Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/02 uku. 1
  • Tuungane kwa Furaha na Yehova na Mwana Wake

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuungane kwa Furaha na Yehova na Mwana Wake
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Juu ya Nini Tunahuzuriaka Ukumbusho?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Kukumbuka Kwa Shukrani Fidia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Yehova Anabariki Bidii Yetu ya Kuhuzuria Ukumbusho
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • “Endeleeni Kufanya Hivi kwa Kunikumbuka Mimi” Kifo cha Yesu Kitaazimishwa Tarehe 2 mwezi wa 4
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 3/02 uku. 1

Tuungane kwa Furaha na Yehova na Mwana Wake

Tukio la Maana Zaidi Mwakani Litaadhimishwa Mnamo Machi 28

1 Kwa kuadhimisha Chakula cha Jioni cha Bwana baada ya jua kutua mnamo Machi 28, 2002, tutaonyesha kwamba tunaungana kwa furaha na Yehova Mungu na Yesu Kristo. Kwenye tukio hilo la pekee sana, mabaki ya Wakristo watiwa-mafuta watafurahia “ushirika” wa pekee walio nao pamoja na warithi wengine wa Ufalme, pamoja na Baba, na pamoja na Mwana wake. (1 Yn. 1:3; Efe. 1:​11, 12) Mamilioni ya “kondoo wengine” watatafakari juu ya pendeleo lao zuri ajabu la kuungana na Yehova na Mwana wake, wakiwa na moyo mmoja na akili moja nao katika kutimiza kazi ya Mungu!​—Yn. 10:16.

2 Tutumike Pamoja Katika Uhusiano wa Karibu: Yehova na Yesu wamekuwa sikuzote wenye kuungana kwa furaha. Kabla ya mtu kuumbwa, walifurahia ushirika wa karibu kwa kipindi kirefu sana cha wakati. (Mika 5:2) Hivyo, kifungo chenye kina kirefu cha shauku nyororo kilisitawi kati yao wawili. Akiwa mfano wa hekima alipokuwa akiishi kabla ya kuwa mwanadamu, Mwana huyo mzaliwa-pekee angeweza kusema: “Nilikuwa . . . furaha yake [Yehova] kila siku, nikifurahi siku zote mbele yake.” (Mez. 8:​30) Kupitisha miaka isiyo na hesabu katika ushirika wa karibu na Chanzo cha upendo kulikuwa na uvutano wenye kina kirefu juu ya Mwana wa Mungu!​—1 Yn. 4:8.

3 Alipofikiri juu ya uhitaji ambao wanadamu walikuwa nao wa ukombozi, Yehova alichagua Mwana wake mzaliwa-pekee, ambaye aliwapenda sana wanadamu, ili atoe dhabihu ya ukombozi, inayotutolea tumaini bora tulilo nalo. (Mez. 8:​31) Kama vile tu Yehova na Mwana wake wanavyoungana katika kutimiza kusudi moja, tunabaki wenye kuungana nao na wenye kuungana na wenzetu katika vifungo vya upendo vyenye nguvu, tukifanya mapenzi ya Mungu kwa furaha.

4 Tuonyeshe Uthamini Wetu Wenye Kutoka Moyoni: Kwa kuhudhuria Ukumbusho na kwa kusikiliza kwa uangalifu na kwa heshima, tunaweza kuonyesha uthamini wetu wa kweli kuhusu upendo wa Yehova na dhabihu ya Mwana wake kwa ajili yetu. Mambo yatakayokaziwa ni mfano wa Yesu wenye upendo, uaminifu wake mpaka kifo katika kutoa ukombozi, na utawala wake akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu uliosimamishwa, na pia baraka ambazo Ufalme huo utaletea wanadamu. Tutakumbushwa pia uhitaji wa kuonyesha imani yetu kwa kuendelea, tukifanya kazi kwa bidii kwa kupatana na mapenzi ya Yehova tukiwa “wafanyakazi wenzi katika kweli.”​—3 Yn. 8; Yak. 2:​17.

5 Tusaidie Wengine Washiriki Pamoja Nasi: Baraza la wazee linapaswa kufanya jitihada ya pekee ili kutia moyo Mashahidi wote wasiotenda walio katika eneo ili wahudhurie Ukumbusho wa kifo cha Kristo. (Mt. 18:​12, 13) Fanyeni orodha ya wale wanaopaswa kutembelewa kusudi wote waalikwe kibinafsi, na yeyote asisahauliwe.

6 Je, mnajua wengine wanaoweza kuja kwenye Ukumbusho? Chukueni hatua ya kujenga uthamini wao kuhusu tukio hilo. Waalikeni kwa shauku, na mwafanye wajisikie kuwa wenye kukaribishwa. Acheni tufanye yote tuwezayo ili kualika kwenye tukio hili la maana zaidi mwakani wanafunzi wetu wote wa Biblia na watu wengine wenye kupendezwa, na pia washiriki wa familia na watu tunaojuana nao. Faida za ukombozi zinaendelea kupatikana kwa wote wanaojifunza “thamani iliyo bora zaidi ya ujuzi wa Kristo Yesu.” (Flp. 3:8) Wale wanaojizoeza imani katika dhabihu ya Kristo wanaweza kupata tumaini thabiti la uzima wa milele.​—Yn. 3:​16.

7 Msipuuze kamwe uvutano ambao Ukumbusho unaweza kuwa nao juu ya watu wanyofu. Miaka miwili iliyopita katika kisiwa cha Papouasie-Nouvelle-Guinée, watu 11 wenye kupendezwa walisafiri katika mashua ndogo kwa saa 17 kupitia bahari zenye dhoruba ili kuhudhuria Ukumbusho. Kwa nini? Walisema: “Tulitaka kusherehekea Ukumbusho wa Kristo pamoja na waabudu wenzetu wa Yehova; kwa hiyo, safari yetu ilikuwa yenye kufaa.” Fikiria bidii iliyoonyeshwa na watu hao wenye kupendezwa, na uthamini wao kuhusu kuungana kwa furaha na Yehova, Mwana wake, na undugu wa Kikristo!

8 Toeni funzo la Biblia kwa wale wote wenye kupendezwa. Watieni moyo wahudhurie mikutano ya kutaniko kwa ukawaida na kushiriki na wengine kweli wanazojifunza. Wasaidieni ‘watembee katika nuru’ na ‘kuzoea kweli’ kwa kutumikisha kanuni za Biblia katika maisha yao. (1 Yn. 1:​6, 7) Wasaidieni wasitawishe uhusiano wa karibu pamoja na Yehova na kuendelea kukomaa katika uthamini kuhusu pendeleo la kufanya mapenzi yake kwa umoja.

9 Ni pendeleo zuri ajabu kama nini kuungana kwa furaha “katika roho moja, kwa nafsi moja mkipigana sambamba kwa ajili ya imani ya habari njema”! (Flp. 1:​27, 28) Na tutazamie ushirika wetu wenye kupendeza kwenye Ukumbusho mnamo Machi 28, tukiwa wenye shukrani sikuzote kwa Yehova na Mwana wake!​—Luka 22:19.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine