Biblia—Kitabu cha Historia na Unabii
Video La Bible : le livre le plus ancien toujours d’actualité ndilo onyesho la kwanza katika mfululizo wa maonyesho matatu ya video yaliyo katika DVD yenye kichwa La Bible : un livre historique et prophétique. Kisha kutazama video hiyo, jibu maulizo yanayofuata:
(1) Biblia inakubaliana na sayansi ya sasa katika njia gani? (2) Namna gani tunaweza kuwa hakika kwamba Biblia tulizo nazo leo ni sawa kabisa na maandishi ya kwanza? (3) Taja jambo kubwa la maana linalopatikana katika maandishi ya zamani ya Biblia? (4) Ni katika njia gani John Wycliffe, Johannes Gutenberg, William Tyndale, John Hus, Martin Luther, Casiodoro De Reina, na Charles Taze Russell walisaidia katika kueneza Neno la Mungu ulimwenguni pote, na namna gani dini ilipinga vikali Biblia? (5) Namna gani mashauri ya Biblia yamesaidia watu kushugulika na matatizo ya afya (Zab. 34:8), michezo ya feza (1 Tim. 6:9, 10), kutengana kwa wenzi wa ndoa, ukosefu wa uaminifu katika ndoa (1 Kor. 13:4, 5; Efe. 5:28-33), na kujishugulisha sana na mali za kimwili (Mt. 16:26)? (6) Kuna uhakikisho gani wa kwamba kutumia kanuni za Maandiko kunaweza kusaidia watu kushinda chuki ya kitaifa, ya kikabila na ya rangi ya ngozi (Luka 10:27)? (7) Ni katika njia gani kushika kanuni za Biblia kumekuletea furaha kubwa zaidi? (8) Namna gani unaweza kutumia video hii ili kusaidia wengine?—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi wa 2, 2006, ukurasa wa 8.