Je! Sisi Ni Mashahidi Wa Wakati Wote?
1 Je! tungeweza kujibu kwa kusema ndiyo kwa ulizo hilo? Hakika, watumishi wote wa Yehova walio wakfu hawawezi kuingia katika huduma ya wakati wote, lakini je! si jambo la akili kutazamia kwamba kila mmoja kati yetu ajione kuwa Shahidi wa wakati wote? Bila shaka.
2 Hakuna Mkristo aliye wa nusu-wakati. Akizungumza juu ya Baba yake, Yesu alisema: “Sikuzote mimi hufanya mambo yale yanayompendeza.” (Yn. 8:29, TUM) Paulo, aliyekuwa katika mwelekeo huohuo, alituhimiza ‘kufanya mambo yote kwa utukufu wa Mungu.’ (1 Kor. 10:31) Kila mmoja wetu angepaswa hivyo kuona kwamba yeye ni Shahidi wa Yehova wa wakati wote. Hilo litakuwa na uvutano mzuri katika utendaji wetu wote.
3 Tuchunguze Mambo ya Hakika: Mvalio wetu, maneno yetu na mwenendo wetu, yote hayo yanaweza kufunua kwa wengine kwamba sisi ni Mashahidi wa Yehova. Tunatambua ulazima wa kuwa na mvalio wenye kiasi, maneno safi na mwenendo mzuri wakati tunapohubiri au tunapohudhuria kwenye mikutano ya Kikristo. Hata hivyo, iwe shuleni, kazini au katika vidumbuizo, yote yangepaswa kuonyesha kwamba tunaheshimu kanuni za haki za Yehova katika maisha yetu.
4 Yesu alisema: “Mji uliojengwa juu ya mlima hauwezi kufichika. . . . Ni lazima mwanga wenu uangaze mbele ya watu, ili wayaone matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.” (Mt. 5:14-16, HNWW) Hilo lingepaswa kuonekana katika mambo yote tunayofanya, kwa kila wakati. Ikiwa tunafikia kuona kwamba hatuko tayari kutoa ushuhuda kwa sababu ya mahali tunapopatikana au kwa sababu ya yale tunayofanya, tunapaswa kujiuliza: ‘Je! mimi ninamtumikia Yehova kwa wakati wote au kwa nusu ya wakati?’ Basi na tusiweze kamwe kujisikia wenye kulazimika kupitisha nafasi ya kuzungumza na wengine habari njema ya Ufalme wa Mungu!
5 Tukumbuke kwamba tunamheshimu Yehova na tunamfurahisha ikiwa, kwa ulizo “Je! wewe ni Shahidi wa wakati wote?” tunaweza kujibu bila kusita: “Ndiyo!”