Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp20 na. 1 uku. 3-5
  • Namna ya Kupata Kweli

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kupata Kweli
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • UNAWEZA KUPATA KWELI?
  • NAMNA UNAWEZA KUPATA KWELI
  • KITABU CHA PEKEE CHA KUTUSAIDIA KUPATA KWELI
  • ‘Endelea Kutembea Katika Kweli’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • “Nitatembea Katika Kweli Yako”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
  • Ungependa Kujua Kweli?
    Ungependa Kujua Kweli?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
wp20 na. 1 uku. 3-5
Mwanaume mumoja iko anatafuta kitabu kimoja kwenye kabati yenye kujaa vitabu

Namna ya Kupata Kweli

Kujua kweli kunaweza kuokoa uzima wetu. Kwa mufano, fikiria faida yenye tumepata mu maisha yetu kwa kujua jibu la ulizo hili, Namna gani magonjwa yenye kuambukiza inafikia kuenea?

Kwa maelfu ya miaka, hakuna mwenye alijua kabisa jibu la ile ulizo. Wakati huo, mapigo na magonjwa yenye kuenea haraka sana iliua mamilioni ya watu. Mwishowe, wanasayansi walijua kweli. Walivumbua kama mara mingi magonjwa ililetwa na mikrobe, ni kusema, viumbe vidogo-vidogo sana, kama vile bakteria ao virusi. Kujua ile kweli kulisaidia watu wazuie na kutunza magonjwa mingi, jambo lenye limesaidia mamiliare ya watu waishi miaka mingi na wakuwe na afya ya muzuri.

Tuseme nini juu ya maulizo ingine ya maana? Unajua faida yenye unaweza kupata kwa kujua kweli ya maulizo yenye kufuata?

  • Mungu ni nani?

  • Yesu Kristo ni nani?

  • Ufalme wa Mungu ni nini?

  • Wakati wenye kuja utakuwa namna gani?

Mamilioni ya watu wamepata majibu ya ile maulizo na wamefanya maisha yao ikuwe muzuri zaidi. Wewe pia, majibu ya ile maulizo inaweza kukuletea faida.

UNAWEZA KUPATA KWELI?

Pengine unaweza kujiuliza, ‘Inawezekana namna gani kupata kweli juu ya kila jambo?’ Kwa kweli, imeanza kuonekana kuwa ni nguvu sana kupata kweli kuhusu mambo mingi. Juu ya nini?

Watu mingi hawatumainie serikali, mambo ya biashara, ao vituo vya kutangaza habari ili kuwaambia kweli. Wanaona kama ni nguvu kujua ikiwa watu wako wanasema mambo ya kweli ao ikiwa wako wanatoa tu maoni yao, kwa kuficha habari fulani, ao hata kudanganya. Juu watu hawatumainiane na juu habari mingi haziko za kweli, watu hawakubali ile yenye inaweza kuwa kweli kabisa, na hata faida yenye inaweza kuwaletea.

Hata kama kuko ile magumu, inawezekana kupata majibu ya kweli ku maulizo ya maana sana katika maisha. Namna gani? Kwa kufanya namna unazoeaka kufanya ili kupata majibu ya maulizo ingine yenye haiko ya maana sana.

NAMNA UNAWEZA KUPATA KWELI

Kwa njia fulani, unatafuta kweli kila siku. Tufikirie hali ya Jessica. Anasema hivi: “Mwili wa mutoto wangu mwanamuke unakataa kabisa kalanga hivi kwamba hata kiasi kidogo sana cha proteine ya kalanga kinaweza kumuua.” Jessica anapaswa kuwa hakika kama chakula chenye ananunua hakitaletea mutoto wake hatari. “Jambo la kwanza lenye ninafanyaka, ni kusoma kwa uangalifu maandishi yenye kuonyesha kila kitu chenye kilitumiwa ili kutengeneza chakula hicho. Kisha ninatafuta habari zingine juu ya chakula hicho ao hata kuita wale wenye walikitengeneza ili wanihakikishie kama proteine fulani ya kalanga haikuingia ndani bila wao kujua. Pia, ninachunguza habari zingine zenye kuwa hakika zenye kuonyesha namna ile kompanyi inatengenezaka chakula chao. Ile inanisaidia nikuwe hakika.”

Uleule mwanaume iko anasoma kitabu chenye alikamata kwenye kabati ya vitabu na iko analinganisha mambo yenye kuwa ndani na yenye alipata katika chombo chake cha kielektroniki

Wakati Jessica anatafuta kweli, anafanya vile kwa uangalifu sana; pengine kwako haiko vile. Lakini kama vile Jessica, unaweza kutumikisha njia zenye kufuata ili kupata majibu ku maulizo yako:

  • Tafuta ukweli wa mambo.

  • Tafuta habari zaidi.

  • Uhakikishe kama habari zenye umepata ni za kweli.

Kufanya vile kunaweza kukusaidia kupata majibu ya kweli ku maulizo ya maana sana mu maisha. Namna gani?

KITABU CHA PEKEE CHA KUTUSAIDIA KUPATA KWELI

Wakati Jessica alikuwa anatafuta kweli ya Biblia, alitumia njia yenye kufanana na ile yenye anatumiaka wakati anatafuta habari juu ya chakula chenye kufaa kwa mutoto wake. Anasema hivi: “Kusoma kwa uangalifu na kufanya utafiti kwa bidii kulinisaidia nipate kweli katika Biblia.” Kama Jessica, mamilioni ya watu wamejifunza mambo yenye Biblia inasema juu ya maulizo yenye kufuata:

  • Juu ya nini tuko ku dunia?

  • Inakuwa namna gani wakati mutu anakufa?

  • Juu ya nini watu wanateseka?

  • Mungu iko anafanya nini ili kumaliza mateso yote?

  • Namna gani familia yetu inaweza kuwa na maisha yenye furaha?

Mwanaume uleule iko anasoma Biblia wakati ordinatere yake iko wazi

Unaweza kupata majibu ya kweli ya ile maulizo na ya maulizo ingine kwa kusoma Biblia na kwa kutafuta habari zaidi ku site yetu ya www.jw.org.

Gazeti hili la Munara wa Mulinzi litajibia maulizo yenye kufuata:

  • Mungu ni nani?

  • Yesu Kristo ni nani?

  • Ufalme wa Mungu ni nini?

  • Wakati wenye kuja utakuwa namna gani?

Kwanza, tuone ni juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama Biblia ni kitabu chenye kinaweza kutusaidia kupata kweli.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine