Matangazo
◼ Toleo la vitabu la Mwezi wa 3: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Wahubiri watafikiria kuanzisha funzo la Biblia wanapomtolea mutu kitabu hicho ao ikiwa msikilizaji amekwisha kukipata. Mwezi wa 4 na wa 5: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Munaporudilia watu wenye kupendezwa, kutia ndani wale waliohuzuria Ukumbusho ao matukio mengine ya kitheokrasi lakini hawajiunge sana na kutaniko, mujikaze kuwatolea kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? mukiwa na kusudi la kuanzisha funzo la Biblia.
◼ Mara tu munapopokea Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, munapaswa kuwagawia wahubiri magazeti hayo ili wajue habari zilizo ndani mbele ya kuzitolea watu katika mahubiri.
◼ Ukumbusho utafanywa Siku ya Pili tarehe 30 mwezi wa 3, 2010. Nyimbo zitakazotumiwa kwa ajili ya Ukumbusho ni namba 8 na 109 kutoka katika kitabu kipya cha nyimbo. Ikiwa kutaniko lenu linafanya mikutano siku hiyo, mujikaze kubadili siku ya mikutano katika juma hilo. Mahali ambapo makutaniko mengi yanafanya mikutano katika Jumba la Ufalme moja, na ni vigumu kutaniko lenu libadili siku ya mikutano, basi munaweza kuondoa mikutano juma hilo. Hivyo, sehemu za mkutano wa utumishi ambazo ni za maana sana hasa kwa kutaniko lenu zinapaswa kuingizwa katika mkutano mwingine wa utumishi.