Programu ya mikutano ya utumishi
Juma Toka Oktoba 9
Wimbo 11
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 12: “Fikirieni Kazi za Ajabu za Mungu.” Fanya maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu. Onyesha picha chache katika kile kitabu kipya, picha ambazo zinajenga uthamini kuelekea unabii wa Isaya.
Dak. 25: “Mileani Mpya—Wakati Ujao Unakuwekea Nini Wewe?” Mazungumzo yenye shauku yakiongozwa na mwangalizi wa utumishi. Baada ya kusoma tangazo linalotolewa katika barua ya Sosaiti ya Julai 3, 2000, kwa wazee, gaweni nakala moja ya Habari za Ufalme Na. 36 kwa kila mhudhuriaji. Kisha, anzeni mazungumzo ya maulizo na majibu ya makala. Onyesha mipango iliyochukuliwa mahali penu ili kutembelea eneo lote. Fikirieni jinsi ya kusaidia wapya na watoto wajifanye wawe wenye sifa za kuwastahilisha kuwa wahubiri wasiobatizwa. Fanyeni onyesho la utoaji mfupi. Kazieni uhitaji wa kila mmoja kushiriki katika kampeni hii.
Wimbo 53 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Oktoba 16
Wimbo 104
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya akaunti. Kumbusha wahubiri kwamba wakati wa utendaji kwenye mwisho-juma, magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yanapaswa kutolewa pamoja na Habari za Ufalme Na. 36.
Dak. 15: Vyombo Vyenye Kuelimisha, Vyenye Kuchochea, na Vyenye Kutia Nguvu. (Mafungu 1 na 2 tu.) Hotuba. Rudilia kwa kifupi historia ya kuingia kwa Sosaiti katika utoaji wa vidio. (Ona kitabu Wapiga-Mbiu, kurasa 600-601.) Tia kila mmoja moyo atazame vidio Les Témoins de Jéhovah — Un non, une orgranisation ili kujitayarisha kwa ajili ya mazungumzo kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma toka Oktoba 30. Wale walio na vidio hiyo wanaweza kuishiriki na wengine wasiokuwa nayo, au labda wanaweza kuitazama pamoja.
Dak. 20: Sisi Sote Tunaweza Kuonyesha Roho ya Upainia. Mazungumzo kati ya kiongozi wa funzo la kitabu na msaidizi wake, yakiwa na msingi juu ya Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 15, 1997, kurasa 22-3. Zungumzieni kwa nini lingekuwa jambo lenye kutia moyo kuwa na mapainia wengi zaidi katika kutaniko, na jinsi wote wanavyoweza kuchangia katika kufikia mradi huo. Zungumzieni pia jinsi ya kutia moyo wale ambao ni mapainia sasa waendelee, na jinsi wote katika kutaniko wanavyoweza kuendeleza bidii katika huduma.
Wimbo 131 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Oktoba 23
Wimbo 150
Dak. 10: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko.
Dak. 20: Jitayarishe Kikamili kwa Ajili ya Mikutano. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Faida tunayopata kutokana na mikutano inategemea kwa kiasi kikubwa jitihada tunazofanya katika kujitayarisha. Rudilia madokezo yenye kutumika yanayotolewa katika Mnara wa Mlinzi wa Machi 1, 1998, kurasa 15-16, mafungu 8-11. Omba wasikilizaji watoe maelezo yenye kuonyesha jinsi wanavyochukua hatua yenye kuhitajiwa, na kupata wakati wa kujitayarisha vizuri.
Wimbo 211 na sala ya kumalizia
Juma Toka Oktoba 30
Wimbo 167
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Oktoba.
Dak. 12: Mambo yaliyoonwa katika kutolea watu Habari za Ufalme Na. 36. Omba wahubiri mbalimbali waeleze matokeo yenye kutia moyo ambayo wamepata mpaka sasa katika kugawa Habari za Ufalme Na. 36. Omba mapainia wa kawaida na wasaidizi waeleze jinsi wanavyothamini ule utendaji wenye kuongezeka muda wa kampeni hii na nafasi waliyo nayo ya kutumika pamoja na wahubiri wengi mbalimbali.
Dak. 25: Les Témoins de Jéhovah — Un non, une organisation. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Chunguzeni yale maulizo yanayotolewa katika fungu 3 la makala “Vyombo Vyenye Kuelimisha, Vyenye Kuchochea, na Vyenye Kutia Nguvu.” Toa madokezo kuhusu jinsi vidio hiyo inavyoweza kutumiwa ili kusaidia wale wenye kupendezwa wapate kufahamiana vizuri na tengenezo letu. Tia ndani jambo moja au mawili yaliyoonwa.—Ona Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 1, 1992, kurasa 30-1.
Wimbo 15 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Novemba 6
Wimbo 198
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Rudilia maendeleo ya ugawaji wa Habari za Ufalme Na. 36. Toa ripoti kuhusu ukubwa wa eneo ambalo limetumikwa mpaka sasa na kile kitakachohitajiwa ili kumaliza kutembelea eneo lote kufikia Novemba 17.
Dak. 20: Sisi Tunaamini Nini? Ndugu mmoja anafanya ziara ya kurudia kwa mtu aliyeuliza, “Mashahidi wa Yehova wanafundisha nini ambalo linawafanya kuwa tofauti na dini nyinginezo?” Zungumzia nukta zinazotolewa katika kisanduku kwenye ukurasa 6 wa Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 1, 1998. Eleza jinsi dini nyinginezo zinavyopuuza au kutupilia mbali kweli hizo za Biblia za msingi na kupendelea mafundisho yaliyotungwa na watu.
Dak. 10: Kuimba—Sehemu ya Maana ya Ibada Yetu. Kiongozi wa funzo la kitabu anaongea na wahubiri wawili kuhusu kuimba kwao kwenye mikutano ya kutaniko. Ametambua kwamba kuimba kwao kunaonekana kwa njia fulani kuwa kwenye kukosa nguvu. Anashiriki nao nukta fulani kutoka katika Mnara wa Mlinzi wa Novemba 1, 1999, kurasa 22-4. Wanachanganua maneno ya wimbo moja kati ya zile zitakazoimbwa kwenye Funzo la Mnara wa Mlinzi juma hili, kama inavyodokezwa katika Mnara wa Mlinzi wa Julai 1, 1999, ukurasa 20, fungu 12. Kwa kuchukua kuimba kwa uzito, tunafanya maneno yetu yenye kutoka moyoni ya sifa kwa Yehova yawe hai.
Wimbo 223 na sala ya kumalizia.