Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/03 uku. 7
  • Barua Kutoka Kwa Baraza Linaloongoza

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Barua Kutoka Kwa Baraza Linaloongoza
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mlango Mkubwa Kuelekea Utendaji Umefunguliwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Hubiri Habari Njema kwa Hamu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • “Niko Safi Kutokana Na Damu ya Watu Wote”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • “Uendelee Kusema na Usinyamaze”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 2/03 uku. 7

Barua Kutoka Kwa Baraza Linaloongoza

NI jambo lenye kupendeza kama nini kuwaandikia! Tunawapongeza kwa upendo na roho ya kujinyima mnayoendelea kuonyesha. Mtaona kutokana na kurasa za kitabu-mwaka hiki kwamba mambo mengi mazuri yalitimizwa mnamo mwaka wa utumishi uliopita. Mara nyingine tena, tumetumia zaidi ya saa bilioni moja katika kazi ya kuhubiri na kufundisha, tukitia watu moyo moja kwa moja wamkaribie Yehova. Je, si jambo la heshima kuwa wafanyakazi wenzi wa Mungu wetu mtukufu na Baba yetu wa mbinguni?—1 Kor. 3:9.

Tunapotazama kazi iliyoko mbele, tuna hakika kwamba mtaendelea kuiga bidii na imani ya watumishi wa Mungu, kama inavyofafanuliwa katika Biblia. Mtume Paulo, kwa mfano, alikuwa na nia ya kuwa mwenye matokeo zaidi iwezekanavyo katika kuendeleza faida za Ufalme. Yaonekana kwamba aliandika barua yake ya kwanza kwa kutaniko la Kikristo la Korintho katika mwaka wa mwisho aliokaa katika Efeso. Kuhusu mipango yake ya karibu, aliandika: “Ninakaa katika Efeso mpaka msherehekeo wa Pentekoste; kwa maana nimefunguliwa mlango mkubwa uongozao kwenye utendaji, lakini kuna wapingaji wengi.”—1 Kor. 16:8, 9.

Paulo alikuwa amepanga kusafiri kwenda Makedonia na Korintho. Hata hivyo, alitambua nafasi ya kufanya kazi yenye mafaa sana kwa kubaki kwa muda katika Efeso. Paulo hakuwa mshupavu; aliona hali yenye kufaa ambayo katika hiyo angeweza kuendeleza faida za Ufalme mahali alipokuwa hasa, naye akarekebisha programu yake kulingana na hali hiyo. Mlango mkubwa unaoongoza kwenye utendaji ulikuwa umefunguliwa kwake, na Paulo alikuwa na hamu ya kutumia vizuri nafasi hiyo ili kuingia kupitia mlango huo.

Kufanya hivyo kungeomba kazi nyingi—kuhubiri habari njema na kujenga kutaniko la Efeso. Baadaye Paulo aliambia wanaume wazee wa kutaniko katika mji ule: “Sikuepuka kuwaambia nyinyi lolote kati ya mambo yaliyokuwa yenye kuleta faida wala kuwafundisha nyinyi hadharani na kutoka nyumba hadi nyumba. Lakini nilitoa ushahidi kikamili kwa Wayahudi na Wagiriki pia juu ya toba kuelekea Mungu na imani katika Bwana wetu Yesu.”—Mdo. 20:20, 21.

Vivyo hivyo, wengi wenu ndugu na dada wapendwa mmetumia vizuri nafasi zilizojitokeza kwenu. Mnamo mwaka wa utumishi uliopita, kwa wastani, wahubiri 798,938 waliweza kupanga mambo yao ili kushiriki katika sehemu fulani ya huduma ya upainia. Wamoja wenu wamesafiri mpaka miisho ya dunia ili kutumikia wakiwa wamishonari. Mnaeneza habari njema kwa bidii na kujenga makutaniko. Wengine wenu mmejifunza lugha nyingine ili mweze kusaidia watu wanaosema lugha ya kigeni wanaokaa katika ujirani. Na bado wengine wamepanga mambo yao ili kutumika katika maeneo yasiyogawiwa au kutumikia mahali ambapo kuna uhitaji mkubwa zaidi. Wengine hata wameona kwamba mlango mkubwa wa utendaji umefunguliwa shuleni, kazini, au katika hali nyingine ambazo katika hizo ushahidi wenye matokeo ungeweza kutolewa, kama vile kwa njia ya simu. Mambo yaliyoonwa kutoka ulimwenguni pote yanashuhudia kwamba watu wa Mungu, vijana na wazee, wanatafuta kwa shauku na wanapata nafasi za kutoa ujuzi wa kweli kwa watu kila mahali.

Iweni hakika kwamba Yehova anaona na anathamini sana jitihada zenu. Biblia inasema: “Mungu si asiye mwaminifu ili asahau kazi yenu na upendo mlioonyesha kwa ajili ya jina lake.” (Ebr. 6:10) Endeleeni kuwa macho ili kuona nafasi zinazowaruhusu kuendeleza ibada safi. Wengine wenu wanaweza kupanua huduma yao. Sisi sote tunaweza kujitahidi kufanya huduma yetu kuwa yenye matokeo zaidi.

Hatutimizi utume wetu wa kuhubiri bila upinzani. Kumbukeni kwamba baada ya Paulo kusema kuhusu mlango mkubwa uliofunguliwa kwake na unaoongoza kwenye utendaji, aliandika: “Kuna wapingaji wengi.” Kwa Paulo, wapingaji hao walitia ndani Wayahudi na Wasio Wayahudi, wale ambao walimshambulia moja kwa moja na wengine ambao kwa ujanja walifanya njama dhidi yake.—Mdo. 19:24-28; 20:18, 19.

Tunapambana na hali hiyohiyo leo. Kwa kuwa tunakaribia uharibifu wa mfumo huu mbovu, tunatazamia upinzani wenye kuongezeka. Shetani anajaa “hasira kubwa,” na hasira hiyo inaelekezwa moja kwa moja kwa wale wanaotumikia Mungu. (Ufu. 12:12) Msisahau kamwe kwamba Shetani ndiye “mtawala wa ulimwengu.” Yesu aliambia wanafunzi wake: “Kama mngekuwa sehemu ya ulimwengu, ulimwengu ungependa sana kilicho chao wenyewe. Sasa kwa sababu nyinyi si sehemu ya ulimwengu, bali nimewachagua nyinyi kutoka ulimwengu, kwa ajili ya hili ulimwengu huwachukia nyinyi.”—Yn. 14:30; 15:19.

Tunaazimia kutoruhusu yeyote aregeze imani yetu katika Mungu au apunguze mwendo wetu katika kazi ya kuhubiri. Tunajua kwamba kutaendelea kuwa wale wanaotushambulia na kufanya njama dhidi yetu. Lakini, tunasonga mbele katika kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme, tukiwa na uhakika kwamba Yesu ataponda Shetani na majeshi yake kwa wakati wenye kufaa wa Yehova. Wapinzani hawakumnyamazisha mtume Paulo; wala hawanyamazishi watumishi wa Yehova leo. Ijapokuwa hasira ya Shetani na chuki ya ulimwengu, roho ya Yehova inafanya kazi kwa nguvu kati ya watu Wake. Ni furaha kama nini kujua kwamba hesabu ya wale wanaotangaza habari njema imefikia kilele kipya cha wahubiri 6,304,645!

Sala yetu ni kwamba mwendelee kutumia nafasi zinazojitokeza ili kuendeleza faida za Ufalme mtukufu wa Yehova. Iweni hakika kwamba tunapendezwa na kila mtu binafsi huku tukifanya kazi ‘bega kwa bega’ katika utumishi wa Mungu Aliye Juu Zaidi, Yehova.—Zef. 3:9, NW.

Ndugu zenu,

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine