Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/08 uku. 2
  • Programu ya Mikutano ya Utumishi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Programu ya Mikutano ya Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Vichwa Vidogo
  • Juma Tokea Tarehe 10/03
  • Juma Tokea Tarehe 17/03
  • Juma Tokea Tarehe 24/03
  • Juma Tokea Tarehe 31/03
  • Juma Tokea Tarehe 7/04
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 3/08 uku. 2

Programu ya Mikutano ya Utumishi

Juma Tokea Tarehe 10/03

Wimbo 131

Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Kwa kutumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 6 ao utoaji mwingine wowote wenye kufaa eneo lenu, fanyeni onyesho la jinsi ya kutolea watu Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1/03 na Amkeni! ya mwezi wa 3 pamoja na kikaratasi cha mwaliko kwenye Ukumbusho.

Dak. 20: Kwa Nini Tukutanike Pamoja? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yenye kutegemea Mnara wa Mlinzi wa tarehe 15/05/07, ukurasa wa 11-13. Omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu jinsi ambavyo wamefaidika kwa kuhuzuria mikutano ya kutaniko na jinsi ambavyo wameshinda vizuizi ili kuhuzuria mikutano kwa ukawaida.

Dak. 15: “Sisi Wote Tuna Kitu Fulani cha Kumtolea Yehova.”* Ikiwa wakati unaruhusu, omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko yanayotajwa.

Wimbo 8

Juma Tokea Tarehe 17/03

Wimbo 144

Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Kumbusha wahubiri walete Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1/04 na Amkeni! ya mwezi wa 4 kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma linalofuata, na wawe wamejitayarisha ili kuzungumzia utoaji mbalimbali wenye kufaa eneo lenu. Matangazo yaliyochaguliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme.

Dak. 15: Kisanduku cha Maulizo. Kitazungumziwa na mzee. Someni na kuzungumzia habari yote.

Dak. 20: “Namna Gani Tutasaidia Wale Watakaohuzuria Ukumbusho?”* Munapozungumzia fungu la 5, fanyeni onyesho fupi kuhusu jinsi ya kuanzisha funzo la Biblia na mgeni aliyehuzuria Ukumbusho.

Wimbo 214

Juma Tokea Tarehe 24/03

Wimbo 111

Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Soma ripoti ya feza na shukrani kuhusu michango.

Dak. 15: Tujitayarishe Kutolea Watu Magazeti Mapya. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Baada ya kutoa maelezo mafupi kuhusu magazeti Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1/04 na Amkeni! ya mwezi wa 4, uliza wasikilizaji habari ambazo zinaweza kuvutia watu katika eneo na kwa nini. Omba wasikilizaji waeleze mawazo fulani yaliyo katika habari wanazopanga kukazia. Ni ulizo gani linaloweza kutokezwa ili kuanzisha mazungumzo? Ni andiko gani katika habari linaloweza kusomwa? Kwa kutumia utoaji mbalimbali uliopendekezwa kwa ajili ya eneo lenu, fanyeni onyesho kuhusu jinsi ya kutolea watu Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1/04 na Amkeni! ya mwezi wa 4.

Dak. 20: Tunaleta Habari Njema za Jambo Bora. Kisha utangulizi usiopita dakika moja, mzee atatoa hotuba yenye kuchukuliwa katika Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1/07/05, ukurasa wa 18-19, fungu la 10-14. Omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu jinsi ujumbe wa Ufalme uliwatuliza na kuwatolea tumaini walipousikia kwa mara ya kwanza.

Wimbo 29

Juma Tokea Tarehe 31/03

Wimbo 37

Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti za mahubiri za mwezi wa 3.

Dak. 20: Tumieni Vizuri Kitabu cha Mwaka 2008. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Zungumzieni “Barua Kutoka Baraza Linaloongoza,” iliyo katika nyongeza, ukurasa wa 3-4. Omba watu wawili ao watatu kati ya wasikilizaji waeleze kila mmoja jambo lililoonwa alilopata katika Kitabu cha Mwaka ambalo lilimtia moyo zaidi. Fanya mipango mbele ya wakati ili mhubiri mmoja ao wawili waeleze jinsi wanavyofanya programu ya usomaji wao wenyewe wa Kitabu cha Mwaka. Malizia kwa kutia wote moyo wasome kitabu hicho tangu mwanzo mpaka mwisho. Ikiwa Kitabu cha Mwaka 2008 hakipatikani, mnaweza kutumia Kitabu cha Mwaka 2007.

Dak. 15: “Tutiane Moyo Tunapokuwa Katika Kazi ya Kuhubiri”*

Wimbo 122

Juma Tokea Tarehe 7/04

Wimbo 186

Dak. 10: Matangazo ya kutaniko lenu.

Dak. 20: Kwa Nini Unachelewesha Ubatizo Wako? Hotuba itakayotolewa na mzee, itachukuliwa katika Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1/07/06, ukurasa wa 29-30, fungu la 14-17. Tia ndani sehemu fupi ya kuuliza watu maulizo; utauliza mhubiri mmoja ao wawili waliobatizwa wakiwa na miaka kati ya 13-19. Ni nini kilichowachochea kuchukua hatua hii ya maana wakiwa bado vijana? Namna gani ubatizo wao uliwasaidia kukomaa kiroho, jambo ambalo ni ulinzi kwao?

Dak. 15: Je, Umejaribu Kuanzisha Funzo la Biblia Moja kwa Moja? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yenye kutegemea nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi wa 1, 2002, ukurasa wa 6. Zungumzieni utoaji mbalimbali wenye kupendekezwa na jinsi unavyoweza kubadilishwa ili kuanzisha funzo la Biblia katika kitabu Biblia Inafundisha. Kisha fanyeni onyesho moja ao maonyesho mawili. Tia moyo wasikilizaji wajaribu hata mara moja, katika juma linalofuata, kuanzisha moja kwa moja funzo la Biblia katika kitabu Biblia Inafundisha.

Wimbo 225

* Maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine