Kuwatafuta Watu Wanaosema Luga Fulani
1. Katika eneo ambamo watu wanazungumuza luga mbalimbali, sababu gani kila kutaniko linapewa mugawo wa kuhubiria kikundi cha watu wanaozungumuza luga fulani?
1 Kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33, wanafuzi wa Yesu walipopokea roho takatifu ‘walianza kusema katika luga tofauti’ na wale ambao walitoka katika maeneo ya mbali ya dunia. (Mdo. 2:4) Matokeo yalikuwa nini? Watu karibu 3000 walibatizwa. Inaonekana kama labda wengi kati ya wageni hao, walikuwa wanazungumuza luga ya Kiebrania ao Kigiriki. Hata hivyo, Yehova alitaka wahubiriwe ujumbe wa Ufalme katika luga yao ya kuzaliwa. Bila shaka, ikiwa Yehova alifanya hivyo sababu moja ni kwamba watu wanapohubiriwa habari njema katika luga yao ya kuzaliwa wanakubali haraka habari njema. Kwa hiyo, katika eneo ambamo watu wanazungumuza luga mbalimbali, kila kutaniko linapewa mugawo wa kuhubiria kikundi cha watu wanaozungumuza luga fulani. (Tengenezo, uku. 107, fu. 2-3.) Vikundi vinavyotumia luga za kigeni havipewe eneo, lakini vinahubiria watu wanaozungumuza luga yao katika eneo la kutaniko linalosimamia vikundi hivyo na makutaniko mengine katika ujirani.
2. (a) Kazi ya kuwatafuta watu wanaosema luga fulani inaweza kufanywa katika maeneo gani? (b) Namna gani makutaniko yanaweza kusaidiana katika maeneo ambamo watu wanazungumuza luga mbalimbali? (c) Tunaweza kufanya nini ikiwa tunakutana mutu anayependezwa lakini anazungumuza luga nyingine?
2 Ikiwa munaishi katika eneo ambamo watu wanasema luga moja, munaweza tu kuhubiri nyumba kwa nyumba. Lakini, hali ni tofauti ikiwa munaishi katika eneo ambamo watu wanazungumuza luga mbalimbali. Makutaniko yanayotumia luga zinazozungumuzwa na watu wa eneo lenu yanaweza kuhubiri katika eneo lenu. Hata ikiwa makutaniko hayo yanaweza kuwapatia maelezo kuhusu watu fulani wanaozungumuza luga fulani katika eneo lenu, ni daraka la kutaniko lenu ao kikundi cha kutaniko lenu kuwatafuta watu ambao mutahubiria katika luga ya kutaniko lenu. (Ona kisanduku “Tusaidiane.”) Kwa hiyo, munaweza kupanga kazi ya kuwatafuta watu wanaosema luga fulani na kutafuta kujua mahali ambapo wanaishi. Kazi ya kuwatafuta watu wanaosema luga fulani inaweza kufanywa namna gani?
3. Ni mambo gani yanayopaswa kufikiriwa kuhusu mahali ambapo kutaniko ao kikundi cha kutaniko kitawatafutia watu wanaosema luga fulani na ni kiasi gani cha wakati kitatumiwa ili kutimiza kazi hiyo?
3 Jinsi ya Kupanga Kazi ya Kuwatafuta Watu Wanaosema Luga Fulani: Kujua wakati gani utapitishwa katika kazi ya kuwatafuta watu hao kunategemea hali za eneo lenu. Kwa mufano, munaweza kujiuliza, ni watu ngapi katika eneo letu wanazungumuza luga hiyo? Kuna wahubiri wangapi katika kutaniko? Kutaniko ao kikundi cha kutaniko kimekwisha kuwa na adresi ngapi za watu hao? Si lazima kutaniko litumie kiasi kilekile cha wakati ili kuwatafuta watu hao katika kila eneo, lakini linaweza kutumia wakati mwingi zaidi kwa kutafuta katika sehemu za eneo zilizo na watu wengi zaidi na ambazo haziko mbali. Hata hivyo, ni lazima kupanga vizuri kazi ya kuwatafuta watu ili watu wengi iwezekanavyo wapewe nafasi ya kuliitia jina la Yehova.—Rom. 10:13, 14.
4. (a) Kazi ya kuwatafuta watu inapaswa kupangwa namna gani? (b) Ni njia gani mbalimbali munazoweza kutumia ili kuwapata wale wanaozungumuza luga ya kutaniko lenu?
4 Ili kuepuka kufanya kazi mara mbili mahali ambapo kazi ya kuwatafuta watu inahitajiwa, wazee, zaidi sana mwangalizi wa utumishi, wanapaswa kupanga na kusimamia kazi hiyo. (1 Kor. 9:26) Katika kikundi kinachotumia luga ya kigeni, ndugu anayestahili, zaidi sana muzee ao mutumishi wa huduma aliyechaguliwa na baraza la wazee la kutaniko linalosimamia kikundi hicho, anaweza kusimamia kazi hiyo. Makutaniko mengi, ao vikundi vingi, yamechukua mipango ya kuwatafuta kwanza watu hao, labda kwa kutumia kitabu chenye kuwa na majina ya watu na adresi zao za telefone ao za Internete ili kukusanya majina ya watu wanaosema luga fulani. Hivyo, kazi ya kuwatafuta watu hao inafanywa kupitia telefone ao kwa kutembelea watu hao ili kujua ni adrese gani zinapaswa kuongezwa katika eneo. Ikiwa inafaa kufanya hivyo, baraza la wazee linalosimamia kikundi fulani, linaweza kufanya mipango ili, mara kwa mara, kutaniko lote lishiriki katika kazi ya kuwatafuta watu.—Ona kisanduku “Jinsi ya Kuwapata Wale Wanaosema Luga ya Kutaniko Lenu.”
5. (a) Ni mapendekezo gani fulani ambayo wahubiri wanatolewa wanapofanya kazi ya kuwatafuta watu wanaosema luga fulani? (b) Tunaweza kusema nini tunapofanya kazi ya kuwatafuta watu wanaosema luga fulani?
5 Tunapaswa kuwa na kusudi fulani wakati tunashiriki katika kazi ya kuwatafuta watu. Kwa kuwa utendaji huo ni sehemu ya huduma yetu, kwa kawaida ni lazima tuvalie vizuri kama wakati wahubiri wanapofanya kazi ya kuhubiri. Wahubiri wengi wametambua kwamba kufanyia mazoezi mambo ambayo watasema, na kusema luga hiyo wanapowatafuta watu hao kunawasaidia waendelee kuwa na bidii na kuongea luga hiyo vizuri. Tunaweza kuhesabu wakati tunaopitisha katika kazi ya kuwatafuta watu, lakini hatuweze kuhesabu wakati tunaopitisha kwa kutayarisha karte ya eneo na kutafuta majina ya watu. Tunapopata mutu anayezungumuza luga fulani, tunapaswa kujikaza kumuhubiria habari njema; kisha hapo na bila kuchelewa, tumujulishe mwangalizi wa utumishi ao mutu aliyechaguliwa naye ili mutu huyo aongezwe kwenye majina ya watu walio katika eneo wanaozungumuza luga hiyo. Mutafanya hivyo iwe mutu huyo alionyesha kupendezwa ao hapana. Hata ikiwa kazi ya kuwatafuta watu ni ya lazima, tunapaswa kuwa na usawaziko; tusikose kushiriki katika kila sehemu ya mahubiri.—Ona kisanduku “Mambo Tunayoweza Kusema Tunapowatafuta Watu Wanaosema Luga Fulani.”
6. Kazi ya kuwatafuta viziwi ina matatizo gani ya kipekee?
6 Kuwatafuta Viziwi: Kazi ya kuwatafuta viziwi ina matatizo yake ya kipekee na inaomba jitihada na uvumilivu. Kiziwi haweze kutambulishwa kwa kutaja jina lake, kwa alama fulani za mwili, ao namna anavyovalia. Pia, watu wa familia yake na marafiki wanaweza kuogopa, na hivyo wanasita kutolea wahubiri habari kumuhusu. Mapendekezo yanayofuata kuhusu kazi ya kuwatafuta viziwi yanaweza pia kusaidia tunapowatafuta wale wanaosema luga fulani.
7. (a) Namna gani viziwi wanaweza kutafutwa? (b) Namna gani tunaweza kumusaidia musikilizaji wetu asiwe na wasiwasi?
7 Makutaniko na vikundi vinavyotumia luga ya ishara yamepata matokeo mazuri kwa kutafuta viziwi. Labda musikilizaji wako amekwisha kuona jirani fulani, mufanya kazi mwenzake, ao mwanafunzi mwenzake akitumia luga ya ishara. Labda amekwisha kuona alama fulani imewekwa barabarani ili kuonyesha mutu anayetembeza motokari ao moto kwamba katika ujirani kuna watoto ambao ni viziwi. Labda mutu fulani wa familia yake ni kiziwi. Kumbuka kama ziara yako inaweza kutiliwa shaka. Lakini, unaweza kumusaidia musikilizaji wako asiwe na wasiwasi, kwa kuzungungumuza naye kwa njia ya kirafiki na kusema mambo machache, kwa kuwa wazi, na kufasiria mambo kwa heshima. Wahubiri fulani wamepata matokeo mazuri kwa kuonyesha Biblia ao DVD zingine za luga ya ishara wanapotaka kujua ikiwa musikilizaji anajua mutu fulani aliye kiziwi. Hivyo, wanasema tu kama wangependa kuzungumuza na viziwi kuhusu habari yenye tumaini ambayo inapatikana katika Biblia. Ikiwa musikilizaji anasita kukutolea habari kuhusu kiziwi, labda anaweza kukubali kuchukua namba zako za telefone na adresi yako ao mualiko unaoonyesha mikutaniko ya kutaniko lenu ili avitolee mutu wa familia yake ao rafiki yake ambaye ni kiziwi.
8. Namna gani kutaniko jirani linaweza kusaidia kutaniko linalotumia luga ya ishara?
8 Mara moja ao mara mbili kwa mwaka, kutaniko linalotumia luga ya ishara linaweza kuomba kutaniko jirani la luga tofauti liwasaidie kutafuta katika moja ya miji iliyo katika eneo lao lenye watu wengi. Mukutano kwa ajili ya mahubiri unaoongozwa na kutaniko linalotumia luga ya ishara unaweza kutia ndani maagizo kuhusu kazi hii, na pia onyesho. Kila kikundi kinaweza kusindikizwa na muhubiri mumoja wa kutaniko linalotumia luga ya ishara na wanaweza kupewa karte inayoonyesha sehemu ambamo kazi ya kutafuta watu itafanywa.
9. Namna gani kazi ya kuwatafuta viziwi inaweza pia kufanywa mahali ambapo viziwi wanazoea kukutana ili wajifurahishe ao kupokea misaada?
9 Kazi ya kuwafuta viziwi inaweza pia kufanywa mahali ambapo viziwi wanazoea kukutana ili wajifurahishe ao kupokea misaada. Wahubiri wanapaswa kavalia mavazi yanayoambatana na hali. Inaweza kuwa vizuri zaidi kuongea na mutu mumoja ao wawili walio hapo na kufanya hivyo kwa busara kuliko kuzungumuza na kikundi chote. Ikiwa mazungumuzo yanakuwa na matokeo mazuri, labda munaweza kupeana adresi zenu na kuona namna munaweza kuonana tena.
10. Namna gani wahubiri wanaweza kutafuta viziwi kwenye sehemu za biashara zilizo katika eneo lenu?
10 Jambo lingine linaloweza kufanywa ni kutayarisha karte inayoonyesha sehemu za biashara zilizo katika eneo, na hivyo kupanga kuhubiri eneo hilo wakati unaofaa. Kwenye karte moja kunaweza kuwa sehemu zilizo na station za essence. Kwenye karte nyingine kunaweza kuonyeshwa mahali palipo mashine za kukausha nguo, mashine za kufulia, restaurant, hoteli, ao aina nyingine za biashara. Ikiwa kila karte inaonyesha aina ileile ya biashara, wahubiri wanaweza kutumia njia ileile na kupata uzoefu na ufundi. Kwa mufano, kwa kuwa mara nyingi hoteli zinapokea pia wageni walio viziwi, tunaweza kumuelezea kwa kifupi yule anayepokea watu kwenye hoteli kuhusu kazi yetu na kumupatia furushi iliyo na DVD na mialiko kuhusu mikutano ya kutaniko ili hoteli iwe inawapatia wageni viziwi. Kwenye sehemu zingine za biashara tunaweza tu kuuliza ikiwa kuna wafanya kazi ao watu wanaokuja hapo kwa kawaida wanaotumia luga ya ishara. Ikiwa kuna masomo ya viziwi katika eneo, tunaweza kutoa vichapo vyetu fulani vilivyo kwenye DVD kwa ajili ya biblioteke ya masomo hayo.
11. Sababu gani kazi ya kuwatafuta watu wanaosema luga ya fulani ni sehemu ya lazima sana ya mahubiri?
11 Kazi ya Lazima: Kuwapata watu wanaosema luga ya kutaniko lenu inaweza kuwa kazi yenye kuchukua wakati. Pia, kwa sababu watu ni wenye kuhamahama, jambo hilo linaweza kufanya hali ya eneo lenu ibadilike kuhusu watu wanaosema luga fulani, na hivyo inaomba kubadilisha-badilisha karte ya eneo na majina ya watu. Hata hivyo, katika maeneo mengi sana, kazi ya kuwatafuta watu wanaozungumuza luga fulani ni sehemu ya lazima sana ya mahubiri. Kazi hiyo inaonyesha kama Yehova, ambaye ametupa mugawo wa kuhubiri, hana ubaguzi. (Mdo. 10:34) ‘Mapenzi yake ni kwamba watu wa namna zote waokolewe na kupata ujuzi sahihi wa kweli.’ (1 Tim. 2:3, 4) Kwa hiyo, acheni basi tutumike pamoja na Yehova na ndugu na dada zetu ili kupata watu wa luga zote walio na ‘moyo muzuri na mwema.’—Lu. 8:15.
[Sanduku katika ukurasa wa 5]
Tusaidiane
Ikiwa kutaniko ao kikundi kingetaka kusaidiwa ili kupata wale wanaozungumuza luga ya kutaniko lao, mwangalizi wa utumishi anaweza kukutana na wazee wa makutaniko jirani yanayotumia luga zingine. Inaweza kuwa vizuri zaidi kukutana na makutaniko yasiyo mbali na eneo letu ao ambayo yana watu wengi wanaozungumuza luga hiyo. Makutaniko yatakayokutana yanaweza kujulisha wahubiri wao kwamba ikiwa wanapata mutu fulani anayezungumuza luga hiyo fulani, basi wanapaswa kuandika adresi yake na kumutolea mwangalizi wa utumishi, ambaye ataitolea kutaniko ao kikundi kinachotumia luga hiyo. Waangalizi wa utumishi wa makutaniko yanayohusika watajifunza namna fulani inayofaa ya kuhubiri eneo lililo na watu wanaosema luga mbalimbali na kuwaongoza watu wenye kupendezwa kwenye kutaniko ao kikundi kinachotumia luga wanayosema na kusikia.
Ikiwa wahubiri wanakuta mutu anayesema luga nyingine na anaonyesha kupendezwa kabisa (ao kiziwi), lazima wajaze bila kuchelewa fomu Tafazali Fuatia Upendezi (S-43) na kuipatia mwandishi wa kutaniko. Jambo hilo litasaidia mutu huyo apate musaada wa kiroho kwa haraka.—Soma km 5/11 uku. 3.
[Sanduku katika ukurasa wa 6]
Jinsi ya Kuwapata Wale wanaosema Luga ya Kutaniko Lenu
• Uwaulize watu wengine: wanafunzi wa Biblia, watu wa familia, wanafunzi wenzako, na wengine.
• Tumia kitabu cha adresi za telefone ili kupata majina ambayo yanatumiwa sana katika luga fulani. Kitabu chenye kuwa na adresi za telefone ao za internete na majina ya watu kinaweza kupatikana kwenye Internete ao kwenye kompanyi ya mambo ya telefone.
• Kwa busara, uliza mahali ambapo watu wengi wanafika, kwa mufano, kwenye biblioteke za kwenu, biro za serikali, na kwenye masomo mbalimbali.
• Chunguza katika magazeti ya habari mahali penu ili kujua matangazo kuhusu kazi zinazotolewa na watu wanaosema luga ya kigeni.
• Tembelea kwenye magaze na mahali pa biashara katika eneo lenu ambapo watu wanaozungumuza luga ya kigeni wanakuja kununua vitu wanavyohitaji.
• Ikiwa unaruhusiwa na wale wanaosimamia kazi, uweke meza iliyo na vitabu vyetu mahali pa biashara, kwenye université, ao vituo vya motokari ambako watu wanaosema luga ya watu munaotafuta wanazoea kufika.
• Ikiwa inaruhusiwa na sheria katika inchi yenu, ununue kitabu kilicho na adresi za telefone na majina ya watu ao programe ya ordinatere inayoweza kukusaidia kupata maeneo yaliyo na watu wengi kwenye internete.
[Sanduku katika ukurasa wa 7]
Mambo Tunayoweza Kusema Tunapowatafuta Watu Wanaosema Luga fulani
Ikiwa munasema kwa njia ya kirafiki na kwa njia iliyo wazi, tutasaidia wasikilizaji wasiwe na wasiwasi. Mara nyingi, kuwaonyesha kwanza kitabu katika luga yao kunasaidia.
Kisha kumusalimia mutu, unaweza kusema: “Tunatafuta watu wanaosema luga ya ______ ili tuwaelezee habari yenye kuletea tumaini inayopatikana katika Biblia. Je, unajua mutu fulani anayesema luga hiyo?”
Munapowatafuta viziwi, unaweza kusema: “Jambo. Naweza kukuonyesha jambo fulani, tafazali? [Tumia mashine ya video ya mukononi, umusikilizishe andiko fulani katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya—kwenye DVD.] Hiyo ni andiko la Biblia katika Luga ya Ishara ya Amerika. Zaidi ya Biblia, tuna video zingine zinazotayarishwa ili kuwasaidia viziwi wamujue Mungu. Hautalipa feza ili kuzipata. Je, unajua mutu fulani ambaye ni kiziwi, ao aliye na magumu ya kusikia na ambaye anatumia luga ya ishara?” Ikiwa musikilizaji wako hajue hata mutu moja, unaweza kumuuliza ikiwa anakumbuka mahali ambapo alimuona kiziwi, kwa mufano, kwenye kazi, kwenye masomo, ao katika ujirani wake.