji mkubwa zaidi iwezekanavyo!