Tuhangaikie Kwelikweli Kila Kupendezwa
1 Hivi karibuni, kazi ya ulimwenguni pote ya mahubiri itamalizika; baadaye, wale “wasiomjua Mungu” watapata uharibifu. (2 Thes. 1:7-9) Hilo ndilo linalowachochea watu wa Yehova, wanaohangaikia kwelikweli uhai wa wengine, kujulisha ujumbe wa Ufalme kwa watu zaidi iwezekanavyo.—Zef. 2:3.
2 Kila mwezi, mamilioni ya saa zinafanywa kwa kuwatafuta wale wanaotaka kusikiliza “habari njema ya mambo mema.” (Is. 52:7, UV) Wakati tulipowatolea toleo la mwezi, wengi walikubali nakala ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! au broshua Mungu Anataka Nini Kwetu? Tutaonyesha kwamba tunahangaikia kwelikweli watu hao kwa kuwa haraka kufuatia kila kupendezwa kulikoonyeshwa.—Mez. 3:27.
3 Tuandike Mambo Kikamilifu: Tutafanya kazi nzuri kabisa ikiwa tunaandika kikamilifu mambo yote ya kupendezwa kulikoonyeshwa na kichapo tulichoacha. Maelezo kama vile jina na anwani ya mtu, siku na saa ya kupita kwetu, kichapo tulichoacha na kichwa cha habari tulichozungumzia vitatusaidia kuwa zaidi wenye matokeo wakati tutakapokwenda kumuona. Tuandike pia maneno yake fulani aliyotoa muda wa mazungumzo ya kwanza; yatatufaidi ili kurudilia upya mazungumzo wakati wa ziara ya kurudi.
4 Turudi Kuwaona Watu Haraka: Ni wangapi kati ya wale ulioachia vichapo mwezi wa nyuma ulijaribu kuwarudilia? Je! majuma yalipita bila kuweko na kuonana tena? Ikiwa tunahangaikia kwelikweli wokovu wa milele wa watu hao, tutarudi kuwaona haraka iwezekanavyo, vizuri zaidi katika siku fulani zinazofuata, wakati mazungumzo yangali bado yanakumbukwa akilini mwao. Ni kwa kufuatia haraka kupendezwa kwamba tunaweza kumtangulia Shetani, ambaye “huja na kuliondoa neno lililopandwa ndani yao.”—Mk. 4:15, TUM.
5 Kujitayarisha ni kwa Lazima: Matokeo mazuri katika ziara za kurudia yanategemea moja kwa moja ubora wa kujitayarisha kwetu. Kabla ya kwenda, tufikiri namna tutakavyoanza mazungumzo na mtu. Ukurasa wa mwisho wa Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 1997 una utoaji mbalimbali wa magazeti na broshua Anataka ambao tunaweza kutumia kwa furaha. Baadaye, tuwe akilini na mawazo fulani ambayo tungependa kutoa wakati wa ziara ya kurudia. Tunaweza kusema nini ili kuitikia kupendezwa? Jinsi gani kuanzisha funzo la Biblia?
6 Ili kuendeleza mazungumzo muda wa hayo tulitaja kile kingehitajiwa ili kusafisha dunia na kuifanya kuwa mahali pazuri pa kuishi, tungeweza kusema:
◼ “Mara ya mwisho, tulikubaliana kwamba, ili kwamba dunia ingeuke kuwa Paradiso yenye amani, ingefaa hatua zenye nguvu zichukuliwe. Je! unafikiri kwamba wanadamu wana sifa zinazohitajiwa kwa ajili ya hilo? [Tuache mtu ajibu.] Angalia kwa nini inafaa kwamba awe Mungu tu ndiye anayeingilia mambo ya wanadamu.” Tusome Zaburi 37:38, kisha tujielekeze kwenye somo 5 la broshua Anataka na tuchague sehemu za mafungu 4-5 zinazoonyesha jinsi Mungu atatimiza unabii huo. Tumalize kwa kupendekeza funzo la Biblia kwa msaada wa broshua.
7 Ikiwa tulizungumza juu ya Ufalme na kuacha broshua “Anataka” wakati wa kupita kwa mara ya kwanza, tungeweza kurudi kumuona mtu kwa kumuambia maneno kama haya:
◼ “Wakati wa mazungumzo yetu ya mwisho, tuliona kwamba Ufalme wa Mungu ni serikali halisi itakayotawala dunia yote. Biblia inaonyesha kwamba Yesu Kristo ndiye atakayekuwa mkuu wayo. Je! una wazo fulani juu ya faida zitakazoletwa na serikali kama hiyo na mkuu kama huyo?” Tuache mtu ajibu. Tufungue broshua Anataka kwenye somo 6. Kwa msaada wa nukta fulani zilizochaguliwa katika mafungu 6-7 na picha ya ukurasa 13, tuonyeshe yale Ufalme wa Mungu utafanyia wanadamu. Tusome Danieli 2:44 na, ikiwa hilo linafaa, tutolee kitabu Ujuzi na tupendekeze funzo la Biblia.
8 Ikiwa mtu ambaye tulikutana naye alitambua kwamba dini za ulimwengu ndizo chanzo cha matatizo ya wanadamu, tumuulize kwa mfano yafuatayo wakati wa ziara ya kurudia:
◼ “Je! haujajiuliza kamwe jinsi gani ya kutambua dini inayokubaliwa na Mungu? [Tuache mtu ajibu.] Katika broshua hii, Mungu Anataka Nini Kwetu?, mnapatikana alama zinazowezesha kutambua dini ya kweli.” Tujielekeze kwenye somo 13 na tutokeze nukta tano zinazoandikwa katika italiki (maandishi yenye kulazwa) za mafungu 3-7. Kisha tunaweza kuendelea hivi: “Kupata dini ya kweli ni jambo la muhimu, lakini imetupasa pia kutafuta kujua kile Mungu anaomba kwa kila mmoja wetu.” Tusome Yohana 4:23, 24. Tupendekeze kuzungumzia hilo kwa urefu zaidi. Tuchukue somo 1 la broshua na tuonyeshe jinsi funzo la Biblia linavyoendeshwa.
9 Ili kuendeleza mazungumzo kuhusu furaha ya familia, tunaweza kuongozwa na haya yafuatayo:
◼ “Mara ya kwanza tulipoonana, nilikufasiria kwamba siri ya furaha ya familia ilikuwa ni kutumikisha mashauri ya Neno la Mungu, Biblia. Kwa maoni yako, je! Biblia inaweza kutosheleza mahitaji ya familia ya kisasa, au ni ya kale?” Tuache mtu ajibu. Tutolee kitabu Ujuzi. Tukifungue kwenye sura 2 na tusome nukulu la fungu 13. Tumtolee funzo la Biblia la kifamilia kwa kutumia hoja za fungu 3.
10 Kwa kuandika mambo kikamilifu, kwa kutayarisha vizuri na kwa kurudi haraka kuwaona watu ili kukomaza kupendezwa kwao, tutaonyesha upendo wa jirani, upendo utakaowavuta kwenye njia ya wokovu.—Mt. 22:39 ; Gal. 6:10.