Tufanye Kupendezwa Kulikoamshwa Na Trakti Habari Za Ufalme Kuzae Matunda
1 Tangu majuma fulani, tunayo furaha na pendeleo la kugawa trakti Habari za Ufalme Na. 35 yenye kichwa: “Je! Kuna Wakati Ambao Watu Wataweza Kupendana?” Kila mahali, wahubiri wanajitahidi kuacha trakti hiyo kwa watu wengi zaidi “wanaostahili.” (Mt. 10:11, TUM) Kampeni hiyo inapaswa kumalizika kwa kawaida Siku ya Yenga Desemba 14, lakini ikiwa kunabaki eneo la kutembelea, wazee watatuomba labda kuendeleza ugawaji wa trakti Habari za Ufalme Na. 35 hadi stoki ya kutaniko itakapomalizika.
2 Chapa hiyo ya trakti Habari za Ufalme inaamsha kupendezwa kwa watu wengi. Wanatambua kwamba shauku ya asili imetoweka kwa walio wengi wa watu wa wakati wetu, pia wanajiuliza wakati ujao utakuwa namna gani. (2 Tim. 3:3) Kupendezwa huko ambako kumetokea, tunataka kukufanya kuzae matunda.
3 Ugawaji wa Trakti Habari za Ufalme Unazaa Matunda Yake: Wakati wa kampeni iliyopangwa katika 1995, mwanamke mmoja aliyepokea trakti Habari za Ufalme alikuja kuhudhuria mkutano kwenye Jumba la Ufalme ili kujua mengi zaidi juu ya imani ya Mashahidi wa Yehova. Alikubali papo hapo kwa furaha funzo la Biblia na, baadaye, ni mara haba alikosa mkutano. Muda mdogo baada ya hapo, akafutisha jina lake katika orodha ya kanisa lake.
4 Leo, mamia ya watu katika eneo letu wamekwisha kusoma ujumbe unaotolewa na trakti Habari za Ufalme Na. 35. Lakini wameitikiaje? Hata ikiwa waliguswa moyo na yale waliyosikia, wengi hawatafanya lolote isipokuwa Shahidi wa Yehova awatembelee tena. Je! tumepanga kurudi kuwaona? Kumjali kwetu jirani, kunakosukumwa na upendo, kunapaswa kutuchochea kufanya hivyo. Wale wote walioonyesha kupendezwa na trakti Habari za Ufalme wanapaswa kutembelewa tena.
5 Tutasema Nini Wakati wa Ziara Yetu ya Pili? Tungeweza kusema maneno machache juu ya habari zinazovuma sasa za ujumbe uliomo ndani ya trakti Habari za Ufalme, na kutoa swali lenye kufanya mtu afikiri. Tusikilize kwa makini msikilizaji wetu ili tuelewe undani wa wazo lake. Baadaye, tuvutie uangalifu wake juu ya wazo moja lenye kufaa la broshua Anataka, linalotolewa katika trakti Habari za Ufalme. Ikiwa mtu anaitikia vizuri, tujaribu kuanzisha papo hapo funzo la Biblia.
6 Hizi ni baadhi ya njia za kuanzisha mazungumzo mara ya pili na watu walioonyesha kupendezwa na trakti “Habari za Ufalme” Na. 35:
◼ “Unakumbuka labda kichapo kidogo nilichokuachia wakati wa nyuma. Yaliyomo yanazungumzia tatizo kubwa lililo chanzo cha migawanyiko kati ya watu: ukosefu wa upendo kwa wengine.” Kwa kutegemeza wazo hilo tutaje mambo yaliyoonwa yanayoripotiwa kwenye ukurasa wa 2 wa trakti Habari za Ufalme, chini ya kichwa kidogo “Upendo kwa Jirani Umepoa.” Tuulize basi: “Je! unafikiri Mungu anatazamia kwamba watu waishi hivi?” Tusikilize jibu. Tufungue broshua Anataka kwenye somo 5 na tujaribu kuanzisha funzo la Biblia.
◼ “Tulipokutana mara ya kwanza, nilikuachia trakti iliyouliza: ‘Je! Kuna Wakati Ambao Wanadamu Wataweza Kupendana?’ Je! unafikiri kwamba hilo lawezekana ulimwenguni pote?” Tusikilize jibu. Tufungue broshua Anataka kwenye somo 6 na tusome fungu la 6. Tusome baadaye ahadi inayotolewa na Mungu katika Mika 4:3, 4. Ikiwa msikilizaji wetu anaonekana kuwa mwenye kupendezwa, tumtolee broshua na funzo.
◼ “Mara ya mwisho tulipoonana, nilikuachia trakti yenye kichwa: ‘Je! Kuna Wakati Ambao Wanadamu Wataweza Kupendana?’ Ndani yake ina toleo kwa ajili ya funzo la Biblia la nyumbani pasipo malipo. Nimerudi kukuona ili nikuonyeshe kitabu cha kibiblia ambacho tunatumia [Tuonyesha kitabu Ujuzi.] Kitabu hiki kinafasiria waziwazi wakati gani tunaweza kutumaini kuona watu wakipendana wamoja na wengine, na kinajibu maswali ambayo labda unajiuliza: Kwa nini uzee na kifo? Sababu gani Mungu huruhusu kuteseka? Inakuwaje kwa wapendwa wetu tunaopoteza?” Kisha tuulize: “Je! ninaweza kukuonyesha namna gani funzo hilo linavyoendeshwa?” Ikiwa mtu anakataa toleo letu, tumuulize ikiwa anapendelea kujisomea mwenyewe kitabu. Ikiwa ndivyo anavyotaka, tumuachie nakala moja na tumfasirie kwamba kazi yetu ya ulimwenguni pote ya elimu ya Biblia inategemezwa na michango ya kujipendea. Tupange ziara itakayofuata.
7 Wakati eneo lote litakapokuwa limetembelewa kwa msaada wa trakti Habari za Ufalme Na. 35, tutaweza kutolea kitabu Ujuzi kwa siku za mwezi zinazobaki. Ili kukitolea, tunaweza kupata mawazo mengi kwenye ukurasa wa mwisho wa Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni 1996; Julai na Desemba 1996; na Julai 1997.
8 Ugawaji wa trakti Habari za Ufalme ni nafasi kwa kila mmoja wetu kuongeza bidii yake katika mahubiri. Tukisaidiwa na Yehova, tunaweza kuwa hakika na mafanikio ya kampeni hiyo: itawawezesha watu kujua kwamba kusudi la Yehova ni kwamba watu wapendane wamoja na wengine. Yehova na aendelee kubariki jitihada zetu zote za kufanya kupendezwa kulikoamshwa na trakti Habari za Ufalme kuzae matunda!