Kukumbuka Kwa Shukrani Fidia
1 Ili kutii amri ya Yesu, Wakristo ulimwenguni pote watakusanyika Siku ya Posho tarehe 22 mwezi wa 3, 2008, kisha jua kutua, ili kuazimisha kifo cha Yesu Kristo. (Luka 22:19; 1 Kor. 11:23-26) Tunachochewa kufanya hivyo ili kuonyesha shukrani nyingi tuliyo nayo kuhusu yale yote yaliyotimizwa siku hiyo, kumekwisha kupita miaka 1,975. Kwa kubaki mwaminifu mshikamanifu alipoteswa na kuuawa kwenye mti wa mateso, Yesu alitakasa jina la Baba yake, akitoa jibu nzuri sana kuhusu uchokozi wa Shetani.—Ayu. 1:11; Met. 27:11.
2 Damu ya Yesu iliyomwangika ilitambulisha haki ya agano jipya, na kufanya iwezekane kwa wanadamu wasio wakamilifu wakubaliwe kuwa wana wa Mungu wakiwa na tumaini la kutawala pamoja na Kristo katika Ufalme wake wa mbinguni. (Yer. 31:31-34; Marko 14:24) Zaidi ya hayo, upendo mwingi wa Mungu kuelekea wanadamu ulionyeshwa waziwazi alipotoa Mwana wake mpendwa kuwa zabihu, kama vile Yesu mwenyewe alivyomwelezea Nikodemo.—Yoh. 3:16.
3 Alika Wengine: Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi wa 1 ilipendekeza kwamba tuandike kwenye karatasi majina ya watu tunaofahamiana nao na tutolee kila mtu kikaratasi cha mwaliko. Je, umeanza kualika watu ambao uliandika majina yao kwenye karatasi? Je, unafanya mipango ili kushiriki sana katika kampanye ya kualika watu kwenye Ukumbusho, itakayoanza tarehe 1 mwezi wa 3? Wale watakaohuzuria watafuata mafundisho ya Biblia yanayoweza kujenga imani katika fidia, fidia inayoongoza kwenye uzima wa milele.—Rom. 10:17.
4 Wote walio na uwezo watapanga kufika mbele ya wakati ili kukaribisha kwa uchangamfu wale watakaokuja kuhuzuria tukio hili la pekee. Kwa kuwa watu wengi sana wanahuzuria Ukumbusho, ni jambo la maana tuhangaikie kwa namna ya pekee wale walio wapya na wengine wanaohuzuria mikutano mara kwa mara.
5 Tayarisha Moyo Wako: Kitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2008 na Kalenda ya 2008 vina programu kuhusu usomaji wa pekee wa Biblia kwa ajili ya Ukumbusho; programu itakayoanza tarehe 17 mwezi wa 3. Unapofikiria matukio ya maana yaliyotokea katika siku za mwisho za maisha ya Yesu hapa duniani, hilo litakusaidia kutayarisha moyo wako ili kuazimisha Ukumbusho. (Ezra 7:10) Kufikiri sana juu ya habari hizo za Biblia na kusali, kutaongeza shukrani yako kuhusu upendo ambao Yehova na Mwana wake walionyesha kwa kutoa fidia.—Zab. 143:5.
6 Kwa kuwa Ukumbusho unakaribia, tujitayarishe kwa uangalifu, na kusaidia wengine wajitayarishe kwa ajili ya tukio hilo la maana. Kukumbuka kwa shukrani fidia kutafanya urafiki wetu na Yehova na Mwana wake uwe mzuri zaidi. (2 Kor. 5:14, 15) Kutatuchochea pia kufuata mfano wao kwa kuonyesha upendo wa kujitoa kwa ajili ya wengine.—1 Yoh. 4:11.
[Maulizo ya Funzo]
1, 2. Kwa nini tunapaswa kukumbuka kwa shukrani fidia?
3. Wale watakaohuzuria Ukumbusho watapata faida gani?
4. Kwa nini tunapaswa kufika mbele ya wakati kwenye Ukumbusho?
5. Namna gani unaweza kutayarisha moyo wako kwa ajili ya Ukumbusho?
6. Ni faida gani tutapata tunapojikaza kuongeza shukrani yetu kuhusu fidia?