Programu ya mikutano ya utumishi
Juma Toka Julai 10
Wimbo 7
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Toa maelezo kuhusu ripoti ya utumishi wa shambani ya Novemba 1999 ya nchi na ya kutaniko lenu. Vuta uangalifu juu ya kisanduku “Tazama Ukurasa wa Mwisho,” na mfanye onyesho la utoaji mmoja kati ya zile zilizopendekezwa, ambao unaweza kuwa wenye matokeo katika eneo lenu.
Dak. 15: “Hatuwezi Kuacha Kusema.” Fanya maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu. Kazia kwa nini tunachukua mgawo wetu wa kuhubiri kwa uzito sana. Tia ndani nukta zenye kupatana na habari hii kutoka katika Mnara wa Mlinzi wa Januari 15, 1997, kurasa 23-4.
Dak. 18: “Acheni Mambo Yote Yatukie kwa Ajili ya Kujenga.” Wazee wawili wanazungumzia makala. Someni kila fungu na maandiko yanayotajwa. Kazieni uangalifu juu ya kanuni zinazohusika. Tieni mkazo juu ya uhitaji wa kuwa na utambuzi wakati wa kushughulika na mambo ya kibiashara au kutoa fedha kwa ajili ya kupata faida. Rudilieni shauri katika Mnara wa Mlinzi wa Machi 15, 1997, kurasa 18-19, 22.
Wimbo 15 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Julai 17
Wimbo 23
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya akaunti. Eleza kwa kifupi jinsi ya kutumia broshua Jina la Mungu ili kusaidia mtu mwenye kupendezwa atambue uhitaji wa kujua na kutumia jina la kibinafsi la Mungu.—Ona kitabu Kutoa Sababu, kurasa 425-6.
Dak. 10: “Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko.” Maulizo na majibu. Tangaza tarehe ya kusanyiko la mzunguko lijalo, na uwahimize wote wahudhurie siku zote mbili. Tia wote moyo wafanye jitihada ya pekee ili kualika wanafunzi wa Biblia. Kuhudhuria kusanyiko kunaweza kuharakisha tamaa yao ya kushirikiana kikawaida na kutaniko.
Dak. 20: Ni Nani Unayepaswa Kuiga? Baba mmoja anaongoza funzo la familia pamoja na mtoto mmoja au wawili matineja. Ameona karibuni kwamba mazungumzo yao mara nyingi yanahusu mabingwa wa michezo, wachezaji wa sinema, watu mashuhuri kwenye televisheni, na wanamuziki. Anaonyesha hangaiko kwa kuwa aina hiyo ya mvutio ni wonyesho wa roho ya ulimwengu. Wanazungumzia Amkeni! ya Mei 22, 1998, kurasa 12-14. Vijana hao wanatambua kwamba kuna hatari katika kuabudu watu wa ulimwengu na wanakubali kwamba kujulikana sana ulimwenguni hakutolei Wakristo jambo lolote. Wanafikiria faida za kuona wazazi, wazee, watu wengine wenye mfano wa kuigwa katika kutaniko—na hasa Yesu Kristo—kuwa watu ambao wao wanapaswa kuiga.
Wimbo 34 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Julai 24
Wimbo 45
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: Kujipendekeza Wenyewe Kama Wahudumu wa Mungu. Watumishi wa huduma wawili wanazungumzia shauri la Kimaandiko linalotolewa katika Mnara wa Mlinzi wa Desemba 15, 1998, kurasa 19-20. Wanatambua uhitaji wa kujistahilisha kwa njia yenye kufaa kama watumishi wa huduma na wanarudilia yale ambayo wanaweza kufanya kibinafsi ili kuonyesha kwamba wanatimiza migawo yao. Wanaona umaana wa kuwa mifano mizuri katika huduma ya shambani na wanazungumzia njia ambazo katika hizo wanaweza kusaidia wazee katika kutoa msaada wa kibinafsi kwa wengine. Wanakubali kwamba wanataka kufanya yote wanayoweza ili kusaidia kutaniko litambue uharaka wa nyakati na kukomaa na kusitawi kiroho.
Dak. 10: Kuandikia Barua Watu Tusioweza Kukutana Nao. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Kwa kuwa inaendelea kuwa vigumu kukuta watu nyumbani, wahubiri fulani hupata matokeo mazuri kwa kuandika barua. Fikiria miongozo ifuatayo. Barua zinapaswa kuwa fupi, zenye msingi wa Kimaandiko, na zenye adabu. Usitume barua zisizokuwa na jina la mtu aliyeziandika. Andika vizuri, kwa mkono au kwa mashini, na kwa namna inayoweza kusomeka vizuri. Toa anwani ya Jumba la Ufalme na saa za mikutano ya kutaniko pamoja na karatasi ya mwaliko ili kuhudhuria. Usitumie anwani ya Sosaiti. Rudilia madokezo yanayotolewa katika kitabu Kiongozi cha Shule, kurasa 87-9, na Majibu kwa Maulizo Yenu kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Desemba 1996.
Dak. 15: Tumia Utoaji Wenye Matokeo. Chagua matangulizi mawili au matatu kutoka kurasa 9-15 za kitabu Kutoa Sababu, na uzungumzie jinsi hizo zinavyoweza kutumiwa kwa matokeo katika eneo lenu. Uliza wasikilizaji: “Ni matangulizi gani mnayotumia wakati mnapokaribia mtu fulani barabarani, ki-vivi-hivi, au kwa njia nyingine?” Fanyeni onyesho la utangulizi mmoja au mawili kadiri wakati unavyoruhusu.
Wimbo 54 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Julai 31
Wimbo 66
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wote watoe ripoti za utumishi wa shambani za Julai. Omba wasikilizaji waeleze mambo waliyojionea wenyewe ambayo walifurahia mwezi huu wakati walipokuwa wakigawa broshua.
Dak. 12: Mahitaji ya kutaniko.
Dak. 18: “Je, Wewe Unathamini Uvumilivu wa Yehova?” Maulizo na majibu. Tia ndani maelezo yenye kupatana na habari kuhusu uvumilivu wa Yehova.—Ona Étude Perspicace, Buku 2, kurasa 499-500.
Wimbo 75 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Agosti 7
Wimbo 88
Dak. 10: Matangazo ya kwenu.
Dak. 17: “Je, Wewe Ni Mtu Mwenye Haya?” Maulizo na majibu. Eleza jambo moja lililoonwa lenye kutia moyo kutoka katika Kitabu-Mwaka 1997, kurasa 43-4.
Dak. 18: Uwe Mwenye Hekima Katika Wakati Wako Ujao. Hotuba inayotolewa na mzee. Vijana hutaka kuwa na wakati ujao wenye furaha pamoja na wale wanaowapenda. Ingawa hilo ni jambo la kawaida, wanapaswa kutumia shauri la kimungu ikiwa wanataka kufanikiwa. (Mez. 19:20) Uvutano kuelekea kwa watu wa jinsia tofauti ni wenye nguvu katika ujana. Ikiwa hisia hazizuiliwi, tokeo linaweza kuwa msiba. Maulizo mengi hutokea kuhusu hekima ya matineja ambao huanza kuvutwa kimoyoni na watu wa jinsia tofauti, wakisitawisha uhusiano wa kimahaba ambao huongoza kwenye mapatano ya kukutana kati ya wavulana na wasichana. Rudilia shauri linalotolewa katika kitabu Vijana Huuliza, kurasa 231-5. Kazia nukta kubwa katika Mnara wa Mlinzi wa Novemba 15, 1999, kurasa 18-23, ambao unaonyesha umaana kwa vijana kutimiza wajibu wao wote kwa Mungu. Tia vijana moyo watafakari shauri hilo na kulizungumzia pamoja na wazazi wao ikiwa wana maulizo.
Wimbo 101 na sala ya kumalizia.